Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAWA A. GHASIA) aliuliza:- Je, ni lini barabara ya uchumi kutoka Mtwara – Nanyamba – Tandahimba - Newala – Masasi, itaanza kujengwa baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri.
Swali langu la nyongeza namba moja, ni kwa nini sasa kwa kuwa, kila kitu kimekamilika na mchakato wa manunuzi umekamilika na barabara hii ni muhimu kwa usafirishaji wa korosho, ujenzi wa barabara hii usianze mara moja badala ya kusubiri mwaka wa fedha 2016/2017, hii maana yake tutaanza Julai na wakati wananchi wanasubiri ujenzi huu uanze mara moja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba Naibu Waziri atupe Kauli ya Serikali kuhusu kilometa 160 zilizobaki, kwa sababu barabara hii ina kilometa 210 na amesema ujenzi utaanza kwa kilometa 50. Naomba majibu?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ilipangiwa bajeti yake kwa mwaka huu wa 2015/2016. Kwa hiyo, kuanza ujenzi kwa mwaka huu wa fedha, fedha zake hatuna. Fedha zimepangwa kwa mwaka wa fedha ujao na naamini Bunge lako Tukufu litaidhinisha bajeti hiyo na hivyo hatuna namna nyingine zaidi ya kuanza kujenga barabara hiyo kuanzia mwaka ujao wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili naomba nimhakikishie kwamba dhamira ya Awamu ya Tano ya Serikali ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni ya dhati na ndiyo maana tumeanza na kipande hiki cha kilometa 50. Mtakumbuka barabara nyingi tumekuwa tukianza na vipande vidogo vidogo sana, lakini katika Awamu hii ya Tano tutachagua miradi michache ili tupeleke rasilimali iweze kukamilika kwa haraka na baadaye tunaendelea kwenye miradi mingine, huo ndiyo mkakati wa jumla.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAWA A. GHASIA) aliuliza:- Je, ni lini barabara ya uchumi kutoka Mtwara – Nanyamba – Tandahimba - Newala – Masasi, itaanza kujengwa baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Katika Jiji la Mbeya tumekuwa na tatizo sugu sana la foleni katika barabara inayotoka Uyole hadi pale kwangu Mwanjelwa, ikifika saa 10 magari hayaendi kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bunge lililopita, Bunge la Kumi hiki kilikuwa ni kilio changu cha muda mrefu kwamba kwa nini tusifanye bypass kutoka barabara ya Uyole hadi uwanja wa ndege wa Songwe, lakini mpaka leo hii hili jambo halijafanikiwa kwenye vikao vyetu vya Road Board nimekwenda mpaka kumwona Meneja wa TANROAD bila mafanikio. Namuomba Mheshimiwa Waziri husika hapa atoe tamko ni lini barabara hii ya bypass kutoka Uyole hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe itakamilika?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taratibu za ujenzi wa barabara zote huwa tunaanzia kwenye vikao vya Road Board vya Mkoa ambavyo Waheshimiwa Wabunge ni wajumbe. Alichokizungumzia ni kwamba inaonekana Road Board ya Mkoa wa Mbeya bado haijaridhia ujenzi wa Bypass hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nitawasiliana na Road Board Taifa pamoja na Road Board Mkoa wa Mbeya kujua sababu halisi, kwa nini bypass hii bado haijakubalika kitaalam. Siwezi kutoa commitment inayoombwa kabla sijajua sababu za kitaalamu za kutokubalika hiyo bypass.