Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini hatma ya kipande cha barabara ya Handeni- Mziha ambacho Serikali iliahidi kwamba Mkandarasi akishalipwa ujenzi utaanza, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inaunganisha mikoa miwili?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza kabisa napenda kuishukuru Serikali kwa kusikia kilio cha Wanahandeni cha muda mrefu kwa kuitengea hela hiii barabara. Barabara ya Mziha - Handeni matatizo yake ni sawasawa na barabara inayotoka Handeni kwenda Kilindi. Barabara hii inaunganisha mikoa karibu minne ambayo ni Tanga, Manyara, Dodoma mpaka Singida. Barabara hii asilimia kubwa wanayoitumia ni wakulima na huwa wanapata tabu sana…

MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swali sasa.

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni lini barabara hii inayotoka Handeni kwenda Kilindi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omar Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali inayo mpango wa kujenga barabara hiii kutoka Handeni kilometa 461 inapita katika maeneo ya Handeni, Kivirashi, Kijungu, Kibaya, Njoro, Mrijo chini inakwenda Chemba hadi Singida. Tunao mpango wa kujenga barabara hii na tayari imeshasanifiwa. Niseme tu kwamba katika mwaka huu wa fedha unaokuja tutapendekeza kwenye Bunge lako ili tuanze kujenga kwa kiwango cha lami barabara hii muhimu kwa sababu barabara hii itakwenda sambamba na bomba la mafuta ambalo litajengwa. Kwa hiyo ni barabra muhimu sana, kwa hiyo nimwombe tu Mbunge avute subira kwamba tutakuja kujenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwenye maeneo ambayo ni korofi ambayo yanapita eneo la Kilindi, kwa mfano, eneo la kutoka kwa Luguru kwenda Kibirashi ni eneo ambalo kidogo lina ukorofi, tumepanga katika mwaka unaokuja kwamba wakati tuna harakati za kujenga kiwango cha lami tutaiimarisha eneo hili kwa kujenga daraja katika eneo la Kigwangulo. Mheshimiwa Kigua naona anapiga makofi pale anafahamu eneo hili lina changamoto, kwa hiyo tutakuja kuimarisha wakati huo Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kujenga kiwango cha lami.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini hatma ya kipande cha barabara ya Handeni- Mziha ambacho Serikali iliahidi kwamba Mkandarasi akishalipwa ujenzi utaanza, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inaunganisha mikoa miwili?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri napenda tu kumkumbusha kwamba Mheshimiwa Rais aliahidi barabara ya kutoka Dutwa Jimboni kwa Mheshimiwa Mwenyekiti kuja Ngasamo kuja mpaka Nyashimo iwekwe kwa kiwango cha lami na maandalizi yameshaanza kidogo kidogo. Nataka tu nipate comfort ya Serikali, ni lini sasa utekelezaji halisi wa barabara hii utaanza kwa ajili ya kuweka lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chegeni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Chegeni nafahamu barabara hii tumeizungumza sana, ni barabara muhimu na hatua kama alivyosema mwenyewe kwamba ziko hatua kwenye ujenzi wa barabara hii tumeshazifikia. Kwa hiyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Chegeni kwamba tunaendelea kuhakikisha kwamba kila tukipata fedha barabara hii tunaijenga ili tuweze kuikamilisha barabara hii muhimu. Kwa hiyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Chegeni na wananchi wa maeneo yote ya Dutwa na Simiyu kwa ujumla kwamba tunawaunganisha vizuri katika maeneo yao.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini hatma ya kipande cha barabara ya Handeni- Mziha ambacho Serikali iliahidi kwamba Mkandarasi akishalipwa ujenzi utaanza, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inaunganisha mikoa miwili?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Singida- Ilongero –Ngamu ambayo pia inaunganisha Mkoa wa Manyara ni barabara muhimu sana kwa wananchi wa Mkoa wa Singida. Barabara hii ilitangazwa kipande cha kilometa 12.6 kutoka Njuki kwenda Ilongero kujengwa kwa kiwango cha lami tangu mwezi Novemba mwaka jana.

MWENYEKITI: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara hiyo kutoka Njuki kwenda Ilongero utaanza? Ahsante sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monko kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumejipanga kujenga barabara hii muhimu kutoka Singida- Ilongero- Ngamu tunakwenda mpaka Hydom na tumetenga fedha katika mwaka huu wa fedha unaoendelea, zoezi la usanifu ili
kujenga barabara hii yote inaendelea. Hata hivyo, kipande hiki cha barabara anachokizungumza kutoka eneo la Njuki kwenda Ilongero ni sehemu muhimu sana kwa kuwahudumia wanachi wa Singida Vijijini. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea na utaratibu wa harakati za manunuzi, zikikamilika tu tutaanza ujenzi wa barabara hii muhimu, kwa hiyo Mheshimiwa Monko avute subira tunakwenda Ilongero kujenga barabara hii.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini hatma ya kipande cha barabara ya Handeni- Mziha ambacho Serikali iliahidi kwamba Mkandarasi akishalipwa ujenzi utaanza, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inaunganisha mikoa miwili?

Supplementary Question 4

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kuniona. Matatizo yaliyopo Handeni-Mziha- Kibindu mpaka Mbwewe yanalingana kabisa na hii barabara ya kutoka Handeni kwenda Mziha. Je, ni lini Serikali inakuja kutujengea barabara ile kwa kiwango cha lami kama ambavyo sasa hivi nyumba zote zimepigwa X kupisha ujenzi huo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge anauliza juu ya barabara ya kutoka Mbweni inakwenda Kibindu ikipita kwa Luhombo itaungana na barabara hii niliyoijibia swali la msingi kwa maana ya kwamba kuwaunganisha wananchi wa maeneo haya na barabara hiyo itakuwa inakwenda Tanga na sehemu hii kweli ina uzalishaji mkubwa. Niombe tu Mheshimiwa Ridhiwani kwamba avute subira kwa sababu najua barabara karibu zote zipo kwenye mpango mkakati wetu wa Wizara na ikimpendeza tuonanane baadaye tuitazame hii barabara
kwamba kwenye mpango wetu wa kipindi cha miaka mitano tumekipangia nini kipande hiki cha barabara kwa maana ya kwamba inajengwa kwenye kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwa sasa tunaiboresha barabara hii na mimi nimeipita mara kadhaa kwamba iko katika kiwango kizuri kwamba inaendelea kuwapa huduma nzuri zinazohitajika wananchi wa maeneo haya.