Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Kumekuwa na ongezeko la matumizi ya dawa za kupunguza maumivu zenye Codeine, Valium, Morphine, Amphetamine, Phenorbabitone ambazo zinauzwa bila cheti cha daktari na zinatumiwa kama mbadala wa dawa za kulevya:- (a) Je, Sheria zinasemaje kuhusu hilo linalosababisha vijana kuwa mateja wa dawa za kawaida? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha hakuna prescription drugs inauzwa bila cheti cha daktari?

Supplementary Question 1

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yaliyotuelimisha, lakini kama alivyokiri mwenye pamoja sheria zilizopo bado dawa za makundi yote matatu zinauzwa holela. Swali la kwanza, je, Serikali inatathimini yoyote inayoonesha madhara gani yanatokea kwa matumizi haya ya hovyo ya dawa za maumivu na antibiotic na dawa zote alizozitaja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jem haoni sasa kuna haja ya kuhamisha hizi dawa ambazo ni restricted kwa maduka ya MSD yaliyoenezwa nchi nzima ili pharmacy zingine ambazo zitatoa dawa hizi ziwe rahisi kufuatilia? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Janeth Mbene kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nianze kwa maelezo ya awali, tunakiri kwamba pamoja na kwamba dawa hizi zipo katika makundi haya bado kuna changamoto ya matumizi ya dawa pasipo na cheti cha daktari. Wimbi la tatizo hii limeanza kuwa kubwa na nitumie fursa hii kutoa elimu kwenye jamii, baada ya Serikali kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya, tumeanza kuona matumizi ya madawa ambayo kwa lugha ya kigeni tunaita prescription drugs zimeanza kutumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge na wananchi wote ambao wanaendelea kutusikiliza, matumizi ya dawa hizi za hospitali na matumizi ya vileo na tumeanza kuona kwamba kuna tatizo kubwa sana ya prescription drugs pamoja na vileo ambavyo vinapelekea athari kubwa sana kwa wananchi. Matumizi ya pombe yana athari katika ubongo wa mtumiaji na prescription drugs zina athari katika mapafu na katika maini ya watumiaji. Kwa hiyo, mtu ambaye anatumia dawa hizi kwa pamoja na pombe yuko katika hatari kubwa zaidi ya kuweza kupoteza maisha kwa sababu hivi vyote vinafanya kazi za aina moja yaani dawa hizi zinaongeza kasi ya zile athari za pombe na zile dawa zinapokuwepo mwilini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tumeliona hili na tumelibaini tatizo na tumeanza ndani ya Wizara kuweka utaratibu mzuri kuhakikisha kwamba hizi dawa ambazo zipo control tumeweka mfumo mzuri toka zinaingizwa nchini mpaka pale ambako zinakwenda kutumika na mtumiaji wa mwisho. Hili ni jambo ambalo tunaendelea kulifanyia kazi ndani ya Wizara.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Kumekuwa na ongezeko la matumizi ya dawa za kupunguza maumivu zenye Codeine, Valium, Morphine, Amphetamine, Phenorbabitone ambazo zinauzwa bila cheti cha daktari na zinatumiwa kama mbadala wa dawa za kulevya:- (a) Je, Sheria zinasemaje kuhusu hilo linalosababisha vijana kuwa mateja wa dawa za kawaida? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha hakuna prescription drugs inauzwa bila cheti cha daktari?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Watumiaji wa madawa ya kulevya hivi sasa Serikali kutokana na jitihada kubwa na nzuri za mapambano dhidi ya madawa sasa hivi wamegeuza kibao wameanza kutumia dawa kama pethidine, benzodiazepine dawa hizi zimekuwa zikisabisha kwamba watu ambao wanatumia madawa kulevya madawa hakuna wanatumia dawa hizi. Je, Serikali iko tayari sasa kuleta sheria ambazo zitakuwa kali sana ili kuweza kudhibiti usambazaji na manunuzi ya dawa hizi ili zifanane na jitihada kubwa na nzuri zinazofanywa na Mamlaka ya Udhibiti wa Madawa ya Kulevya Tanzania?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali zuri la Mheshimiwa Lucy Mayenga, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya awali tumeanza kuona ongezeko
la madawa ya hospitali ama prescription drugs zikianza kutumika ndivyo sivyo kama mbadala wa madawa haya ya kulevya. Sisi kama Wizara tumeanza kuchukua hatua na ni mambo ambayo tunaendelea kuyafanya kama ndani ya Serikali. Kuanza kutoa elimu kama ambayo nimeitoa hapa kwamba hizi dawa zinatakiwa zitumike kwa malengo ambayo yamekusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili tumeanza sasa kuweka utaratibu mzuri wa kufanya udhibiti wa hizi dawa kuhakikisha pale tangu zinapoingia mpaka kwa mtumiaji wa mwisho. Niseme kwamba uratibu huu tumeshauanza ndani ya Wizara na tutaendelea nao. Sheria tulizonazo za matumizi ya madawa ya kulevya zinaongelea vilevile hizi dawa za prescription drugs na sheria ni nzuri tu zinajitosheleza kwa adhabu.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Kumekuwa na ongezeko la matumizi ya dawa za kupunguza maumivu zenye Codeine, Valium, Morphine, Amphetamine, Phenorbabitone ambazo zinauzwa bila cheti cha daktari na zinatumiwa kama mbadala wa dawa za kulevya:- (a) Je, Sheria zinasemaje kuhusu hilo linalosababisha vijana kuwa mateja wa dawa za kawaida? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha hakuna prescription drugs inauzwa bila cheti cha daktari?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa sana la vijana wetu kutumia madawa ya kulevya na kwa kuwa sober nyingi sana zinamilikiwa na watu binafsi na kwa kweli zimekuwa zikifanya vizuri, lakini gharama za kuziendesha tunaona ni kubwa kiasi kwamba vijana wengi wanashindwa kumudu gharama zake. Je, ni kwa nini sasa Serikali isitoe ruzuku kwa hizi sober house za watu binafsi au kuanzisha za kwake ili kusaidia vijana wetu kurudi katika hali zao?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakiri kwamba kumekuwa na tatizo la dawa ya kulevya na Serikali imechukua juhudi
na hatua ya kuhakikisha kwamba tunadhibiti uingizaji wa dawa za kulevya na kwa kiasi kikubwa kwamba tumepunguza sana matumizi ya madawa za kulevya hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tunatambua vilevile kwamba kuna wahanga ambao walikuwa wanatumia hizi dawa za kulevya, sisi Serikali tumeendelea tukishirikiana na wadau binafsi. Kwa upande wa Serikali tumeanzisha vituo mbalimbali vya matibabu katika hospitali zetu za Mkoa wa Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na hivi karibuni tumezindua hapa Itega Dodoma, lakini tunatambua mchango mkubwa wa sober houses na sisi kama Serikali tumetoa mwongozo wa usimamizi wa hizi sober houses, lakini sasa hivi bado ni mapema sana kusema kwamba Serikali itakuwa inachangia Ruzuku kwa uendeshaji wa hizi sober houses.