Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Tanga kuna uwekezaji wa bomba la mafuta toka Hoima - Chongoleani, viwanda mbalimbali vya saruji, vivutio vya utalii vya Amboni Caves, Magofu ya Tongoni na Saadani National Park:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kiwanja cha ndege kikubwa na cha kisasa katika Jiji la Tanga?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kabla sijauliza swali langu la nyongeza kwanza niipongeze timu yangu ya Coastal Union ya Tanga ambayo imepanda daraja mwaka huu, lakini pia niwapongeze timu ya African Sports kwa kubakia katika ligi daraja la kwanza. Maswali yangu ya nyongeza ni kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia ukarabati unaofanywa na ambao ulishawahi kufanywa uwanja wa ndege wa Tanga, katika eneo la Magomeni kuna nyumba zaidi ya 228 ambazo zilifanyiwa evaluation mwaka 2008 lakini mpaka leo hawajalipwa. Lakini pia kuna nyumba nyingine 802 ambazo nazo zinahitajiwa kuvunjwa ili kupanua uwanja ule wa ndege.
Sasa je, nataka kujua, Serikali ni lini itawalipa Wananchi wale fidia ili kuweza kufanya ukarabati huu mkubwa unaotakiwa kufanywa kufuatia ufadhili wa Benki ya Dunia?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili, kwa kuwa Jiji la Tanga sasa hivi route za ndege zimeongezeka na kuna shughuli nyingi za mipango ya kiuchumi amabzo zinafanyika. Je, ni lini Bombadier itaanza kwenda Tanga? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, nyumba zote ambazo zilifanyiwa evaluation kwa ajili ya malipo ya fidia, shughuli za fidia zinafanyika na evaluation imekwishafanyika na tunafahamu idadi ya pesa zinazodaiwa lakini tuko kwemnye uhakiki kupitia Wizara ya Fedha ya kulipa fidia hiyo, kwa hiyo, wakati Wizara ya Fedha itakapomaliza kupitia fidia hiyo, malipo yatafanyika kwa watu ambao wataathirika na upanuzi wa uwanja wa ndege huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Bombadier itaanza lini safari za kwenda Tanga, kiutaratibu Bombadier wanafanya biashara pamoja na kutoa huduma kama mashirika mengine ya ndege kwa hiyo, hilo tutalichukua, tutawapelekea ATCL basi waje wafanye tathmini ya masuala ya soko, usalama na mambo mengine ambayo yanahusika kabla ya kupeleka ndege kufanya shughuli za safari za uwanja huo wa Tanga, ahsante.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Tanga kuna uwekezaji wa bomba la mafuta toka Hoima - Chongoleani, viwanda mbalimbali vya saruji, vivutio vya utalii vya Amboni Caves, Magofu ya Tongoni na Saadani National Park:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kiwanja cha ndege kikubwa na cha kisasa katika Jiji la Tanga?

Supplementary Question 2

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Mheshimiwa Waziri, wananchi wa Kata ya Makole, Manispaa ya Dodoma walisitishiwa uendelezaji wa nyumba zao kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege ulioko hapa wakati huo kuna wananchi wa Kata ya Msalato 89 wanaidai Serikali tangu mwaka 2005.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kujua wananchi wa Msalato watalipwa lini lakini pili wananchi wa Makole waliositishiwa uendelezaji wa nyumba zao…

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kumekuwepo na upanuzi wa uwanja wa ndege au tutautumia sasa hivi hapa Dodoma na wananchi wa Makole madai yao ya fidia yanashughulikiwa kupitia Wizara ya Fedha na sasa hivi Wizara ya Fedha wako kwenye uhakiki wa kuhakikisha kwamba wanalipa hayo madai yao wakati watakapomaliza uhakiki.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Tanga kuna uwekezaji wa bomba la mafuta toka Hoima - Chongoleani, viwanda mbalimbali vya saruji, vivutio vya utalii vya Amboni Caves, Magofu ya Tongoni na Saadani National Park:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kiwanja cha ndege kikubwa na cha kisasa katika Jiji la Tanga?

Supplementary Question 3

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri kutokana na tamko lake la juzi, Jimbo la Segerea katika Kata ya Kipawa kuna wananchi 1,800 wanasubiri malipo tangu mwaka 1992 na juzi alisema kwamba waondoke. Sasa nilitaka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini sasa atawafanyia malipo yao watu wa Kata ya Kipawa, Mtaa wa Kipunguni na wanahusika vipi kuondoka kabla hawajalipwa malipo yao?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna wananchi wanatakiwa wapishe eneo la uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere International Airport ambao walivamia miaka ya nyuma, lakini Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kwamba walipwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya hao kuna wananchi 59 ambao tayari wamekwishapokea malipo yao kwa ajili ya kupisha upanuzi wa uwanja huo. Tunaowazungumza na ambao nilitoa agizo waondoke ni hao wananchi 59 na bado naendelea kusisitiza kwamba hao wananchi 59 ambao tayari wamekwishakupokea malipo yao ya fidia, wanatakiwa waondoke wapishe upanuzi wa uwanja wetu wa ndege.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nikiri kwamba kuna baadhi ya wananchi ambao hawajalipwa kwa sababu mbalimbali, kuna baadhi walifungua kesi na kuna wengine ambao hawajafungua kesi lakini hawakuridhika na fidia, hao bado tunaendelea kutafuta utaratibu mwingine wa kuwashawishi kwa njia moja au nyingine ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja huo wa ndege.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Tanga kuna uwekezaji wa bomba la mafuta toka Hoima - Chongoleani, viwanda mbalimbali vya saruji, vivutio vya utalii vya Amboni Caves, Magofu ya Tongoni na Saadani National Park:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kiwanja cha ndege kikubwa na cha kisasa katika Jiji la Tanga?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mkoa wa Mara una shughuli nyingi sana ambazo zingeweza kuliongezea Taifa letu uchumi kwa maana ya utalii, tuna Ziwa Victoria lakini pia makumbusho ya Baba wa Taifa. Katika majibu yake Naibu Waziri ametueleza kwamba wamefanya usanifu pia kwenye uwanja wa ndege wa Musoma, ningependa kujua uwanja wa ndege wa Musoma na wenyewe upo kati ya viwanja vilivyopewa priority maana yake umetaja Tanga tu kama ndiyo umepewa kipaumbele na unaanza kukarabatiwa? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Kwenye jibu langu la msingi wakati najibu kuhusu uwanja wa ndege wa Tanga nilieleza viwanja 11 ambavyo vimeshafanyiwa Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na uwanja wa Musoma ukiwemo. Ni kweli kwamba viwanja vyote vimepewa kipaumbele kinacholingana na pesa itakapopatikana kama nilivyoeleza tutafuta mkopo kutoka Benki ya Dunia, pesa itakapopatikana basi viwanja vyote vitapewa kipaumbele kujengwa kwa sababu tunahitaji viwanka vyote vya Mikao viwe na kiwango kizuri ambacho ndege yoyote inaweza ikashuka, ahsante.