Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Tarafa ya Wampembe ina Kata za Kala, Wampe mbe, Kizumbi na Ninde na ambazo zote ziko umbali wa zaidi ya km 80-150 kutoka Makao Makuu au mahali ambapo huduma za Mahakama zinaweza kupatikana:- Je, ni lini Serikali itajenga walau Mahakama ya Mwanzo katika moja ya Kata hizo hususani Kata ya Wampembe ili kusogeza huduma hiyo kwa Wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana nishukuru sana majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza katika majibu ya Serikali nimeeleza kwamba kuna juhudi zinafanyika za kupata eneo ili jengo la Mahakama ya Wampembe lipatikane. Lakini niseme tu kwamba tatizo la kupata eneo si tatizo kupata eneo mimi na wananchi tunaahidi kutoa eneo kwa haraka. Tunaiomba Serikali kupitia na kwa vile sasa hivi tunaenda kwenye bajeti.

Je, Serikali itakuwa tayari kuweka au kutenga pesa ya ujenzi wa jengo hilo la Mahakama ya Wampembe kwa mwaka huu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kupitia bajeti ya Serikali tumekuwa tukiahidiwa wananchi wa Nkasi kupata Mahakama ya Wilaya miaka mitatu mfululizo na leo kwenye kupitia majibu ya swali hili Serikali inatoa ahadi kwamba mwezi wa tani ujenzi huo utaanza. Je, zile sababu ambazo zipelekea tukashindwa kujenga na wananchi wakaanza kutuona Wabunge tunapoenda kuwaaambia tutapata jengo kwamba ni waongo? Je, zimeondoshwa? (Makofi)

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ingawa hatutajenga Mahakama katika eneo hilo mwaka huu katika bajeti yetu lakini tutatoa kipaumbele katika bajeti itakayofuata mwaka kesho kama inaavyosema tufanye kazi kwa pamoja na tutajitahidi kutumia Mahakama ambayo sasa hivi iko katika hilo jengo ambalo tumeliazima lakini tunajitahidi tuingize katika bajeti ya mwaka kesho suala hili la ujenzi wa Mahakama haki. Tunatoa kipaumbele kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lako la pili tumejitahidi na mmjeitahidi na tunashukuru tumeondoa vikwazo vyote tumeingiza kwenye bajeti ya mwaka huu na mwezi Mei, nakuhakikishia ujenzi wa Mahakama hiyo utaanza bila wasiwasi ahsante sana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Tarafa ya Wampembe ina Kata za Kala, Wampe mbe, Kizumbi na Ninde na ambazo zote ziko umbali wa zaidi ya km 80-150 kutoka Makao Makuu au mahali ambapo huduma za Mahakama zinaweza kupatikana:- Je, ni lini Serikali itajenga walau Mahakama ya Mwanzo katika moja ya Kata hizo hususani Kata ya Wampembe ili kusogeza huduma hiyo kwa Wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni wilaya ambayo ilianzishwa mwaka 75 leo ina umri wa miaka 45. Wilaya ile ina kata 20 lakini Mahakama mbili tu Mwanzo, na Mahakama ya Mwanzo ya Liwale Mijini ndio inayochangiwa na Mahakama ya Wilaya kwa maana kwamba Mahakama ya Wilaya hawana jengo. Lakini nilipouliza swali hili mwaka 2017 Mheshimiwa Kabudi akiwa hapo kwenye hicho kiti alisema mwaka 2018 inajengwa hospitali ya Wilaya. Je, Serikali kwenye majibu yale mlikuwa mnanidanganya?

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyoelewa ni kwamba huwa kunakuwa na jitihada za pekee, kama Waziri anatoa majibu, anafanya kila njia kuweza kuhakikisha kwamba inatekelezwa. Ningependa kurudi na kutazama rekodi za mazungumzo hayo na jitihada ambazo zilifanywa, lakini Liwale ni mahali ambapo kama ulivyoona mchakato wa kufungua Mahakama katika Wilaya za Lindi na Mtwara, umekuwa ukiendelea kwa kasi sana. Kama kulikuwa na ahadi kama hiyo, Wizara tungependa kufuatilia na Mahakama iendelee kujitahidi kutekeleza ahadi hizo.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Tarafa ya Wampembe ina Kata za Kala, Wampe mbe, Kizumbi na Ninde na ambazo zote ziko umbali wa zaidi ya km 80-150 kutoka Makao Makuu au mahali ambapo huduma za Mahakama zinaweza kupatikana:- Je, ni lini Serikali itajenga walau Mahakama ya Mwanzo katika moja ya Kata hizo hususani Kata ya Wampembe ili kusogeza huduma hiyo kwa Wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kwa ridhaa yako naomba niipongeze Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa utekelezaji wake wa Ilani wa ujenzi wa Mahakama za Wilaya nchini Tanzania. Tunashuhudia Mahakama mbalimbali za Wilaya zikizinduliwa zikiwemo za Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niulize swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuboresha Mahakama za Mwanzo za Kariakoo, Magomeni, Ilala, Temeke na Mbagala?

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Dar es Salaam ni mahali pa watu wengi, mashauri ni mengi na kioo cha Taifa na cha Wizara yangu. Ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba Mahakama hizi zinakuwa na sura nzuri na zinafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuboresha ina maana tatu. Kwanza ni kufanya ukarabati wa kuhakikisha kwamba Mahakama hizi ziko katika hali nzuri. Kuboresha pia kunamaanisha kwamba, Mahakama hizi zipewe teknolojia ya kisasa hasa katika uwezo wa kuandikisha Mahakama na kuweza kusikiliza kesi hizi. Tunaingiza utaratibu wa teknolojia ya kuweza kusikilizwa kesi hizi na kuandikisha na Mahakama za Dar es Salaam zinapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika mkakati wetu wa kutumia magari ya kusikiliza kesi, tumeanza utaratibu huo na kufanya majaribio katika Mkoa wa Dar es Salaam. Katika uboreshaji wa aina hii mwanzo itakuwa ni Dar es Salaam kabla hatujapeleka sehemu nyingine zaidi.