Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Maeneo mengi katika Jimbo la Tabora Mjini na Iramba Mashariki hayana mawasiliano ya simu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo wapate mawasiliano?

Supplementary Question 1

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa, hili swali limekuwa la muda mrefu na maeneo mengi ya Tabora Mjini zikiwemo Kata za Itetemya maeneo ya Kipalapala, lakini pia maeneo ya Ndevelwa, Ikomwa, Kakola, Uyui na mengine bado yana matatizo mengi sana ya mawasiliano ya simu. Namuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa hili Bunge lina muda mrefu na tutakuwa na siku za katikati za mapumziko ya wiki, ni lini atakuwa tayari kuongozana na mimi angalau tukakague pamoja miradi hii aweze kuona shida ya wananchi wa sehemu hizo kwenye mambo ya mawasiliano?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Adam Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mwakasaka kwa juhudi nyingi sana anazozifanya katika kushughulikia kero za wananchi katika Jimbo la Tabora Mjini. Mwenyewe nimekwishafika pale, Mheshimiwa Mwakasaka na unakumbuka tulikuwa wote tukazungukia baadhi ya maeneo niliyozungumza yamefungiwa minara na nakuhakikishia kwamba niko tayari wakati wowote twende kutembelea maeneo mengine na nitaambatana na timu ya watalaam kutoka Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, ahsante.

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Maeneo mengi katika Jimbo la Tabora Mjini na Iramba Mashariki hayana mawasiliano ya simu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo wapate mawasiliano?

Supplementary Question 2

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Katika Jimbo la Nkasi Kusini vipo vijiji kadhaa ambavyo havina mawasiliano ya simu na nimefanya juhudi sana kumtembelea Mheshimiwa Waziri, mara tatu hivi na kumuandikia barua, vipo Vijiji vya Kasapa, Msamba, Mlalambo, Ng’undwe na vinginevyo. Je, ni lini sasa vijiji hivi vitapata mawasiliano ya simu ambayo ni muhimu sana? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mipata, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba amekwishafika Ofisini kwangu mara tatu, kwa ajili ya kufuatilia changamoto ya mawasiliano katika Jimbo lake la Nkasi Kusini. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari orodha ya vijiji ulivyoniandikia kikiwemo Kasapa, Msamba na Mlalambo vimekwishaorodheshwa kwa ajili ya kutangaziwa tenda hivi karibuni kabla ya mwezi Mei ili viweze kuingizwa kwenye mpango wa kupewa minara ya mawasiliano.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Maeneo mengi katika Jimbo la Tabora Mjini na Iramba Mashariki hayana mawasiliano ya simu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo wapate mawasiliano?

Supplementary Question 3

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wilaya ya Urambo haikutokea katika orodha ya kwanza iliyotolewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa maeneo ambayo hayana usikivu mzuri wa simu, je, kwa kuwa yuko tayari kwenda kwa Mheshimiwa Mwakasaka Tabora Mjini, hawezi pia kupitiliza kuja Urambo ili ajionee mwenyewe maeneo yasiyokuwa na usikivu wa simu?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali la mama yangu, Mheshimiwa Margaret Sitta, Mbunge wa Urambo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mwezi Agosti, 2018 tulitangaza orodha ya kata 273 zinazopelekewa minara kwa ajili ya kusambaza mawasiliano na bahati mbaya Jimbo la Urambo halikupata. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika vijiji ambavyo aliniletea barua ofisini kwangu, vijiji vya Urambo vitaingizwa kwenye mpango wa mawasiliano kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Namhakikishia nitakapokwenda kwenye Jimbo la Mheshimiwa Mwakasaka basi nitapitia mpaka Urambo kuangalia changamoto za mawasiliano, kama kuna jipya tutaweza kuongeza zaidi.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Maeneo mengi katika Jimbo la Tabora Mjini na Iramba Mashariki hayana mawasiliano ya simu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo wapate mawasiliano?

Supplementary Question 4

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mwaka 2016, Serikali ilitutaka sisi Wabunge kuorodhesha vijiji, vitongoji pamoja na mitaa yote ambayo haina mawasiliano na sisi Wabunge tulifanya hivyo, tukaorodhesha vijiji vyetu vingi sana. Jimbo langu la Mbozi niliorodhesha vijiji vingi sana kikiwepo Kijiji cha Mbozi Mission ambacho kina hospitali kubwa na taasisi nyingi kama vyuo, hakina mawasiliano, Kijiji cha Maninga, vijiji vingi sana Jimbo la Mbozi havina mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nijue kwa nini Serikali ilituambia sisi Wabunge tupeleke orodha ya vijiji na maeneo ambayo hayana mawasiliano lakini mpaka sasa maeneo hayo hatujapata mawasiliano. Je, Serikali ilikuwa inadanganya Wabunge?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Haonga, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mwaka 2016 tuliwaomba Waheshimiwa Wabunge waorodheshe maeneo mbalimbali ya majimbo yao ambayo hayana mawasiliano. Kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote tulifanyia kazi maeneo mengi sana na ndiyo maana mpaka sasa hivi kwa mawasiliano takwimu zinasema Watanzania tunawasiliana kwa asilimia 94. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo yake ya Mbozi Mission na mengine aliyoyazungumza inawezekana kabisa kwenye orodha ambayo tunategemea kuitangaza mwisho wa mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi wa tano yakawemo na hivyo atapata mawasiliano. Hiyo ndiyo Serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Maeneo mengi katika Jimbo la Tabora Mjini na Iramba Mashariki hayana mawasiliano ya simu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo wapate mawasiliano?

Supplementary Question 5

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo lililoko Tabora Mjini kwa watoto wetu ni sawasawa na tatizo lililoko Pemba kwa wazazi wao, tatizo la mawasiliano. Mheshimiwa Waziri swali hili uliulizwa mwaka jana na Wabunge wawili na ukaahidi kuja Pemba na ukaja Pemba wewe mwenyewe ukaona tatizo lililopo, hususan kwa Mheshimiwa Maida na Mheshimiwa Bi. Mgeni lakini hadi leo tatizo liko vilevile halijatatuka hakuna mawasiliano katika maeneo hayo. Sasa nini impact ya safari yako kuja Pemba zaidi ya marashi ya karafuu?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Yussuf, rafiki yangu sana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilikwenda Pemba mwezi Januari kwa ajili ya kukagua hali ya mawasiliano ya Kisiwa cha Pemba na ni kweli nilikuta hali si nzuri sana. Nikuhakikishie tu Mheshimiwa Yussuf kwamba impact ya safari yangu pamoja na marashi ya Pemba vilevile ni kuhakikisha tunawaletea mawasiliano ili wananchi wa Pemba waweze kuwasiliana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto tuliyoikuta kule ni kwamba kuna hali ya kijiografia ya mabonde na milima, halafu ina minazi mingi sana. Kwa hiyo, badala ya kuweka mnara mmoja u-supply radius ya kilometa 15 kama kawaida ina supply radius isiyozidi kilometa 4, kwa hiyo, inahitaji minara mingi sana. Kama unavyojua mnara mmoja ni shilingi milioni 300 mpaka 600, kwa hiyo, ni lazima tuwe na uwekezaji wa kutosha. Nakuhakikishia kwamba tutaweka uwekezaji huo kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ili wananchi wa Pemba na hasa kwenye kihoteli kile cha chini ya bahari waweze kupata mawasiliano.