Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- Pembejeo za kilimo ni ghali sana, hivyo wakulima wengi hushindwa kununua na kusababisha kupata mavuno haba. Je, Serikali ipo tayari kupunguza au kuweka bei elekezi iliyo nafuu kwa mkulima ili aweze kupata pembejeo za dawa, mbolea na zana za kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa mwaka 2018 kwa maana ya mwaka uliopita Serikali ilipora fedha za wakulima wa korosho zaidi ya bilioni 300 ambazo zilikuwa ni za export levy na kusababisha wakulima wa korosho kushindwa kununua sulphur. Mwaka huu tumeona uzalishaji wa korosho ulikuwa wa chini sana kwa sababu wakulima wanashindwa kununua sulphur.

Je, Serikali ipo tayari sasa msimu huu wa korosho unaokuja kuweza kugawa sulphur bure kwa wakulima wa korosho ili tija iweze kuongezeka katika uzalishaji wa korosho?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa bei ya kahawa imeendelea kuwa chini mwaka hadi mwaka na hali hii imetokana na suala la pembejeo kuwa juu sana wakati bei ya kahawa imeendelea kuwa chini kabisa. Je, Serikali iko tayari sasa kuanzisha mfuko wa kuimarisha bei kwenye zao la kahawa yaani Price Stabilization Fund ili pale kahawa inaposhuka bei Serikali iweze kufidia kupitia mfuko huo?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anataka kujua kuhusu suala la export levy, kwanza sio kweli, Serikali haijapora pesa za wakulima wa export levy, wakulima wa korosho kule Mtwara. Haya yalikuwa ni mapato ya Serikali kama mapato mengine na tulileta mapendekezo hapa na yalipitishwa na Waheshimiwa Wabunge. Kwa hiyo, Serikali ilichofanya ni utekelezaji wa sheria ile ambayo ilipitishwa na Wabunge akiwepo Mheshimiwa Haonga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu kahawa kwamba tuanzishe mfumo wa price stabilization kwa ajili ya kufidia pale bei zinapoanguka. Kwanza, ni wazo zuri ambalo na sisi Serikali tunalipokea. Lakini katika mazao sio la kahawa peke yake ambayo yanaanguka katika masoko ya dunia, ni suala la msingi, sio bei. Hatuna uwezo wowote wa ku-control bei katika soko la Kimataifa. Uwezo wetu sisi ambao tumegundua kama Serikali ni tija ndogo wanayoipata wakulima katika mazao kwamba wanatumia gharama kubwa lakini wanachokipata ni kidogo na ndiyo maana sasa hivi tunaimarisha mfumo wa upatikanaji pembejeo ili kuongeza tija kwa wakulima, watumie gharama ndogo wapate mavuno vizuri ili tuweze kushindana katika masoko ya ndani na ya nje ambayo hatuna uwezo wa kupanga bei.

Name

Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- Pembejeo za kilimo ni ghali sana, hivyo wakulima wengi hushindwa kununua na kusababisha kupata mavuno haba. Je, Serikali ipo tayari kupunguza au kuweka bei elekezi iliyo nafuu kwa mkulima ili aweze kupata pembejeo za dawa, mbolea na zana za kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza swali kuhusu kilimo cha korosho. Juzi wakulima wa korosho wamelipwa fedha chini ya kiwango ni theluthi moja ya haki yao. Je, Mheshimiwa Waziri unawaambia nini wakulima hawa, hizi fedha ndiyo basi au watalipwa zingine na sababu gani ambazo zimefanywa hawakuweza kulipwa hela zote?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunafahamu malipo yote wanayopaswa kulipwa wakulima wa korosho ni zaidi ya bilioni 723 na mpaka sasa tumelipa zaidi ya bilioni 633. Bado kuna wakulima ambao wanadai Serikali bilioni 100 hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka wiki iliyopita tulipeleka zaidi ya bilioni 50 na malipo yanaendelea mpaka sasa hivi na kama anachokizungumza, kama tunavyofahamu, wanunuzi wa korosho kabla Serikali hatujaweza kuokoa hali ilivyokuwa, walikuwa zaidi ya 100. Lakini mwaka huu mnunuzi ni mmoja tu na ukizingatia kwamba hii benki ya maendeleo ya kilimo na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ilikuwa haijajiandaa katika ununuzi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ilipaswa mjue kwamba Mbunge ungeipongeza Serikali na Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko kwa hatua ilizochukua mpaka leo tumeweza kulipa zaidi ya bilioni 633 na mnunuzi akiwepo mmoja kitu ambacho kilikuwa hakuna kwenye bajeti badala ya kusema kwenda kwenye…

MWENYEKITI: Ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- Pembejeo za kilimo ni ghali sana, hivyo wakulima wengi hushindwa kununua na kusababisha kupata mavuno haba. Je, Serikali ipo tayari kupunguza au kuweka bei elekezi iliyo nafuu kwa mkulima ili aweze kupata pembejeo za dawa, mbolea na zana za kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa katika jibu la msingi la Serikali kwenye suala la pembejeo tunakiri kwamba moja ya sababu ya kupanda na kuongezeka kwa gharama ni kwa sababu pembejeo zinaagizwa kutoka nje. Katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM, katika Mpango wa Serikali, kulikuwa na ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea Kilwa Mkoani Lindi. Serikali imefikia wapi kukamilisha ahadi hii ya Ilani ya Uchaguzi ili kusaidia upatikanaji wa pembejeo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Naomba nijibu kidogo swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi tuliweka ahadi ya kuhakikisha kwamba tunajenga kiwanda cha kuzalisha mbolea pale Kilwa. Naomba nimhakikishie tu kwamba hatua za ujenzi wa kiwanda hicho tuko katika hali nzuri sana. Mpaka sasa hivi wiki mbili zilizopita wataalam kutoka Pakistan, Ujerumani na Morocco wamekuja kwa ajili ya kuangalia na kufanya tathmini ya mwisho na kufanya mazungumzo na Serikali ili kuhakikisha kwamba kiwanda hiki cha mbolea kinajengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni matumaini yetu kwamba baada ya muda mfupi, kiwanda hiki kitaanza kujengwa sambamba na maeneo mengine ya viwanda ambavyo vitajengwa ili kuweza kupunguza gharama za pembejeo hapa nchini. Nashukuru.