Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Mwantum Dau Haji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Dalili za maji safi na salama kuchanganyika na maji chumvi (bahari) zinatishia ustawi. Je, nini utatuzi wa tishio hili?
Supplementary Question 1
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mazingira kwa suala lake zuri ambalo alilolitoa hivi sasa hivi hapa. Lakini pia nimpongeze kwa suala langu la Bunge lililopita wakaja Zanzibar wakaja kutuhimiza ahadi yake ya kuja kuangalia mambo ya hali ya hewa ya mmomonyoko wa ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza, kwa kuwa mikoko ina mchango mkubwa wa kunusuru mazingira nini mpango wa Serikali katika kuhakikisha inaotesha mikoko ambayo inauwezo wa kunusuru maji chumvi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili bila maji baridi hatima ya kilimo na uhai wa binadamu viko hatarini. Je, kuna tafiti zozote za kuyalinda kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji baridi ahsante? (Makofi)
Name
Mussa Ramadhani Sima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ridhaa yako nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji Mbunge wa Viti Maalum ni kweli amekuwa mstari wa mbele na sasa hivi amekuwa mwana mazingira tunamtumia sana hasa kwenye eneo hili la Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru kwa maswali yake mawili; moja, tunao mkakati maalum na unaendelea kwa kushirikisha wenzetu wa Serikali za Mitaa hasa kwenye halmashauri zetu kuhakikisha wanaweka miche kwa ajili ya mikoko ambayo itatumiwa kwenye maeneo hayo tuliyoyaeleza ya Pwani pembezoni mwa bahari. Na mkakati huo unaendelea na miche ipo ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namba mbili, utafiti zinaendelea na mpaka sasa tupo na utafiti unaendelea na wakati wowote tutaweka suala hili katika utaratibu ambao tutahakikisha maeneo haya kunakuwepo na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwenye kila eneo ambalo kuna mwambao wa bahari ahsante sana.
Name
Saada Salum Mkuya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Welezo
Primary Question
MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Dalili za maji safi na salama kuchanganyika na maji chumvi (bahari) zinatishia ustawi. Je, nini utatuzi wa tishio hili?
Supplementary Question 2
MHE. SAADA SALUM MKUYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa fursa nikauliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri tunajua ama ni ukweli kwamba mazingira hasa kwenye upande wa carbon and mission ni nchi ambazo zilizoendelea ndio zinazo- emit hii carbon na athari kubwa inatokea kwa nchi ambazo zinaendelea ikiwemo Tanzania. Lakini nchi hizo ambazo zinaharibu sana mazingira haya zimekuwa zinasita kutoa finance kwenye climate change. Labda Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejipangaje kuhakikisha kwamba inapambana katika kukabiliana na matatizo haya ya climate change ikiwemo mitigation adaption? (Makofi)
Name
Mussa Azzan Zungu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ilala
Answer
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri ni kweli kuna baadhi ya nchi kubwa duniani ambazo zimejitoa kwenye mkataba huu wa tabianchi kutokana na maslahi yao binafsi, lakini vilevile nchi zilizobakia zikiongozwa na Ufaransa na Qatar na nchi zingine wameanzisha mfuko wa one bilioni 100 Us dollars ambazo zitatumika kwa nchi zote ambazo zitahitaji pesa hizi kuboresha mazingira katika nchi zao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania hatuko nyuma tulishaanza mkakati wa kuziomba pesa hizi na program mbalimbali za kuhakikisha nchi yetu inafaidika na pesa hizi na kulinda mazingira. Programu ya kwanza ni kuhakikisha tunapanda miti Mlima Kilimanjaro zaidi ya miti bilioni moja ili kulinda barafu ambayo ipo katika nchi yetu. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved