Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Juma Kombo Hamad
Sex
Male
Party
CUF
Constituent
Wingwi
Primary Question
MHE. JUMA KOMBO HAMAD (K.n.y. MHE. MBAROUK SALIM ALI) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa Watanzania hususan kizazi kipya, kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ili kutoa uelewa wa pamoja na dhamira njema za Muungano huo?
Supplementary Question 1
MHE. JUMA KOMBO HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mara kadhaa maafisa mbalimbali ambao wanatumia magari ambayo yamekuwa na namba za Zanzibar wamekuwa wakikumbana na vikwazo vya TRA pamoja na Polisi kwamba, namba hizo ni namba za kigeni wakati anapotembea Tanzania Bara. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, yupo tayari sasa kutenga muda mahususi kuwapa taaluma Polisi pamoja na TRA kuona kwamba, Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kuambatana na sisi au na mimi kwenda kuangalia namna Maafisa wa TRA wanavyofanya kazi pale bandarini kwamba, unapokuja tu na kilo tano za sukari kutoka Zanzibar au Tv ya nchi 21 unatakiwa ulipe kodi? Je, hili yupo tayari kwenda kulishuhudia Bandari ya Zanzibar ili kutoa mwongozo na taaluma kwa ajili ya shughuli hizo za kibiashara?
Name
Mussa Ramadhani Sima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS – MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbarouk, kwa niaba yake Mheshimiwa Juma ameuliza vizuri sana:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza niko tayari kwa yote mawili, lakini kwa ufafanuzi zaidi hili la vyombo vya moto kwa sababu, bado lipo tayari kwenye majadiliano na vikao vinaendelea, nadhani baada ya hivyo vikao sasa nitakuwa tayari kwa ajili ya kutoa hiyo elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, niko tayari kuambatana na wewe na Wabunge wengine ambao wanatoka Zanzibar kwenda kushiriki kwa pamoja kuhakikisha kwamba, eneo hili tunalifanyia ufumbuzi. Ahsante sana.
Name
Maryam Salum Msabaha
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JUMA KOMBO HAMAD (K.n.y. MHE. MBAROUK SALIM ALI) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa Watanzania hususan kizazi kipya, kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ili kutoa uelewa wa pamoja na dhamira njema za Muungano huo?
Supplementary Question 2
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais watumishi wengi wanakaimu.
Je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha watumishi hawa sasa, wale wanaokaimu wanapandishwa madaraja?
Name
Mussa Ramadhani Sima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru. Nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Serikali ina dhamira ya dhati kabisa kuhakikisha maeneo yote ambayo watumishi wanakaimu waweze kufanya kazi yao kwa ukamilifu. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tayari ofisi yetu imeshafanya utaratibu wa kuomba kibali kwa ajili ya kuhakikisha watumishi wote wale au maeneo yote, position zote ambazo zinakaimiwa ziweze kupata watalaam ambao wako kamili. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru ili nami niweze kufafanua swali la Mheshimiwa Mbunge, Maryam Msabaha. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), naomba nifafanue kidogo juu ya suala zima la kuhusu watumishi kukaimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli watumishi wamekuwa wakikaimu kwa muda mrefu sana na nimekuwa nikilizungumza hili kwamba, hii ni kutokana na watumishi wengi wamekuwa wakikaimishwa na waajiri wao kienyeji na nafasi za kukaimu ni kukaimu tu sio kwamba, ni nafasi ya kuthibitishwa au ni kwamba, umeshapewa ile kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi nafasi za kukaimu ziko katika uwezo wa madaraka kwa maana ya superlative substantive post. Kwa maana hiyo, sisi kama Serikali, tumetoa waraka kwamba, kukaimu mwisho miezi sita. Kwa maana hiyo waajiri wote nchini wanapaswa kuomba kibali na kama unataka mtumishi aendelee kukaimu basi tuandikie tena barua. Kukaimu lazima iwe kulingana na level ya ile nafasi ambayo unastahili kukaimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved