Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Daraja la Godegode limesombwa na maji wakati wa mvua za masika na daraja hilo ni kiungo kikubwa kati ya Jimbo la Kibakwe na Jimbo la Mpwapwa ambalo ndiyo Makao Makuu ya Wilaya Mpwapwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja hilo ili kurudisha mawasiliano kati ya Wananchi na Kata za Godegode, Pwaga, Lumuma, Mbuga na Galigali?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili. Kwa kuwa daraja lililosombwa na maji lilijengwa kwa gharama ya shilingi milioni 500 na limesombwa na maji, leo mnajenga daraja la shilingi milioni 325 hilo si ndiyo litachukuliwa mapema. Kwanini msiongeze fedha Mheshimiwa Naibu Waziri?

Swali la pili kwa kuwa barabara ya kutoka Mpwapwa, Lupeta, Mbori, Makutupa, Chamkoroma, Mlali mpaka Pandambili ni barabara muhimu sana kwa Majimbo mawili. Jimbo la Mheshimiwa Spika Mheshimiwa Ndugai Kongwa na Mpwapwa. Na kwa kuwa barabara hili huwa linatengewa fedha kidogo sana kwa ajili ya ukarabati.

Je, ni lini mtatenga fedha za kutosha ili barabara hii iweze kutengenezwa?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Lubeleje, kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niruhusu nimpongeze sana Mheshimiwa Lubeleje, mimi siku hizi namuita mzee wa Godegode, anafuatilia sana ujenzi wa daraja hili na Godegode na maeneo mengine. Nikiri kwamba ni kweli, kama Mheshimiwa Mbunge anavyosema, kwamba daraja hili lililokuwepo lilijengwa muda mrefu na lilijengwa kwa gharama alizozitaja Mheshimiwa Mbunge, kwa milioni 500. Katika jibu langu la msingi nimezungumza juu ya kutenga milioni 325 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuhakikishie kwanza Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii itafanyika vizuri tunafanya shughuli ya ujenzi kwa kutumia utaratibu wa design and construction. Kwa maana hiyo niseme tu kwamba tumetenga milioni 325 kwa ajili ya ule usanifu ambao utachukua muda mfupi sana kwasababu tutafanyakazi wenyewe kupitia wakala halafu baadaye tutaanza kujenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nikuhakikishie Mheshimiwa Lubeleje ukiangali kwenye kitabu chetu cha bajeti ukurasa 323 utaona kwamba pamoja na fedha hizi nilizozitaja kwamba baada ya design tutaanza kujenga na tumetenga milioni 180 ili sasa approach ya Kilomita 6 kwenye daraja la Godegode ili ujenzi uende sambamba kwa hiyo kuna fedha zingine milioni 180 tumezitenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalenga kwamba katika ujenzi wetu maeneo haya Godegode na maeneo mengine kusimamia vizuri ili gharama za ujenzi ziende chini huu ni mkakati wetu kama Wizara sio kama kujenga kwa fedha nyingi tumejipanga ili kusimamia vizuri gharama za ujezi ziweze kupungua. Mheshimiwa Lubereje utakubaliana na mimi kwamba sehemu ambapo daraja hili lipo ni sehemu ambayo imejengwa muda mrefu na mmomonyoko ni mkubwa na urefu wa daraja lile ni kubwa sana. Sasa tumejipanga kwamba kwenye daraja na godegode upande wa kulia kwake kama unaelekea kibakwe kwa maana kwamba tutalijenga upande kulia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalenga kwamba span ya daraja lile itakuwa fupi, sasa span ikiwa fupi gharama ya ujenzi zitapungua, span ikiwa fupi pia tutatumia muda ili wananchi haya waweze kupata huduma za kupita katika maeneo haya. Na kwa maana hiyo pia tumejipanga ndio maana nikasema tutakuwa na approach tutaboresha ili ku- control mmomonyoko ili daraja hili liwe bora. Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubereje nikutoe wasiwasi kwamba tumajipanga vizuri kwamba tumejipanga vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu B Mheshimiwa Lubereje anasema kumekuwa bajeti ndogo katika eneo la mpwapwa, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mpwapwa ni kati ya Wilaya zilizokuwa katika Mkoa wa Dodoma ambayo ni Makao Makuu na Mpwapwa ndio wilaya pekee ambayo haijaunganishwa vizuri na mkoa wa Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tumejipanga kama Serikali kufanya Mpwapwa iwe na barabara nzuri ili sasa iweze ku-support kazi nyingi ambazo zinafanyika katika Makao Makuu. Na kwa ushahidi tu Mheshimiwa Mbunge anafahamu tutaanza ujenzi wa lami kuanzia Mpwapwa kilometa kadhaa kuja kongwa. Lakini Mheshimiwa Lubereje nikuhakikishie kwamba kutoka Mpwapwa kwenda Gulwe kwenda Rudi, Chipogolo na penyewe tunasanifu kwa ajili ya ujenzi wa lami. Na barabara uliyo itaja barabara ya pandambili, Mlali Nghambi yapo kama maeneo manne matano ambayo tumeyatengea fedha za kutosha eeh…

MWENYEKITI: Ahsante

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): …sehemu korofi tumetengea milioni 120 kuna daraja pia milioni 150, tatu kuna zaidi ya milioni 600 ambazo tumezipanga katika mwaka huu wa fedha unaokuja ili kuifanya mpwapwa nao iweze kupata huduma za barabara.