Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Mwantum Dau Haji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Kasi ya mmomonyoko wa ardhi na uhaba wa udongo katika Visiwa vya Unguja na Pemba inatishia uhai wa Visiwa hivyo:- Je, ni hatua zipi za makusudi zimechukuliwa katika kuvinusuru Visiwa hivyo?
Supplementary Question 1
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu ya kina kuhusu swali langu hili, nampongeza sana, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, yamekuwepo matukio ya ongezeko la kina cha bahari kiasi cha kuwepo kwa tishio la kimazingira katika baadhi ya maeneo. Je, Serikali inasema nini kuhusiana na suala hilo katika Visiwa vya Unguja na Pemba?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tatizo hili ni la muda mrefu kweli, toka lilivyogundulika kuhusu mazingira katika Visiwa vyetu vya Pemba na Unguja. Mheshimiwa Naibu Waziri atakuja lini sasa Zanzibar kuangalia maeneo yaliyoathirika katika Visiwa vya Pemba na Unguja? Nataka unihakikishie utakuja lini Zanzibar mbele ya Bunge letu hili.
Name
Mussa Ramadhani Sima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mwantum Dau Haji kwani amekuwa mdau mzuri wa eneo hili la mazingira. Nimhakikishie tu kwamba katika miradi ambayo inaendelea na kama nilivyosema kwamba tunashirikiana vizuri na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar sasa tunaifanyia tathmini. Katika tathmini ile ambayo tunaifanya kila baada ya miezi mitatu maana yake sasa nitakuja rasmi baada ya Bunge hili, walau siku mbili hivi kwa ridhaa ya Mwenyekiti, ili tukishirikiana nawe na Wabunge wengine kwenye maeneo ya Pemba kuyaona hayo maeneo vizuri na kuhakikisha tunayapatia ufumbuzi wa kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Name
Dr. Immaculate Sware Semesi
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Kasi ya mmomonyoko wa ardhi na uhaba wa udongo katika Visiwa vya Unguja na Pemba inatishia uhai wa Visiwa hivyo:- Je, ni hatua zipi za makusudi zimechukuliwa katika kuvinusuru Visiwa hivyo?
Supplementary Question 2
MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Suala la mmomonyoko wa udongo ni kubwa na lipo dhahiri kabisa, ukiona mkusanyiko wa udongo na mchanga katika mapito ya njia za maji za mito. Kumekuwa pia na uchimbaji holela wa michanga hii, inazidi kuvunwa au pia vina vya maji vinakuwa vifupi na nyakati za mvua basi husababisha mafuriko. Wizara husika ina mkakati gani kuleta suluhisho katika suala hili ambalo ni muhimu sana na lina effect kubwa sana katika mazingira?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
Name
Mussa Ramadhani Sima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Sware.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikubaliane naye kumekuwa na changamoto kubwa sana ya mmomonyoko wa ardhi hasa kwenye maeneo ambayo kuna mapito ya maji. Eneo hili kwa kweli nikiri kabisa tumeendelea kulifanyia kazi na limekuwa na changamoto kubwa. Mkakati uliopo ni kuhakikisha maeneo yote haya kwa kushirikiana na viongozi wa Halmashauri wanatupa taarifa zilizo rasmi ili kutengeneza miradi ya kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumekuwa tukitoa maelekezo kwenye Halmashauri husika ili kukabiliana na maeneo ambayo yanahitaji kupata ufumbuzi wa muda mfupi lakini yale ya muda mrefu Wizarani tunapata taarifa na tunachukua hatua stahiki.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved