Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza:- Usanifu na upembuzi yakinifu wa barabara ya kutoka Mwanza – Solwa – Bulige kwa kiwango cha lami umekamilika:- Je, ni lini mradi huu utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba pia nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, ndugu yangu Chifu Kwandikwa kwa majibu mazuri aliyoyatoa. Pamoja na majibu hayo mazuri nilikuwa naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara kubwa tatu zinazopita Jimbo la Msalala kwa maana ya barabara hii ya Solwa - Kahama kupitia Bulige; Busisi, Nyang’hwale - Kahama na Kahama – Geita, zote upembuzi yakinifu ulishakamilika. Bajeti ya mwaka huu mwezi Juni, tulipitisha fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kahama - Geita. Barabara hii imekuwa ni kero kubwa, nilitaka kujua na wananchi wafahamu ni hatua gani sasa imefikiwa ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kahama - Geita kuanzia pale Manzese – Segese - Bukoli - Geita?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maige, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa Mbunge alivyozungumza ukiangalia kwenye ukanda ule barabara hizi zote zinahusiana. Sisi kama Serikali tumejipanga kufanya barabara hizi ziwe kwenye mnyororo mzuri. Mheshimiwa Maige anafahamu hatua nzuri tuliyofikia ya ujenzi wa barabara hii kutoka Kahama kupitia maeneo aliyoyataja ya Bulige, Jimbo la Mheshimiwa Bukwimba kwenda mpaka Geita Mjini. Tumejipanga na tupo kwenye hatua za mwisho kuanza ujenzi wa barabara hii muhimu. Hatua hii sasa itapunguza urefu wa barabara hii ambayo Mheshimiwa Nassor naye ameuliza hapa na nimejibu muda uliopita kwa maana itaunganisha barabara hiyo kwa maana ya kupita kwenye mji wa Nyang’hwale.

Mheshimiwa Spika, hata barabara hiyo niliyojibu kwenye swali la msingi inapita kwenye maeneo mengi, alijaribu kutaja maeneo machache. Kimsingi inagusa Jimbo la Misungwi, inapita kwenye eneo la Kwimba na inaunganisha pia Jimbo la Solwa, Msalala na Mji wa Kahama.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwa wananchi wa Kahama kwa ujumla na wananchi wa Mkoa wa Geita na Mwanza kwamba tumejipanga vizuri, tutaenda kwa awamu hivyo hivyo. Barabara hii kubwa itaanza lakini pia barabara hizi zingine tuko kwenye mpango wa kuzishughulikia. Tukionana baadaye ataangalia pia kwenye mpango mkakati wetu kama Wizara tumejipangaje hatua kwa hatua kukamilisha barabara zote hizi. Nampongeza sana kwa umahiri mkubwa katika kuwahudumia wananchi wa Msalala.