Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Ujenzi wa Jengo la Utawala na vyumba vya madarasa katika Chuo cha Uuguzi Korogwe bado haujakamilika:- Je, ni lini ujenzi huo utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa majengo yanayotumika sasa hivi yana uchakavu mkubwa na ya muda mrefu, je, watakuwa tayari sasa angalau kuwapa fedha waweze kukarabati yale majengo ambayo yanatumika sasa hivi ikiwa ni pamoja na uzio?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, chuo kile kina uhaba wa watumishi wa kada ya ualimu watano pamoja na karani, mpiga chapa na mtu wa IT. Wizara itakuwa tayari kutusaidia angalau kuweza kupatikana hao walimu watano pamoja na hao watumishi wengine niliowataja?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kumpongeza sana Mheshimiwa Mary Pius Chatanda, Mbunge wa Korogwe Mjini kwa ufuatiliaji wa karibu sana wa chuo hiki na niliweza kufika katika chuo kile na kuona hali ya majengo. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge hili sisi kama Wizara tunalichukulia kwa kipaumbele cha hali ya juu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi sasa hivi tuko katika zoezi la kufanya uhakiki kuangalia mahitaji, vipaumbele na kitu gani ambacho tunahitaji kukifanya kwa haraka zaidi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pindi utaratibu huu utakapokamilika basi chuo hiki nacho tutakipa kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo vilevile amegusia suala la uhaba wa watumishi. Hili kama Wizara tumelipokea na tumekuwa tunaendelea kufanya tathmini katika vyuo vyetu hivi vya afya. Kadri tunavyopata vibali vya ajira basi na chuo hiki nacho tutakipa kipaumbele kupata hawa watumishi ambao wamepungua.