Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Je, kwa nini mikopo ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu imekuwa ikitolewa kwa ubaguzi?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru, wanafunzi wengi waliokuwa wanasoma shule binafsi wamekuwa wakinyimwa mikopo ya elimu ya juu kwa kigezo kuwa wazazi wao wana uwezo wa kuwalipia. Je, ni kwa nini sasa Serikali isifute kigezo hicho kwa sababu si wanafunzi wote wanaosoma binafsi wana uwezo, lakini wengine wamekuwa wakienda binafsi kwa kukosa nafasi katika shule za umma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Halima Bulembo ni kati ya Wabunge wanaowakilisha vijana Bungeni na hakika na hili sidhani kama ni la mjadala, amejitahidi sana katika miaka hii muhimu kufanya kazi yake vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina hakika vijana wenyewe wanamfuatilia na hata anapouliza swali hili sasa la leo, ni katika jitihada hizo za kuwakilisha vijana katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sheria yetu inayotuongoza kwenye mikopo haibagui watoto wanaosoma kwenye shule binafsi. Sheria inataka tu tutumie vigezo vile vya kuangalia uwezo wa mtu kujilipia masomo ya chuo kikuu. Kwa hiyo, kinachofanyika ni kwamba, waombaji wote tunawafanyia kitu kinaitwa minutes testing, wanajaza fomu, tunangalia taarifa na kuangalia kama wanaweza wakajifadhili. Kwa hiyo, mtu anaweza akawa amesoma kwenye shule binafsi, lakini kumbe amefadhiliwa, tunachoomba, kama mtu amefadhiliwa, alete ushahidi, alete kiambatisho wakati anajaza fomu.

Mheshimiwa Spika, mwaka huu, kuna wanafunzi 500 ambao wamesoma shule binafsi, wengine wamesoma mpaka Feza School, lakini kwa sababu wameleta uthibitisho wa kwamba wamesomesha na wazazi wao hawana uwezo, tunawasomesha. Kwa hiyo, naomba niendelee kutoa rai na ufahamu kwamba, kusoma kwenye shule binafsi siyo kigezo cha kukosa mkopo! Tunaaangalia uwezo, inawezekana mtu amesoma lakini kafadhaliwa.

Mheshimiwa Spika, naomba vilevile ifahamike kwamba, tuna rasilimali kidogo na tuna wahitaji wengi, ndiyo maana, kama tukipata fursa ya kutoa mikopo, tutatoa kwanza kwa wale ambao hali zao ni mbaya zaidi, kabla hatujatoa kwa wengine kwa sababu tunataka tulete ulinganisho katika elimu. Tunafanya kitu kinachoitwa equity, kwa hiyo, hakuna upendeleo, ni sheria ambayo imetungwa na Bunge hili, ndiyo inatuelekeza.

Mheshimiwa Spika, na katika miaka hii tumefanikiwa kuendelea kuongeza wigo wa wanafunzi wengi kupata mikopo na ndiyo maana mwaka huu tumeweza kuongeza kutoka wanafunzi 41,000 wa mwaka wa kwanza, hadi kufikia wanafunzi 45,000. Nina hakika tutaendelea kuboresha taratibu hizo za kutoa mikopo na ikiwezekana huko mbele ya safari, kadri uwezo utakavyoruhusi, inawezekana hata kila mtu yeyote anayetaka mkopo akapata. Isipokuwa tunapenda kuendelea kusisitiza kwamba ule ni mkopo. Kwa hiyo, kama mzazi ana uwezo wa kumsomesha mwanaye, asitafute mikopo kwa sababu baadaye atawajibika kulipa.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Je, kwa nini mikopo ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu imekuwa ikitolewa kwa ubaguzi?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Ili uweze kwenda chuo kikuu ni lazima uwe na ufaulu unaostahili na ufaulu huu unategemea jinsi ambavyo wanafunzi wametengenezwa, wanafunzi wamejengwa kuanzia ngazi ya Msingi hatimaye Sekondari, A-Level na O- Level.

Mheshimiwa Spika, hali ya ufaulu ndani ya Mkoa wa Lindi ni mbaya, ni mbaya! Mkoa wa Lindi bila kuzungusha, umekuwa wa mwisho katika ufaulu. Kwa misingi hii, kuwa wa mwisho si tatizo, unaweza ukawa wa mwisho katika mazingira ya kufanya vizuri, lakini unaweza kuwa wa mwisho katika mazingira ya kufanya vibaya.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa kuwa, Lindi tumekuwa wa mwisho katika mazingira ya kufanya vibaya, Je, Serikali ina mpango gani wa kuangalia changamoto zilizojitokeza ndani wa Mkoa wa Lindi mpaka kuwa wa mwisho? Na hii itapelekea kwamba kama Mheshimiwa Waziri husika akija na kuangalia nini changamoto zinazokabili Mkoa wa Lindi kuwa wa mwisho? Naomba Mheshimiwa Waziri, atengeneze ziara ili aje atambue changamoto zinazokabili Mkoa wa Lindi, pamoja wana Lindi wenyewe wameshakaa vikao vya mkakati kuangalia changamoto hizo. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze mama yetu Mama Salma Kikwete, hakika amekuwa mama mpambanaji sana kuhakikisha elimu inasonga mbele kwa wato wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nilichukue jambo hili na ni kweli, Lindi imekuwa haifanyi vizuri na ndiyo maana hapa kipindi cha katikati, Ofisi ya Rais TAMISEMI kuona hivyo, niliweza kumtuma Naibu wangu Waziri Waitara alikwenda Mkoani Lindi kwa ajili ya kutembelea miongoni mwa shule mbalimbali na mambo mengine.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo lengo letu kubwa ni kuboresha shule zile kwanza mazingira yawe rafiki zaidi na ndiyo maana maombi ambayo Mama Kikwete naye aliyaomba hasa katika shule mfano kama ile Lindi Sekondari. Ndiyo maana hata katika kipindi cha sasa hivi hapa, tutakwenda kuifanyia ukarabati shule yote ya Lindi Sekondari, lakini siyo Lindi Sekondari, isipokuwa kuzipitia shule za Lindi kuziweka katika mazingira rafiki.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mwenyewe nitafanya ziara maalumu Mkoani Lindi kwa ajili ya kuhakikisha jinsi gani tunafanya kuufanya mkoa huu sasa uinuke kielimu na ndiyo maana hata katika mgao wa walimu, kipaumbele chetu sasa hivi tunaona kwamba jinsi gani hata badaye tupeleke walimu wa kutosha na hata uhamisho wa walimu katika Mkoa wa Lindi hivi sasa tumesimamisha kaika mkoa ule kwa lengo kubwa kwamba mkoa huu tuweze kuu-promote uwe katika hali nzuri.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mama yangu Salma Kikwete. Kwanza nimpongeze sana mama Salma Kikwete kwa kazi nzuri ambayo anaifanya katika kuhakikisha kwamba elimu inasonga mbele na hasa kwa mtoto wa kike.

Mheshimiwa Spika, na kuhusiana na swali lake, pamoja na majibu mazuri ambayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI ameyazungumzia kuangalia miundombinu, nami nimuahidi Mheshimiwa Mama Salma Kikwete kama Wizara ya Elimu, ambayo kazi yetu ni kuweka Sera ya Elimu na kuhakikisha kwamba viwango vya elimu vinafikiwa, tutafanya ukaguzi maalum katika Shule za Mkoa wa Lindi, ili tuweze kubaini changamoto ambazo zinapatikana na tuweze kuchukua hatua mahususi kuhakikisha kwamba Mkoa wa Lindi unainuka katika ufaulu kwa wanafunzi ambao wanasoma katika shule za sekondari na shule za msingi.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Je, kwa nini mikopo ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu imekuwa ikitolewa kwa ubaguzi?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. LYIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu ya Serikali, kilio kikubwa cha wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu ni pamoja na tozo ya asilimia moja kwa ajili ya administrative costs za bodi. Nilitaka kujua, Serikali haioni kwamba huku ni kuwaibia wanafunzi? Kwa sababu tunajua tuna bodi nyingi ambazo hazitegemei makato ama ya watumishi au ya wafanyakazi wake, ni kwa nini Bodi ya Mikopo unawatoza wanufaika asilimia moja kwa ajili ya administrative costs za bodi!

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, Serikali inatoza tozo ya asilimia moja kama management costs kwa ajili ya mkopo unaotolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu, lakini ifahamike kwamba, kazi ya kuweza kufuatilia na kutoa mikopo ile ina gharama kubwa na ni kawaida katika utoaji wa mikopo, kwamba mkopo ule vilevile uweze kugharamia uendeshaji wake, vinginevyo inahitaji utafute fedha za ziada ili kuendesha ule mkopo.

Mheshimiwa Spika, asilimia moja anayosema Mheshimiwa Mbunge, inatozwa mara moja, haitozwi kwa mwaka. Kwa hiyo, ni one off payment na ukiangalia, ukilinganisha sisi tunachotoza na nchi zingine, sisi tunatoza asilimia ndogo sana, hata kwenye tozo zingine kwa ujumla wake. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hii ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha kwamba utoaji wa mkopo unafanyika kwa ufasaha zaidi.

Mheshimiwa Spika, na nimhakikishie tu kwamba, asilimia hiyo moja, imetuwezesha katika hii miaka minne kuongeza marejesho ya mikopo kutoka shilingi bilioni 23 toka mwaka 2015/2016 mpaka sasa kufikia bilioni 183 mwaka huu. Ile fedha inatusaidia kufuatilia kwa sababu watu ambao hawataki kutoa ni wengi, ina gharama. Kwa hiyo, naomba ajue tu kwamba lengo letu siyo kuwaumiza wanafunzi wala wazazi lakini ni kuhakikisha kwamba mikopo ile inarejeshwa na inatolewa kwa utaratibu ambao ni mzuri na yeye mwenyewe ni shahidi, yeye mwenyewe ameshatusifu mara nyingi kwamba tumefanikiwa sana kwenye elimu ya mikopo ya elimu ya juu.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Je, kwa nini mikopo ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu imekuwa ikitolewa kwa ubaguzi?

Supplementary Question 4

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi. Ukosefu wa Ofisi za Bodi ya Mikopo kwa upande wa Zanzibar umekuwa ukileta usumbufu mkubwa sana kwa wazazi na wanafunzi kusafiri kuja Dar es Salaam kwa ajili ya huduma hizo.

Mheshimiwa Spika, ukizingatia hali duni ya wazazi, ni lini Serikali itasogeza huduma hizo kwa upande wa Zanzibar. Ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kumekuwepo na changamoto hiyo ya ofisi kutoka Zanzibar, lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba tayari kuna jitihada za kuhakikisha kwamba ofisi inakuwepo Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, pia, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, pamoja na ofisi kutokuwepo, bodi ya mikopo imeendelea kurahisisha namna ya kuomba mikopo na kurejesha, kiasi kwamba unaweza ukafanya maombi na kurejesha popote ulipo kwa sababu siku hizi kuna teknolojia, lakini naomba vilevile nimhakikishie kwamba bado kuna jitihada za kuhakikisha Zanzibar nayo inakuwa na ofisi.