Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AZZA H. HAMAD aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka maji katika Sekondari ya Masengwa?

Supplementary Question 1

MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maji kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Mradi huu wa maji ni ahadi ya toka mwaka 2006 ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Rais Mstaafu hivyo imekuwa ni ahadi ya muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Wizara ya Maji ipo tayari sasa kuondoa vikwazo vyote vilivyopo Wizara ya Maji na kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kuhakikisha mradi huu unaanza mara moja?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwa na hofu kubwa kwa wananchi wangu wa Mji Mdogo wa Tinde kutokana na kwamba mradi wa maji wa Ziwa Victoria bomba kubwa linapita mbali sana na Mji Mdogo wa Tinde, hivyo kuwa na hofu kubwa kwamba mradi huu hautawezekana kufika kwa wananchi wa Tinde. Je, Wizara ya Maji imefikia wapi kuwaondoa hofu wananchi wa Tinde kuhakikisha kwamba wanapata maji safi na salama katika mradi huu wa mkubwa wa maji ya Ziwa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Mbunge Azza kwa jinsi ambavyo anawapenda wananchi wa Shinyanga na jinsi anavyowatetea katika Bunge hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza la Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kabisa kwamba miradi hii ilianza bajeti ya mwaka 2006/2007 na Mheshimiwa Mbunge naomba tu akumbuke ndipo tulioanza ile program ya maendeleo ya sekta ya maji, tukaweka kwamba tutajenga miradi 1,810. Tumeshakamilisha miradi 1,468, bado miradi 366 na mradi wake ukiwa ni mmojawapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, umechelewa kwa sababu usanifu ulichelewa, lakini kwa sasa tunamhakikishia kwamba hakuna vikwazo vya aina yoyote, tunatekeleza kwa mujibu wa sheria. Mradi wowote baada ya usanifu, baada ya manunuzi ili kuepuka upotevu wa fedha lazima tuupeleke kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali akaufanyie vetting, tusaini, ndiyo tuanze utekelezaji. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba mradi utatekelezwa bila ya wasiwasi wowote.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kweli bomba la KASHIWASA limepita mbali kidogo mbali na ule Mji wa Tinde, nimemwagiza Mhandisi Mshauri anayesimamia huu mradi wa Tabora na tayari ameshabaini vijiji vitakavyopelekewa maji ukiwemo Mji wote Tinde na vitongoji vyake na amekamilisha utaratibu wa awali sasa hivi tunaingia kwenye usanifu wa kina.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati tunaendelea na utekelezaji wa mradi wa Tabora basi wakati unakamilika na Tinde yote itakuwa imeshapata maji. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. AZZA H. HAMAD aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka maji katika Sekondari ya Masengwa?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba niiulize Serikali ni lini itapeleka maji kwenye Kata ya Mjele ambayo ni ahadi ya muda mrefu ya Serikali? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nitumie nafasi hii nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya na nimeshafika hadi Mjele. Namwomba sana Mhandisi wa Maji wa Jimbo la Mbeya Vijijini asilale ili kuhakikisha wananchi wale wanapata maji safi, salama na ya kuwatosheleza. Jambo la msingi sisi kama Wizara a-raise certificate tuko tayari kulipa kwa wakati ili wananchi waweze kupata maji.