Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Moja kati ya majukumu ya kuimarisha Muungano ni pamoja na kuhakikisha kuwa kero zote za Muungano zinatatuliwa; na vikao vingi vimekaa na kujadili kero hizo:- Je, ni kero ngapi tayari zimetatuliwa na zipi ambazo hadi sasa zimeshindikana kupatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ambayo yalikuwa ni madogo ila hakutoa ufafanuzi, lakini nitakuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa sababu jambo lolote linalokuwa linataka lifanikiwe linakuwa na ratiba au linakuwa na mpangilio maalum. Hata hivi vikao wanavyovifanya kwa vyovyote inabidi viwe na maandalizi na maandalizi yake kuwe na ratiba.

Sasa nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri kabla ya kufanya hivi vikao vyao vya pamoja vya mashirikiano, wanajiandaa kwa ratiba ya pande zote mbili baina ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa sababu baadhi ya Mawaziri huwa hawashiriki vikao kwa kuwa wanapotaarifiwa hivyo vikao wanakuwa nje ya nchi au wanakuwa na dharura nyingine za vikao vingine ambavyo wameshajipangia. Sasa nataka anijulishe, wanapokuwa wanakaa kufanya vikao hivyo wanakuwa wameandaa ratiba mapema baina ya SMZ na SMT ili wahakikishe kwamba viongozi wote hao wanatakiwa kushiriki? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wamesema kwamba changamoto zilikuwa 15, changamoto 11 zimepatiwa ufumbuzi zimebakia nne, sasa hizo changamoto nne ambazo anasema bado ziko katika maandalizi ya kupata ufumbuzi, ni zipi za SMT na zipi za SMZ katika hizo nne ambazo bado zimo katika changamoto zinazopatiwa ufumbuzi?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumjibu Mheshimiwa Fakharia Shomar maswali yake mawili ya nyongeza. Moja kila kikao kinaandaliwa ratiba mapema sana na nimkumbushe tu kwamba tarehe 9 Februari, 2019 kulikuwa na kikao cha Kamati ya Pamoja cha SMT na SMZ kujadili changamoto zote hizi na hasa hizi nne nazo pia zimetolewa maelekezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ni kweli hizi changamoto nne kwa mujibu wa swali lake la msingi alivyokuwa ameliuliza, ningependa pia nizitaje, moja ni mgawanyo wa kodi ya misaada; lakini ya pili, ni usajili wa vyombo vya moto; ya tatu, ni hisa za SMZ katika Bodi ya Sarafu ya Afrika ya Mashariki na Benki Kuu; na ya nne ni Tume ya Pamoja ya Fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongezee katika majibu mazuri sana yaliyotolewa na Naibu Waziri katika suala hili hasa la ratiba na utaratibu. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mwezi uliopita zimepitisha rasmi utaratibu mpya wa kushughulikia changamoto za Muungano na kuweka ratiba mahsusi ya vikao. Kwa hiyo, kile kikao kikubwa kabisa cha Makamu wa Rais ambacho ni cha Serikali zote Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza la Mawaziri la SMZ kinakutana mara moja kwa mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna kikao cha Mawaziri na chenyewe kinakutana mara moja kwa mwaka, kikao cha Makatibu Wakuu wote kinakutana mara mbili kwa mwaka na kikao cha Wataalam wa Serikali zote na chenyewe kinakutana mara mbili kwa mwaka. Kwa hiyo ratiba zimetolewa na Waraka wa Serikali (circular) imesambazwa na kueleza Wajumbe wote wa vikao hivi na utaratibu wa kuviitisha, utaratibu wa kuleta ajenda katika vikao ili kuwepo na utaratibu unaotabirika na unaoeleweka na ambao umepitishwa katika mfumo wa Serikali kushughulikia suala hili.

Vilevile, zimeundwa Kamati za hii Kamati ya Pamoja, Kamati ya Fedha, Uchumi na Biashara na Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ili zile changamoto ambazo ni za kutafutiwa majawabu haraka haraka zisingoje kikao kikubwa, Mawaziri waweze kukutana haraka katika hizi Kamati zao na kuzishughulikia. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeweka utaratibu madhubuti kabisa wa kushughulikia changamoto za Muungano katika Serikali hii ya Awamu ya Tano.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Moja kati ya majukumu ya kuimarisha Muungano ni pamoja na kuhakikisha kuwa kero zote za Muungano zinatatuliwa; na vikao vingi vimekaa na kujadili kero hizo:- Je, ni kero ngapi tayari zimetatuliwa na zipi ambazo hadi sasa zimeshindikana kupatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 2

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwanza kabisa nipende kuzipongeza Serikali zote mbili kwa jitihada ambazo zimekuwa zikichukua katika masuala haya. Kwa kuwa jitihada hizi, wananchi wengi hawana taarifa nazo na hawana uelewa nazo, Serikali sasa haioni umuhimu wa kuanza kuweka utaratibu maalum wa kutoa taarifa hizi ili wananchi waweze kupata uelewa wa pamoja? Ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru. Nichukue fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Khadija Nassir lakini pia nipokee ushauri wake, tufike mahali sasa tuanze kuziweka wazi taarifa hizi japo tumekwishaanza lakini kuweka kwa mapana zaidi. Kwa hiyo, napokea ushauri.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Moja kati ya majukumu ya kuimarisha Muungano ni pamoja na kuhakikisha kuwa kero zote za Muungano zinatatuliwa; na vikao vingi vimekaa na kujadili kero hizo:- Je, ni kero ngapi tayari zimetatuliwa na zipi ambazo hadi sasa zimeshindikana kupatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 3

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Wabunge hawa wanapouliza kuhusu kero za Muungano na vipi zinatatuliwa, ni kwamba tunaporudi kwa wapiga kura wetu tunazikuta. Kwa hiyo, inaonesha kwamba kero za Muungano zinatatuliwa kwenye meza, lakini kwenye vitendo hakuna. Kwa mfano, msafirishaji wa ng’ombe kutoka Zanzibar akija akichukua ng’ombe Bara kupeleka Zanzibar analipishwa ushuru sawasawa na anayesafirisha kupeleka Kenya kwa Sh.37,500 badala ya Sh.7,500. Sasa ni ipi faidi ya Wazanzibari kuwa ndani ya Muungano? Nakushukuru.

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli haikutazamiwa kwamba Mheshimiwa Mbunge atauliza ni zipi faida za kuwepo Muungano, kwa sababu hata yeye kuwepo kwake hili ni Bunge la Jamhuri ya Muungano. Muungano huu kwa pale tulipofikia hata haihitajiki kueleza faida zake kwa sababu zinaonekana dhahiri. Ukweli upo kwamba, zipo changamoto katika shughuli za kila siku za maingiliano na mahusiano hiyo haikataliwi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ziko changamoto kubwa za kisera ambazo ndiyo zinashughulikiwa katika vikao vya viongozi, lakini kuna yale mambo ya kila siku kwamba Afisa Forodha pale ameamua mwenyewe kwa anavyoona afanye jambo. Tunachosema sisi kwa wananchi wa pande zote mbili ni kwamba yanapojitokeza mambo kama haya, kama hili alilosema Mheshimiwa Mbunge, yaletwe kwetu haraka kwa sababu ni masuala ya kiutendaji ambayo yanashughulikiwa haraka. Yako mambo mengi ya namna hii ambayo yametatuliwa kwa taarifa tu kwamba, kuna jambo hili sisi tunadhani haliendi vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo sisi tunasema kwamba, changamoto hizi ndogondogo zisitumike kuupa jina baya Muungano, kwa sababu wakati mwingine ndipo makosa yanapofanyika, kwamba inatokea tatizo ambalo lipo tu, ni la kiutendaji, la kibinadamu, lakini linatumika kwamba Muungano wetu haufai kwa sababu kuna kitu hiki. Muungano huu ni mpana zaidi na ni mkubwa zaidi na una maana kubwa zaidi kuliko changamoto zinazojitokeza kila siku.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Moja kati ya majukumu ya kuimarisha Muungano ni pamoja na kuhakikisha kuwa kero zote za Muungano zinatatuliwa; na vikao vingi vimekaa na kujadili kero hizo:- Je, ni kero ngapi tayari zimetatuliwa na zipi ambazo hadi sasa zimeshindikana kupatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 4

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa vijana wengi hasa wa kizazi hiki kipya hawaelewi vizuri umuhimu wa kuuenzi Muungano, Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu ya kutosha hasa kwa vijana wa sasa na hata wale wa zamani ili kujua umuhimu wa kuuenzi Muungano?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimdhihirishie tu kwamba Serikali inaendelea na mchakato na imeendelea kutoa elimu juu ya faida za Muungano na labda kama bado ziko changamoto ambazo elimu hii haiwafikii vijana walio wengi, nadhani ni wakati muafaka sasa wa kuendelea kuhimiza kuhakikisha kwamba elimu hii inawafikia vijana wote.