Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya maandalizi ya awali ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuweka lami barabara muhimu ya Kibaoni-Kasansa-Muze- Kilyamatundu-Kamsamba kutokea Mlowo; ambayo inaunganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa, naipongeza Serikali kwa ujenzi wa daraja, imekuwa ni faraja kubwa kwa kweli kwa wananchi, tunaipongeza sana Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu hayo, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Kwa kuwa Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa barabara hiyo na imekubali kuanza kutenga fedha kwa ajili ya usanifu kwa maana ya kuweka lami lakini bado katika barabara hiyo yapo maeneo korofi ambayo yanasababisha magari kukwama wakati wa masika. Je, kwa nini Serikali isitenge fedha za kutosha kutatua tatizo hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kipande cha barabara ya Ntendo - Muze chenye kilometa 37.07 ni barabara inayotegemewa na wananchi wa Bonde la Ziwa Rukwa katika kupeleka mazao Mji wa Sumbawanga; na kwa kuwa barabara hiyo ina changamoto nyingi sana ya kukwamisha magari.

Mheshimiwa Mwwenyekiti, mwaka 2017/2018 Serikali ilitenga fedha kwa ajili ya kuweka lami kilometa 2 jambo ambalo linaweza likachukua miaka 18 kumaliza barabara hiyo. Kwa nini Serikali isiongeze fedha zaidi kuhakikisha barabara ile inakamilika ili kutoa huduma kwa wananchi?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya mwanzo nimeeleza tu kwamba kwenye mwaka huu wa fedha 2019/ 2020 tutakuja kuliomba Bunge lako Tukufu litupitishie bajeti yetu ili tuweze kutatua changamoto mbalimbali za barabara zetu hapa nchini ambazo zina mtandao mrefu sana na ambao kwa ujumla kabisa tayari upembuzi yakinifu ulishafanyika na tunaendelea na usanifu wa kina kwa maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, jibu lake la kwanza ni kweli kwamba mwaka huu tutatenga fedha nyingi kwa maeneo korofi ambayo yako kwenye barabara niliyoitaja hapo juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kwenye barabara ya Ntendo – Muze kwanza kuna milima mikali sana, na kwa kweli barabara ile ni mbovu na ina changamoto na ndiyo barabara ambayo tunategemea kupata mazao mengi kutoka maeneo hayo. Kuna fedha ambayo tumetenga kupitia TANROAD kwa ajili kwenda kurekebisha maeneo korofi ili barabara iweze kupitika mwaka mzima.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya maandalizi ya awali ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuweka lami barabara muhimu ya Kibaoni-Kasansa-Muze- Kilyamatundu-Kamsamba kutokea Mlowo; ambayo inaunganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara hii ya kutoka Kibaoni mpaka Mlowo imekuwa ikitajwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na pia imekuwa ikitajwa kwenye kila bajeti inayopitishwa na Bunge hili. Je, kutokana na majibu aliyotoa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, barabara imekwisha fanyiwa upembuzi yakinifu? Hivyo basi wanatafuta fedha ili kuja kuiwekea lami.

Je, Serikali haioni sasa kwamba ni hasara kuifanyia barabara upembuzi yakinifu na baadaye kuja kuitafutia fedha kwa ajili ya kuweka lami jambo ambalo utasababisha tena kuja kufanya upembuzi yakinifu mwingine?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi kabisa Serikali ikishafanya upembuzi yakinifu na ikafanya usanifu wa kina huwa hakuna gharama tena ya kurudia zoezi hilo kwa miaka ijayo hata miaka sita, lakini baada ya hapo ndiyo unaweza kufanya tena feasibility study upya baada ya kujiridhisha kwamba kuna mazingira ya kijiografia yaliyosababisha eneo hilo kubadilika, lakini ni ndani ya miaka mitano tunakuwa tumeshaanza kufanya utekelezaji wa miradi mbalimbali baada ya upembuzi yakinifu.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya maandalizi ya awali ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuweka lami barabara muhimu ya Kibaoni-Kasansa-Muze- Kilyamatundu-Kamsamba kutokea Mlowo; ambayo inaunganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya wananchi wa Momba na wananchi wa Kwela kwa ndugu yangu Malocha tunashukuru sana kwa ujenzi wa daraja bora kabisa ambalo nafikiri wananchi tutakavyo kwenda kulizindua wataona kazi ambayo tumeifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja hili ni muunganisho wa hiyo Mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe lakini barabara inayozungumzwa inatokea kwenye Jimbo la Malocha inapitia Jimbo langu halafu inakwenda mpaka katika halmashauri ya Wilaya ya Mbozi. Ni barabara ndefu zaidi ya kilomita mia mbili na kitu, na barabara hii inajumuiya ya watu wasiopungua zaidi ya 150000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachoomba ni commitment ya Serikali ni lini itakwenda kuanza ujenzi ili wananchi hawa sasa wapate barabara ya lami kama ambavyo ahadi ya Mheshimiwa Rais Kikwete na ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Magufu itekelezwe kabla ya kumaliza mwaka huu wa uchaguzi. Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli eneo lile lina watu wengi lakini kwa kweli ni eneo la kimkakati kwa sababu kuna uzalishaji mzuri sana wa mazao mbalimbali ambayo yanasaidia kwenye uchumi wa nchi. Kama nilivyozungumza hapa awali tunaleta bajeti yetu hivi karibuni, tunaliomba sana Bunge lako Tukutu litupitishie bajeti yetu halafu tuanze ujenzi baada ya kupata fedha mara moja.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya maandalizi ya awali ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuweka lami barabara muhimu ya Kibaoni-Kasansa-Muze- Kilyamatundu-Kamsamba kutokea Mlowo; ambayo inaunganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?

Supplementary Question 4

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. Tunayo barabara ya kutoka Mbalizi kwenda Wilaya ya Songwe, Mbalizi ni Mkoa wa Mbeya na Songwe ni Mkoa wa Songwe na TANROADS Mbeya, TANROADS Songwe tayari kuna mgawanyiko wa kugawana hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Ilani na kwenye agizo la Mheshimiwa Rais barabara hiyo yenye kilometa 91 na ilishafanyiwa tayari upembuzi kilometa 56 kutoka Mbalizi mpaka Galula ili iweze kupata lami, lakini mpaka leo kupo kimya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iniambie ni lini watafanya upembuzi yakinifu ili tuweze kupata lami kutoka Mbalizi mpaka Mkwajuni?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge amekiri kabisa kwamba kuna kipande cha barabara kutoka Mbalizi mpaka Songwe ambacho upande mmoja tayari umekwisha fanyiwa upembuzi yakinifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunatafuta fedha hivi karibuni TANROADS upande mwingine wa pili wataanza kufanya upembuzi yakinifu ili tuwe na upembuzi yakinifu wa jumla wa kilomita 91 kwa ajili ya kuingiza kwenye mipango ya kuanza kufanya utekelezaji wa kujenga kwa kiwango cha lami.