Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Miundombinu ya Shule ya Sekondari Rugambwa ilijengwa mwaka 1964 na Sekondari ya Bukoba imejengwa mwaka 1939, hivyo imechakaa sana:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia ukarabati shule hizo?

Supplementary Question 1

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Bukoba Sekondari ina umri wa miaka 80, Rugambwa Sekondari ina umri wa miaka 55 lakini pamoja na uzee shule zote zilipitiwa na tetemeko na Bukoba Sekondari ikaja vilevile ikaezuliwa na kimbunga. Kwa niaba ya Mkoa wa Kagera na wanafunzi wanaosoma katika shule hizo, naipongeza sana Serikali kwa kutoa Sh.1,481,000,000 kwa ajili ya kukarabati Bukoba Sekondari na kuahidi kukarabati Rugambwa mwaka huu kuanzia mwezi huu wa Aprili. Kwa kuwa Rugambwa wakati wa tetemeko nyumba za walimu na zenyewe zilianguka na nyingine zikaathirika sana, hadi leo Mkuu wa Shule hana mahali pa kuishi, je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea nyumba za kuishi walimu wa Shule ya Sekondari Rugambwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, shule zote mbili, Bukoba Sekondari na Rugambwa zinahitaji kumbi za mikutano. Bukoba Sekondari haina ukumbi kabisa, Rugambwa ukumbi wake ni mdogo sana unachukua watoto 300 wakati wako wanafunzi karibu 700/800. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea kumbi za mikutano ili wanafunzi wapate mahali pa kufanyia mitihani na kufanyia mikutano?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kwa dhati kabisa na kwa furaha kubwa nipokee shukrani na pongezi za Mheshimiwa Mbunge kwa kazi ambayo Serikali imefanya katika shule zake. Lazima niseme kwamba Mheshimiwa Mushashu ni moja kati ya Wabunge makini sana katika Sekta ya Elimu na tumeendelea kufarijika na uzoefu wake mkubwa kama Mwalimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maswali yake, kwanza kuhusiana na nyumba za Walimu katika Shule ya Rugambwa, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunavyozungumza tayari Serikali inafikiria kujenga nyumba nane za Walimu katika shule ya Rugambwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na kumbi za mikutano katika shule zote mbili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ikiwa ni pamoja na miundombinu katika shule zake kadiri uwezo wa fedha utakavyoruhusu.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Miundombinu ya Shule ya Sekondari Rugambwa ilijengwa mwaka 1964 na Sekondari ya Bukoba imejengwa mwaka 1939, hivyo imechakaa sana:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia ukarabati shule hizo?

Supplementary Question 2

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kupata nafasi hii. Tatizo lililopo Bukoba ni sawa na tatizo lililopo katika Mkoa wa Mara hasa Jimbo la Bunda Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunda Vijijini tuna Shule za Sekondari 12…

MWENYEKITI: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naweka hoja vizuri ili swali lieleweke. Ili mtoto awe na usikivu mzuri darasani, mazingira ya shule zile ni mabaya sana, maboma hayajamaliziwa, kwa hiyo, ili mtoto awe na usikivu darasani ni vizuri kuwe na miundombinu mizuri na mazingira mazuri. Je, ni lini Serikali itahakikisha inajenga na kuzimalizia zile Shule za Sekondari katika Jimbo la Bunda Vijijini? Ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule zetu na ndiyo maana Serikali imeendelea kutenga fedha kwa mabilioni kuhakikisha kwamba tunaondoa changamoto ya miundombinu katika shule zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu katika mwezi wa Januari ilitoa shilingi bilioni 56 kwa shule tofauti 500 nchi nzima. Lengo lake ni kuendelea kupunguza changamoto za miundombinu katika shule hizo. Hata Mkoa wa Mara na Bunda anapotoka Mheshimiwa Mbunge nao wamefaidika na mpango ule wa ujenzi kupitia mradi wa kulipa kulingana na matokeo (EP4R).

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Wizara ya TAMISEMI hivi karibuni imetoa fedha kwa ajili ya kumalizia maboma nchi nzima. Naomba Mheshimiwa Mbunge awasiliane na Halmashauri yake kupata taarifa sahihi kwa sababu fedha hizo zimeenda nchi nzima. Kama bado kuna upungufu ni nia ya Serikali kuendelea kukabiliana na changamoto hizo kadiri uwezo wa fedha utakavyoruhusu.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Miundombinu ya Shule ya Sekondari Rugambwa ilijengwa mwaka 1964 na Sekondari ya Bukoba imejengwa mwaka 1939, hivyo imechakaa sana:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia ukarabati shule hizo?

Supplementary Question 3

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa kunipa nafasi. Naipongeza Serikali kwa kutupatia fedha Korogwe Girls za ukarabati wa shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya sana katika ukarabati ule bweni moja la Thabita limeshindikana kabisa kukarabatiwa kutokana na ubovu wa bweni lile.

Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutupatia fedha ili tuweze kujenga jengo hilo kutokana na watoto 120 kwenda kutawanywa kwenye mabweni mengine?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mary Chatanda pale Wizarani kwangu ameshatengewa kiti kwa sababu kila wakati amekuwa akija Wizarani kufuatilia changamoto za miundombinu kwa ajili ya shule zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu siyo mara ya kwanza kuleta changamoto hii, Wizara yangu imejipanga kuondoa hiyo kero moja kwa moja ili watoto wetu waweze kusoma katika mazingira mazuri.