Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS aliuliza:- Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imeongeza idadi ya Majimbo ya Uwakilishi kutoka 50 hadi 54, kabla ya ongezeko hilo Majimbo ya Uwakilishi na Ubunge yalikuwa sawa kwa ukubwa, mipaka na idadi ya wapiga kura. Ongezeko hili limefanya Majimbo mawili ya uwakilishi kufanywa Jimbo moja la Ubunge:- Je, ni lini Tume ya Taifa ya Uchaguzi itafanya uhakiki wa Majimbo ya Ubunge Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kumwuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko la Majimbo yaliyoongezwa na Baraza la Wawakilishi Zanzibar mwingiliano wake unaleta usumbufu na kupunguza kasi ya maendeleo. Nataka kujua: Je, Tume ya Taifa iko tayari kuongeza Majimbo manne ili yaende sambasamba ili tufanye kazi vizuri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ZEC ni Wakala wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi; NEC kwa Zanzibar kwa Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Wabunge, lakini wanatumia daftari moja, kura inapigwa siku moja katika chumba kimoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uchaguzi wa 2015 ZEC walifuta matokeo ya Uchaguzi wakati ambapo Wawakilishi na Madiwani walishatangazwa katika Majimbo yao na wamepewa hati zao za ushindi, katika mazingira kama hayo, nataka kujua: Je, NEC wametumia sheria gani ya kukubali uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Wabunge kutoka Zanzibar?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, nikianza na swali la kwanza kuhusu Majimbo manne ya Uwakilishi, kama katika majibu yangu ya msingi yalivyosema, suala hili la ugawaji wa Majimbo yanafanyika kwa mujibu Ibara ya 75(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na katika maneno yaliyotumika ni baada ya kufanyika uchunguzi na kugawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa mujibu wa Katiba hii, ni kwamba pindi pale matakwa ya Katiba hii na hasa katika Ibara ya 98(1)(b) ambayo inasomwa pamoja na Orodha ya Pili ya Nyongeza item Na. 8 ya kwenye Katiba ambayo inahitaji ongezeko la Wabunge wa Zanzibar, lazima pia ipitishwe na theluthi mbili ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na wenzetu kutoka Zanzibar. Kwa hiyo, kwa mujibu wa Katiba, jambo hilo linawezekana baada ya taratibu hizo kufuatwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusiana na matokeo ya uchaguzi; kwa mujibu wa Katiba yetu inazungumza vyema kabisa kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi ina jukumu la kusimamia Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge kwa upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, chaguzi nyingine zote zinakuwa chini ya ZEC ambao pia kwa mujibu wa Katiba nao wana majukumu ya kusimamia uchaguzi katika ngazi hiyo. Kwa hiyo, jambo ambalo limetokea ambalo Mheshimiwa Mbunge amelisema, maana yake ni kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitumia mandates yake ya Katiba ambayo inampa mamlaka ya kusimamia uchaguzi huo.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS aliuliza:- Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imeongeza idadi ya Majimbo ya Uwakilishi kutoka 50 hadi 54, kabla ya ongezeko hilo Majimbo ya Uwakilishi na Ubunge yalikuwa sawa kwa ukubwa, mipaka na idadi ya wapiga kura. Ongezeko hili limefanya Majimbo mawili ya uwakilishi kufanywa Jimbo moja la Ubunge:- Je, ni lini Tume ya Taifa ya Uchaguzi itafanya uhakiki wa Majimbo ya Ubunge Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kuna Wilaya ambazo zina Majimbo mawili na Wilaya hizi ziligawanywa Majimbo kwa sababu ya ukubwa wa zile Wilaya na idadi kubwa ya watu, lakini hivi sasa kuna tetesi ambazo zinatembea chini kwa chini huko Serikalini kwamba yale Majimbo ambayo yaligawanywa kutokana na ukubwa lakini pia na wingi wa watu yanataka kurudishwa kuwa Jimbo moja moja.

Je, kama hilo ni kweli, hatuoni kwamba Serikali ita-hinder utendaji wa Majimbo hayo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kama Mbunge mwenyewe alivyoli-phrase swali lake kwamba ni tetesi, naomba nami kwa upande wa Serikali tusijibu tetesi, ikiwa rasmi itasemwa kama ni rasmi.