Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Barabara ya Likuyufusi – Mkenda yenye urefu wa kilometa 123 inayounganisha nchi mbili za Tanzania na Msumbiji, bado haijaanza kujengwa kwa kiwango cha lami:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza pia Mbunge wa Jimbo la Peramiho, dada yangu, Mheshimiwa Jenista Mhagama, kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia ujenzi wa barabara hii na hata alipokuja Mheshimiwa Rais, alijaribu kusema pale ili barabara hii iweze kujengwa.

(a) Swali langu la kwanza; ni kwa nini Serikali inachukua muda mrefu sana kufanya upembuzi yakinifu lakini pia na usanifu wa kina? Barabara hii imechukua karibu miaka kumi kupitia maneno hayo ya upembuzi na usanifu. Ni lini Serikali itamaliza upembuzi huu na usanifu huu ili barabara hii ianze kujengwa?

(b) Swali la pili; licha ya Serikali kuonesha kwamba imetenga shilingi bilioni 5.86, lakini fedha hizi hazikuweza kwenda kwa mwaka 2018/2019: Je, Serikali haioni kwamba kutokupeleka fedha hizi inaendelea kuchelewesha maendeleo kupitia barabara hii kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma, hususan Jimbo la Peramiho?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, uniruhusu tu nimpongeze Mheshimiwa Jacqueline, lakini nimpongeze Mbunge wa Peramiho kwa kufuatilia kwa sababu amekuwa akifuatilia sana jambo hili. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge mwuliza swali kwamba inachukua muda mrefu kwa sababu kwanza mtandao wa barabara ni mkubwa, mahitaji ya ujenzi ni makubwa na tunaendelea kutafuta fedha na kutenga fedha. Hata mwaka unaokuja tutaliomba Bunge lako liweke fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Fedha. Tukipata fedha tu mara moja tutatangaza na kuanza kujenga barabara hii. Kwa hiyo, kwa majibu hayo, Mheshimiwa Jacqueline avute subira kidogo, tumejipanga vizuri, mahitaji ni makubwa, tunakuja Peramiho kuhakikisha kwamba tumewaunga wananchi wa…

MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Kemi.

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Barabara ya Likuyufusi – Mkenda yenye urefu wa kilometa 123 inayounganisha nchi mbili za Tanzania na Msumbiji, bado haijaanza kujengwa kwa kiwango cha lami:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Nyakato Steel – Igombe, kilometa 18 na Barabara ya Mwaloni – Kirumba, kilometa 1.2 zimekuwa zikisuasua na ujenzi wake kwa muda mrefu sana. Mheshimiwa Angeline Mabula, amekuwa akifuatilia barabara hizi kwa muda mrefu lakini bado hatujapata majibu sahihi ya Serikali. Ni lini sasa barabara hizi zitakamilika na wananchi wa Mkoa wa Mwanza, hususan Wilaya ya Ilemela waweze kupata barabara safi na salama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua changamoto za barabara za Ilemela, nami nimekwenda, nimeona. Nitoe tu maelekezo na wito kwa Mameneja wetu kule kwenye Mkoa wa Mwanza kwamba wasimamie kwa ukaribu nami nitakwenda kuhakikisha kwamba maeneo haya; na yapo maeneo siyo haya tu aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge, yapo maeneo mengi kwenye Jimbo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Angeline Mabula kwa sababu amekuwa akifuatilia sana, ilinichukua siku nzima, mtandao ni mkubwa sana kwenye Jimbo lake, mjini lakini…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, majibu mazuri na muhimu, fanya ziara naye.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, nitakwenda.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Barabara ya Likuyufusi – Mkenda yenye urefu wa kilometa 123 inayounganisha nchi mbili za Tanzania na Msumbiji, bado haijaanza kujengwa kwa kiwango cha lami:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naomba niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya kutoka Tabora kwenda Kigoma ambayo inatuunganisha na Tabora bado haijakamilika; na kipande cha kutoka Malagarasi mpaka Uvinza ambacho kilikuwa na Mkandarasi wa Abu Dhabi Fund tumesikia kuna matatizo ya kiufundi: Je, Mheshimiwa Waziri unasema nini juu ya jambo hilo? Vinginevyo barabara hii haitakamilika mpaka tufike mwaka 2020.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Nsanzugwanko anafahamu, tumezungumza mara nyingi sana juu ya barabara hizi. Niseme tu kwa ufupi, Chagu – Kazilambwa pamoja na barabara ya Malagarasi – Uvinza zitakamilisha mtandao wa barabara kutoka Tabora kwenda Kigoma tukikamilisha vipande hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutazungumza tu na Mheshimiwa Mbunge tuone kama kuna changamoto, basi tujue nini kinachoendelea. Kwa kifupi tunakwenda kujenga barabara hii.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Barabara ya Likuyufusi – Mkenda yenye urefu wa kilometa 123 inayounganisha nchi mbili za Tanzania na Msumbiji, bado haijaanza kujengwa kwa kiwango cha lami:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Barabara za lami hugharimu pesa nyingi za Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mara tu barabara hizo zinapojengwa, hubomolewa na kupitishwa miundombinu mingine, hatimaye hazirejeshwi katika ubora wake:-

Je, Serikali inatuambia nini juu ya jambo hili?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ujenzi wa barabara unachukua fedha nyingi, lakini niseme tu shughuli zozote zitakazohusisha kukata barabara lazima zifanyike kwa mujibu wa sheria. Kwa hiyo, kama kuna mtu anakata barabara na kuacha uharibifu ni makosa. Nami nielekeze viongozi wote, Mameneja wote wa Mikoa; mtu ambaye atafanya shughuli za kibinadamu na kuharibu barabara bila kurejesha kwa ubora wake na bila kupata kibali kwa mujibu wa sheria ni makosa, wachukue hatua kwa mujibu wa sheria.