Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Kutokana na tatizo kubwa la ukosefu wa maji katika Mji Mdogo wa Muze Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilipitisha mpango wake wa kuondokana na tatizo hilo kwa kuanzisha mradi mkubwa wa kuchukua maji toka Mto Kalumbaleza na kusambaza katika Vijiji vya Muze, Mlia, Mnazi Mmoja Asilia, Ilanga, Mbwilo Kalakala, Isangwa na Uzia:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kutekeleza mradi huo?

Supplementary Question 1

MHE. IGNAS A. MALOCHA. Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana. Kwanza nimpongeze Naibu Waziri na Waziri wake kwa utendaji wa kazi, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, mradi huu wa Muze Group unategemewa kupeleka maji katika vijiji 10 vyenye wakazi 40,000 ambavyo ni Kijiji cha Kalumbaleza A, B, Muze, Mbwilo, Mlia, Mnazi mmoja Asilia, Ilanga Kalakala, Izia na Isangwa. Maeneo haya hukumbwa na kipindupindu kila mwaka kutokanana na shida ya maji, mwaka huu wananchi wapatao 605 waliugua kipindupindu, katika hao wananchi 15 walikufa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuharakisha ujenzi wa mradi huu ili kunusuru vifo kwa wananchi?
Swali la pili, kwa vile Mtaalam Mshauri wa mradi huu alishaanza kazi na amesha- raise certificate Wizara ya Maji; Je, ni lini watamlipa fedha zake haraka ili mradi huu uweze kuanza mapema? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna ya kipekee anavyowatetea wananchi wake. Nataka niwahakikishie kwamba maji ni uhai, Wizara ya Maji hatutakuwa sehemu ya kupoteza uhai wa wananchi wake. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutakuwa sehemu ya kusimamia mradi huu ili uweze kutekelezeka kwa wakati wananchi wake waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge cha saa saba tukutane ili twende kuhakikisha Mkandarasi huyu analipwa kwa wakati ili mradi usikwame na wananchi waweze kupata maji. (Makofi)

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Kutokana na tatizo kubwa la ukosefu wa maji katika Mji Mdogo wa Muze Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilipitisha mpango wake wa kuondokana na tatizo hilo kwa kuanzisha mradi mkubwa wa kuchukua maji toka Mto Kalumbaleza na kusambaza katika Vijiji vya Muze, Mlia, Mnazi Mmoja Asilia, Ilanga, Mbwilo Kalakala, Isangwa na Uzia:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kutekeleza mradi huo?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Mji wa Makambako ni Mji mkubwa na ni Mji ambao una tatizo kubwa sana la maji. Baadhi ya wananchi wanashindwa kujenga viwanda kwa sababu ya uhaba wa maji. Kuna miradi 17 ya fedha kutoka Serikali ya India. Serikali iniambie hapa je, ni lini sasa miradi hii ambayo mmojawapo ni ya Mji wa Makambako utaanza ili wananchi wa Makambako waweze kunufaika na wajipange kwa ajili ya kujenga viwanda?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Mbunge wa Makambako pamoja na Ludewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na Mheshimiwa Mbunge wa Makambako, kwanza kabisa tunaishukuru Serikali kwamba mkataba wa kifedha kati ya Serikali ya India na Tanzania umeshasainiwa tayari. Pili, kulingana na masharti ya mkataba huo, Serikali ya India imeshaleta Wahandisi Washauri tayari, wengi ambao sasa hivi tutafanya manunuzi kupitia kwenye hilo group.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba shughuli hii inakwenda kwa kasi sana na matarajio yake ni kwamba kabla ya mwaka huu tulionao 2018 haujafika Desemba, tunataka tuhakikishe kwamba Wakandarasi wako site na wanaanza utekelezaji wa miradi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Ludewa. Mheshimiwa Mbunge yeye mwenyewe ni shahidi kwamba nilishaelekeza mamlaka yangu ya maji ya Iringa na wanaendelea kutekeleza miradi katika Jimbo lake na mwaka huu tumetenga fedha. Kwa hiyo, tutaendelea kutekeleza pamoja na pale Mjini ambapo mimi mwenyewe nilipatembelea, tutahakikisha kwamba tunawapatia maji safi na salama wananchi wake. (Makofi)

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Kutokana na tatizo kubwa la ukosefu wa maji katika Mji Mdogo wa Muze Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilipitisha mpango wake wa kuondokana na tatizo hilo kwa kuanzisha mradi mkubwa wa kuchukua maji toka Mto Kalumbaleza na kusambaza katika Vijiji vya Muze, Mlia, Mnazi Mmoja Asilia, Ilanga, Mbwilo Kalakala, Isangwa na Uzia:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kutekeleza mradi huo?

Supplementary Question 3

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Tatizo la maji katika Wilaya ya Ludewa limekuwa ni la kudumu na ikizingatiwa kwamba Wilaya ya Ludewa ina vyanzo vya maji vingi sana. Je, Serikali inajipangaje katika kuhakikisha kwamba Ludewa inapata maji ya uhakika hususan Ludewa Mjini na Mavanga?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Mbunge wa Makambako pamoja na Ludewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na Mheshimiwa Mbunge wa Makambako, kwanza kabisa tunaishukuru Serikali kwamba mkataba wa kifedha kati ya Serikali ya India na Tanzania umeshasainiwa tayari. Pili, kulingana na masharti ya mkataba huo, Serikali ya India imeshaleta Wahandisi Washauri tayari, wengi ambao sasa hivi tutafanya manunuzi kupitia kwenye hilo group.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba shughuli hii inakwenda kwa kasi sana na matarajio yake ni kwamba kabla ya mwaka huu tulionao 2018 haujafika Desemba, tunataka tuhakikishe kwamba Wakandarasi wako site na wanaanza utekelezaji wa miradi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Ludewa. Mheshimiwa Mbunge yeye mwenyewe ni shahidi kwamba nilishaelekeza mamlaka yangu ya maji ya Iringa na wanaendelea kutekeleza miradi katika Jimbo lake na mwaka huu tumetenga fedha. Kwa hiyo, tutaendelea kutekeleza pamoja na pale Mjini ambapo mimi mwenyewe nilipatembelea, tutahakikisha kwamba tunawapatia maji safi na salama wananchi wake. (Makofi)