Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Mwaka 2015, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli aliwaahidi wananchi wa Makamboko kulipa fidia kwa ajili ya eneo hili linalojengwa Kituo cha One Stop Centre yalikuwa maeneo mawili, tunaishukuru Serikali imelipa fidia kwa ajili ya kujenga soko la kimataifa na sasa bado hili la Idofi ambalo linajengwa kituo hiki. Nashukuru Mheshimiwa Naibu Waziri alipotoka Njombe alifika eneo la Makambako na tukampeleka pale Idofi ambapo alikutana na wananchi na Mheshimiwa Diwani mhusika na wananchi wana imani kubwa na Serikali juu ya kulipa fidia zao. Je, ni lini sasa Serikali itawalipa fidia wananchi wa Idofi ili waweze kuendelea na shughuli mahali pengine watakapohamia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mwaka huu wa fedha wa 2019/2020, hivi sasa tutaanza kuandaa bajeti, naiomba Serikali, ni kwa nini kwenye bajeti hii ya 2019/2020 usiingizwe mpango huu ambao umeingizwa hapa? Nakushukuru.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Deo Sanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mheshimiwa Rais aliahidi, lakini aliahidi kujenga mradi wa Kituo cha Ukaguzi wa Pamoja sasa katika ujenzi wa kituo hicho kuna process kama ambavyo jibu la msingi limesema; kuna usanifu wa awali usanifu wa kina na hatuwezi kujenga mradi bila kulipa fidia. Kwa hiyo, Mheshimiwa Deo pamoja na wananchi wa Jimbo lake Makambako ni kwamba mradi ni ujenzi wa kituo cha pamoja lakini katika mradi ndio kuna hizo hatua zingine, kwa hiyo nimhakikishie kwamba…

MWENYEKITI: Waheshimiwa tunaomba utulivu ndani ya Bunge.

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Kwa hiyo nimwahidi Mbunge na wananchi wa Makambako kwamba mradi utatekelezwa hatua zote pamoja na ulipaji wa fidia utafanyika.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza, niwashukuru sana Wizara ya Ujenzi kwa kunipa fedha za kutengeneza barabara ya Mugeta Siloli Simba. Na kwa kuwa ile barabara ilikuwa na km 21 na zimetengenezwa kilomita fulani na zimebaki kilomita tisa. Naomba kujua kutoka kwa Waziri ni lini sasa watapeleka fedha ili kumalizia kilomita tisa zilizobaki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumefanya ujenzi wa kuboresha sehemu ya barabara ya Mugeta kwenda Siloli Simba, lakini Mheshimiwa Mbunge atakubaliana name kwamba sehemu ya kilomita 11 iliyojengwa, barabara haikuwepo kabisa, lakini kile kiwango cha barabara kimewavutia Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa eneo hili ili sehemu ambayo ilikuwa na barabara awali na yenyewe ifanyiwe maboresho. Kadri tunavyopata fedha kilomita hizi chache zilizobaki tunafanya maboresho.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Madai ya wananchi ya kudai fidia kutokana na miradi ya ujenzi nchini yapo kila siku, ni mengi na ni makubwa. Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha wanawalipa wananchi hawa kwa uhakika na kwa wakati?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Paresso kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu tumeendelea kufanya malipo ya fidia miradi inapotekeleza nchi kote katika maeneo mbalimbali. Pia niseme tu shughuli za miundombinu zinaendelea, kwa hiyo tutaendelea kuwalipa wananchi fidia na kadri miradi itakavyoendelea tutaendelea kufanya malipo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge tusiwe na wasiwasi tumejipanga vizuri, kwa mwaka wa fedha mmetupitishia fedha zakufanya usanifu kilomita 3,856. Sasa tuone kwamba hitaji la kufanya maboresho ya miundombinu litaendelea na kulipa fidia kwa wananchi tutaendelea kulipa kulingana na sheria na taratibu.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 4

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa Majibu mazuri. Pamoja na majibu yake, lakini naomba niulize swali la nyongeza. Katika kutekeleza mradi wa barabara kwa kiwango cha lami barabara ya Namtumbo - Tunduru – Tunduru – Mjini Nakapanya wananchi wale wamekuwa wakusubiri kulipwa fidia zao kwa muda mrefu. Je, Serikali ina mkakati gani katika kuhakikisha wanalipwa na kuwaondolea adha hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chikambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu, mradi huu ulikopita wananchi walipwa fidia isipokuwa natambua tumezungumza na Mheshimiwa Chikambo, wapo wananchi wachache sana ambao walikuwa wana malalamiko yao, suala hili tunaendelea kulifuatialia, tukitatua tutawalipa hawa wachache kulingana na stahili zao.

Name

Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 5

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi shapu wa Jimbo la Kishapu, naomba nitoe pongezi kwa Wizara kwa kazi nzuri manayoifanya, lakini nina swali la nyongeza kwakuwa bararaba ya Kolandoto kwenda Kishapu ni muhimu kwa kuwekwa lami kwa sababu za kiuchumi na mambo mengine. Je ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo ya lami kutoka angalau Kolandoto kwenda Kishapu?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nchambi, Mbunge shapu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba eneo hili kutoka Kolandoto kwenda Mwangongo na bararaba hii inaenda kuunganisha kupita Sibiti na maeneo ya mikoa mingine. Kwa hiyo, tutakapopata fedha tutaanza kujenga barabara hii muhimu.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 6

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, ni lini sasa watamalizia barabara ya Kimanga ambayo inajengwa sasa kwa muda wa miaka miwili, mpaka sasa imeleta usumbufu mkubwa katika Kata ya Kimanga na mpaka sasa haijamalizika imesimama na mkandarasi hayupo, ni lini Serikali itamalizia hiyo barabara?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kaluwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba, baada ya Bunge hili nitatembelea mradi huu niangalie pamoja na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuona changamoto zilizopo ili tujue hatua za kuchukua kwa haraka ili barabara iweze kuboreshwa.

MWENYEKITI: Kwa hiyo unakwenda jimboni kwake?

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la mradi.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuza:- Serikali ilichukua eneo la Idofu kwa ajili ya kujenga One Stop Center lakini hadi leo wananchi hawajalipwa fidia:- (a) Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga One Stop Center kama ilivyokudia?

Supplementary Question 7

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya barabara ambayo nimeizungumza sana na Mheshimiwa Waziri pamoja na TAMISEMI wanajua, ni Barabara ya Chuo cha Ardhi – Makongo - Goba. Imekwama kutengenezwa kwa sababu ya fidia, sasa nataka Waziri aniambie, ni lini kipande hicho kitalipwa fidia ili wananchi wa Makongo waweze kujengewa barabara ya lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali na nyongeza la Mheshimiwa Halima Mdee kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa sana imefanyika kuboresha miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam na Mheshimiwa Mbunge anafahamu. Changamoto ambazo zimebaki ni kulipa fidia kwa hizi kilometa nne zilizobaki. Barabara hii ni muhimu kwa sababu tunavyojenga barabara ya juu pale Ubungo, barabara hii itatumika pia kupunguza msongamano ili kufanya ujenzi uende kwa haraka. Tunatambua umuhimu huo, kwa hiyo nimwombe tu Mheshimiwa Mdee avute subira, suala hili tunalifuatilia kwa umakini kuhakikisha kwamba kipande hiki kinatengenezwa.