Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR aliuliza:- Vitendo vya ukatili kwa watoto vimezidi kuendelea kwa kasi siku hadi siku kama vile ubakaji, kunajisiwa kwa watoto wa kiume na kuingiliwa kinyume na maumbile watoto wa kike:- Je, ni lini Serikali italeta Muswada wa Sheria Bungeni ili kurekebisha sheria hiyo iwe kali zaidi?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza; Serikali wamesema wameweka mikakati, nataka kujua ni mikakati ipi ambayo wameweka ili kupunguza ama kumaliza tatizo hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba; kwa kuwa tatizo hili ni kubwa sana na kesi mbalimbali zinapelekwa mahakamani na baadhi ya kesi watuhumiwa wanashinda kutokana na kwamba kuna vitu ambavyo vinakosekana kama vile shahawa ama majimaji ambayo yanalingana na yule mwanaume ambaye amembaka au kumnajisi mtoto, je, Wizara ya Afya imeshusha mwongozo gani kuwashushia Madaktari ili kuwaongoza waweze kupima vitu kama hivyo ili wananchi wasikate tamaa kupeleka kesi zao mahakamani na kushindwa?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zainab Mussa Bakar kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kubaini ukubwa wa tatizo na nianze kwa kutoa takwimu tu kwamba kati ya Januari mpaka Desemba, 2017 tulikuwa na matukio 41 ya ukatili wa kijinsia na kati ya hayo, 13,000 yalikuwa ni masuala ya ukatili dhidi ya watoto. Sisi kama Serikali tumeandaa mpango mkakati wa kuzuia ukatili wa jinsia dhidi ya wanawake na watoto ambao unaitwa MTAKUWA wa mwaka 2017/2018 ambao unaisha mwaka 2021/2022. Katika mkakati huu tumejielekeza katika maeneo makubwa yafuatayo:-

Moja, kuanzisha Kamati za Ulinzi na Usalama wa Wanawake na watoto ambapo mpaka sasa hivi kuna kamati zaidi ya 10,000 tumezianzisha katika ngazi mbalimbali kuanzia Taifa, Mikoa, Wilaya na katika ngazi ya Halmashauri hadi katika Kata; kuanzisha madawati ya jinsia ndani ya Jeshi la Polisi zaidi ya madawati 400 tumeshaanzisha. Sambamba na hilo, kumekuwa na kuanzishwa na mahakama maalum za watoto ili mashauri ya watoto yaweze kukaa na kusikilizwa. Tunaendelea kushauriana na Wizara ya Elimu kuhakikisha kwamba kunakwa na Walimu walezi ambao wanaweza wakatoa ushauri nasaha na kupokea baadhi ya mashauri kwa watoto ule ukatili ambao wanafanyiwa wakiwa majumbani.

Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu kama nilivyoeleza katika jibu la msingi ni kwamba mashauri mengi tunashindwa kuyafikisha mwisho kwa sababu wanaofanya ukatili huu ni watu ambao wako ndani ya familia. Kwa hiyo, nami nitoe rai kwa jamii kwamba tusiyamalize mashauri haya kifamilia na badala yake turuhusu mkondo wa kisheria uweze kuchukua nafasi yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ameelezea kwamba kushindwa kwa baadhi ya kesi kwa sababu ya ushahidi wa kitaalam kutoka kwa wataalam wetu wa afya. Hili tumeshalitolea maelekezo kwa wataalam wetu wote wa afya na tumeweka msisitizo mkubwa sana kwamba mtu yeyote katika Sekta ya Afya ambaye amepewa jukumu la kuthibitisha vipimo ambaye atakwenda kinyume na misingi na miiko ya maadili ya taaluma hatutasita kumfungia na kumfutia leseni ya Udaktari.

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR aliuliza:- Vitendo vya ukatili kwa watoto vimezidi kuendelea kwa kasi siku hadi siku kama vile ubakaji, kunajisiwa kwa watoto wa kiume na kuingiliwa kinyume na maumbile watoto wa kike:- Je, ni lini Serikali italeta Muswada wa Sheria Bungeni ili kurekebisha sheria hiyo iwe kali zaidi?

Supplementary Question 2

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Tatizo la ubakaji na ulawiti kwa watoto bado ni changamoto kubwa sana, hasa kwa Mkoa wetu wa Iringa. Sasa wenzetu wa Chuo cha Mkwawa na RUCO walifanya utafiti na walibaini kuwa wazazi na walezi wamekuwa wanaachwa na mzigo mkubwa sana kugharamia matibabu ya watoto hao.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa kuweka utaratibu maalum kwa matibabu, ukizingatia hawa watoto huwa wanaachwa na physical damage na psychological damage kubwa ili waweze kuwalea watoto hawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Rose Tweve kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto tulishalitolea tamko suala hili kwamba wahanga wote wa ukatili wa kijinsia Serikali itatoa matibabu bure.