Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMAN J. ZEDI aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Itobo - Kagongwa yenye urefu wa Kilometa 149 utaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Kwani ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na pia imo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020.

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongezea Serikali kwa kazi ambayo imefanywa kwenye barabara hii. Kimsingi wakati naandika swali hili, kuliwa hakuna kazi yoyote ambayo imefanyika, lakini sasa hivi nakubaliana kabisa na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Mshauri Mhandishi NIMETA Consult ameshaanza kazi, nami mwenyewe ni shuhuda nimemwona akifanya kazi hii ya usanifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba kwa kuwa Serikali imesema kazi ya usanifu wa kina inaisha mwezi Juni, 2019 na hii barabara ni ahadi ya Rais na pia ni jambo ambalo lipo kwenye ilani:-

Je, Serikali inaweza ikatoa kauli hapa kwamba barabara hii kwa kuwa usanifu utakuwa umekamilika mwezi Juni, sasa kwenye bajeti ijayo itatengewa fedha ili Mkandarasi wa kuanza kujenga aanze kazi kabla ya Awamu hii ya Tano haijamaliza muda wake?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunapokea pongezi kwa moya wa dhati kabisa lakini napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Selemani Zedi kwa jinsi ambavyo anafuatilia sana kipande cha barabara hii iliyotajwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mpango wa Serikali na nia ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara zote nchini kwanza zimepitika na pili zinaunganishwa kwa kiwango cha lami. Nimhakikishie Mheshimiwa Zedi kwamba barabara yake kama tulivyoahidi kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na kama ahadi ya Mheshimiwa Rais, tutaijenga kwa kiwango cha lami kabla ya mwaka 2020 kwisha.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMAN J. ZEDI aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Itobo - Kagongwa yenye urefu wa Kilometa 149 utaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Kwani ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na pia imo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020.

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kama ilivyo ahadi kwa Jimbo la Bukene, Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni zake na hata Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga barabara ya Tarime Mugumu ambayo ni kilometa 89 kwa kiwango cha lami; na kwa kuwa hii barabara ikijengwa itakuza uchumi siyo tu wa Tarime au Mara, bali wa Taifa, maana yake watalii watakao toka Kenya wataweza kupita kwenye njia ile:-

Ni lini sasa hii ahadi ya Mheshimiwa Rais itatimilika kwa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Tarime Mugumu almaarufu kama Nyabwaga Road?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali iliahidi kujenga kipande cha kilometa 44 kutoka Tarime mpaka Mugumu kwa kiwango cha lami. Naamini hata Mheshimiwa Mbunge anajua kwamba upembuzi yakinifu ulishafanyika, usanifu wa awali ulishafanyika na usanifu wa kina ulishafanyika. Sasa hivi tunatafuta pesa kwa ajili ya kumpa Mkandarasi wa kujenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekitik, kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo, tutajenda hiyo barabara kwa sababu ya umuhimu wa utalii wa nchi yetu kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMAN J. ZEDI aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Itobo - Kagongwa yenye urefu wa Kilometa 149 utaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Kwani ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na pia imo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020.

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. John Magufuli kwa uzinduzi wa barabara ya kutoka Makambako mpaka Mufindi jana. Naomba niulize swali moja. Katika ujenzi wa barabara ya kutoka Dodoma - Mtera mpaka Iringa, pale katika kona za Nyang’holo huwa kunakuwa na maporomoko makubwa sana ambayo huwa yanajitokeza hasa wakati wa mvua:-

Je, Serikali inatusaidiaje? Maana kutakuja kutokea ajali kubwa sana, hata jana nimepita pale. Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tayari ameshafika ofisini zaidi ya mara tatu akifuatilia kipande cha barabara hii ya kutoka Mtera - Iringa hasa kwenye kona zile za Nyang’holo ambazo ni korofi kabisa. Tunakiri na bahati nzuri nimeshamwelekeza Meneja wa TANROAD Mkoa kufuatilia eneo hilo ili tuanze tararibu za kulirekebisha kwa ajili ya usalama wa Watanzania.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. SELEMAN J. ZEDI aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Itobo - Kagongwa yenye urefu wa Kilometa 149 utaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Kwani ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na pia imo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020.

Supplementary Question 4

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi hii niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mji wa Mwanza unaendelea kukua kila siku na miundombinu ya barabara hasa barabara ya Kinyata inayotoka Mwanza Mjini kwenda Usagara hali yake kimsongamano siyo nzuri; na leo nauliza karibia mara ya nne:-

Ni lini sasa Wizara itakuwa tayari kuhakikisha barabara inayotoka Mwanza Mjini kupitia Igogo - Mkuyuni na Butimba - Nyegezi mpaka Buhongwa, inapanuliwa kwa njia nne sasa na kuweza kuwa barabara inayofanana na maziringira halisi ya mji wenyewe?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Jiji la Mwanza linapanuka kwa kasi sana na ni mipango ya Serikali kuhakikisha kwamba Jiji hilo linaundiwa program maalum ya kupanua barabara zake kupunguza msongamano. Namshauri Mheshimiwa Mbunge, baada ya kikao hiki, baada ya kipindi cha Maswali na Majibu, tuambatane naye mpaka Wizarani akaone mipango ya Serikali kuhusu Jiji la Mwenza kurekebisha barabara zake.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. SELEMAN J. ZEDI aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Itobo - Kagongwa yenye urefu wa Kilometa 149 utaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Kwani ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na pia imo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020.

Supplementary Question 5

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Mhandisi Mshauri yupo site kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa barabara ya Nyakahura - Lulenge – Mulugarama; na kwa kuwa barabara hii ni ya muda mrefu.

Ni lini sasa ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami utaanza?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Gashaza, ni kwa muda mrefu sana amekuwa akifuatilia hii barabara ambayo naomba niitamke kwa ladha yake; inaitwa Nyakahuura – Kumubuga, inapatia Murusangamba - Lulenge mpaka Murugarama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri anakiri kwamba Mshauri Mwelekezi yupo pale kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na baada ya kumaliza zoezi hilo atafanya usanifu wa awali kisha usanifu wa kina kupata michoro kwa ajili kutambua gharama za ujenzi. Hatua zinakwenda vizuri mpaka sasa hivi. Namshauri Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo. Tukishapata nyaraka zote hizo husika, hiyo barabara itaanza kurekebishwa tena kwa kiwango cha lami.