Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake lakini nimfahamishe tu kwamba miaka mitatu iliyopita wananchi wa maeneo ya Mruki, Hangoni, Sinai pamoja na Kwere walizuiwa na Halmashauri kuendelea kuendeleza maeneo yao yaliyohisiwa kwamba ndiko barabara itakapopita wakiwa wamefanyiwa tathimini nakuhadiwa fidia. Je, kwa kauli ya Serikali sasa wananchi hawa wanaruhusiwa kuendelea na majukumu yao ya kuendeleza maeneo yao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa kuwa majibu ya Serikali pia hayajatoa time frame yaaani lini sasa upembuzi huo wa kina utakamilika. Je, Serikali iko tayari kusema ni lini upembuzi utaanza na kukamilika? Ahsante. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze tu Mheshimiwa Mbunge Mahawe kwa sababu amekuwa akifuatilia sana juu ya maendeleo ya Babati na Manyara kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba Halmashauri kuwazuia wananchi au kuwaelekeza wananchi kwa vyovyote vile haikuwa sahihi sana kwa sababu ilitakiwa Mamlaka inayohusika na ujenzi wa barabara ifanye hivyo. Kwa hiyo, niwaombe mahali popote kutakapokuwa na miradi ya barabara tusubiri kupata kauli ya Mamlaka halisi ili tusiweze kuwachanganya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya usanifu inaendelea sasa hivi kuanzia tarehe 01 Julai, 2019 kazi hiyo imeanza na wakati wowote tutapata inspection report, kwa maana ya report ya awali itakapokuwa imepatikana tutaweza kufanya sasa maamuzi, kwa sababu tutakuja na altenative kama tatu, halafu Serikali iamue tuende hatua ya mwisho sasa ya kukamilisha michoro pamoja na kuona kwamba tunapata gharama halisi za kuwafidia wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo uvute subira kazi inaendelea na ninalishukuru sana Bunge lako limetupitishia fedha kwa ajili ya kazi hii ya usanifu wa hii barabara na kwamba kazi itaisha haraka sana, katika mwaka huu wa fedha kwa sababu fedha tunazo na kazi inaendelea itakamilika, gharama zitajulikana na wananchi tutawajulisha wale watakaopitiwa na mradi na Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tuko pamoja hapa taarifa hizi za kuhusu wananchi ni wepi watapitiwa na mradi ili tuweze kuwalipa fidia tutaweza kuwasiliana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kazi kubwa inayofanywa na Serikali katika kuboresha miundombinu ya barabara, lakini kipo kipande cha barabara kutoka eneo la Rusaunga kuelekea Rusumo mpakani barabara inayoelekea Rwanda kimeharibika kuna mashimo utafikiri ni mahandaki, hii inapelekea magari kuharibika na kusababisha ajali zisizo za lazima. Magari sasa yanachepuka kupitia barabara ya Rusaunga, Rurenge, Mrugarama ambayo ni ya vumbi na hivyo kuendelea kusababisha uharibifu kwenye barabara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini commitment ya Serikali katika kuhakikisha kwamba barabara hii inatengenezwa kwa kiwango kinachostahili ukizingatia kwamba ni barabara ya kiuchumi? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii kutoka Rusaunga kwenda Rusumo kilomita 92 ni barabara ambayo imechoka imechakaa ina mashimo, ina mahandaki na imekuwepo kwa miaka mingi sana ni zaidi ya miaka 34 na Serikali imekuwa ikifanya juhudi ya kuiboresha barabara hii kwa sababu imejengwa muda mrefu kutoka Isaka kwenda Rusumo, kwa sehemu kubwa ya barabara hii matengenezo yamekuwa yakifanyika tumebakiza hizo kilomita 92.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote katika Mkoa huu wa Kagera kwamba tumetenga fedha kwenye Bunge hili la kuifanyia matengenezo upya barabara hii, lakini kwa hatua za awali kuboresha haya mahandaki ambayo Mheshimiwa Mbunge anayaita kuna fedha tayari Serikali imeshatoa na tulikuwa tunakamilisha hatua za manunuzi, mkandarasi ameshapatikana tutaanza kwanza kuboresha ili kuyapunguza haya mashimo Mheshimiwa Mbunge, tutayapunguza wakati harakati zile za kuanza mradi mkubwa wa kuboresha barabara hii haya mashimo tutakuwa tumeyaondoa.(Makofi)

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu baada ya kupiga kelele hatimae kuna kila dalili za kujengwa barabara ya Pangani. Nataka kujua sasa je, wale wananchi ambao walielezwa kwamba wasiendeleze mashamba na majengo waliyoko pembezoni mwa barabara, ni lini wataanza kulipwa fidia zao? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejipanga vizuri kujenga barabara hii ya Tanga - Pangani kama Mheshimiwa Mbunge ulivyosema, lakini ni utaratibu wa Serikali ni kulipa fidia kwanza kabla ya ujenzi kuanza, kwa vile Mkandarasi ameshapatikana niwahakikishie tu wakazi wa maeneo haya ambao mradi utapita watalipwa fidia yao mara moja. (Makofi)

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru sana Serikali kwa kutupa barabara nzuri ya kutoka Ndono mpaka Urambo na inakatisha mpaka katikati ya Mji, naishukuru sana Serikali kwa niaba ya wananchi wa Urambo. Swali ni kwamba ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja kuangalia round about ambayo wameiweka pale inasababisha ajali kwa jinsi ambavyo kona iliyopo ni kali sana, magari yanapata ajali, watu wanapata ajali. Kwa heshima na taadhima naomba kujua ni lini Serikali itakuja kutusaidia round about ya Urambo? Ahsante sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisha kwenda Urambo lakini nitakwenda tena kwa sababu nafikiri kuliwa na zoezi hili la kuangalia sehemu bora zaidi ya kufanya marekebisho kuweka round about katika Mji ule. Kwa hiyo, Mama yangu nikuhakikishe kwamba tutakwenda lakini wataalam wanaendelea kukamilisha ili kuona ni wapi patafaa vizuri ili tuweze kuweka huo mzunguko. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza. Swali la kwanza napenda niipongeze Serikali kwa kusikia kilio chetu Wabunge na kilio cha wananchi sasa wameanza kufanya tathmini ya barabara ya Kirwa Road kutoka eneo la Mbagala Kokoto kwenda Kongowe, eneo ambalo lilikuwa na msongamano mkubwa wa magari naiopongeza sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kusikia kilio chetu Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi wa eneo la Mbagala Kokoto mpaka Kongowe wameanza sasa kufanyiwa tathmini ya maeneo yao na kuwekewa alama ya X. Je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kwamba wananchi hawa watalipwa kwa wakati ili kupisha zoezi hilo la upanuzi wa barabara ya Kirwa Road. Ahsante sana? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mbunge najua tumezungumza miradi mingi sana na anafahamu juhudi ambazo zinafanyika ndiyo maana anatoa pongezi, kwa niaba ya Serikali nazipokea pongezi hizo.

Mhehimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumejipanga kuboresha barabara hii ili kuweza kupunguza pia msongamano ambao unajitokeza na usumbufu ambao unajitokeza, nami eneo hili nimelitembelea. Vile vile niwahakikishie tu wananchi hawa kwamba tumejipanga vizuri kwa sababu hata kwenye bajeti tuna fedha kwa ajili ya kuendeleza maendeleo ya maeneo haya na kulipa fidia, tutawalipa mara moja wakati tukiendelea kuboresha mradi huu. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuwa barabara ya Karatu - Mang’ola katika Mkoa wa Arusha imekuwa ikitengenezwa mara kwa mara na kuisababishia Serikali gharama kubwa. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami kwa sababu eneo la Mang’ola ndilo linalotegemewa kwa uchumi wa Karatu kwa sababu lina ulimaji Mkubwa wa zao la vitunguu? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejipanga vizuri kuijenga barabara hii. Barabara hii ni muhimu inaunganisha Mkoa wa Arusha pamoja na Mikoa mingine Ukanda wa Ziwa, kwa hiyo, tuko katika hatua za mwisho kwa sababu kazi ya kufanya usanifu katika barabara hii ilishafanyika tunafanya review na mara tu tutakapopata fedha barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 7

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa changamoto iliyopo katika Bypass ya Babati inafanana kabisa na katika Jimbo letu la Iringa Mjini ambako Serikali imeshabomoa makazi ya watu lakini ujenzi haujaanza. Je, Serikali itaanza lini ujenzi huo ili kupunguza adha kubwa kabisa wanayopata wananchi kwenda katika stendi mpya ya Igumbilo? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejipanga kuijenga barabara hiyo ni kilomita Saba na katika bajeti ya mwaka huu tumetenga fedha kuanza ujenzi wa barabara hiyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ritta Kabati ninakupongeza tu unafuatilia sana barabara hii lakini nikuhakikishie pia kwamba tumejipanga vizuri tunajua usumbufu wananchi wa Iringa Mjini wanaopata wa magari makubwa yanayopita katika ya Mji, kwa hiyo ujenzi wa barabara hii utaanza tu mara moja kwa sababu tumeshajipanga vizuri na tutaendelea kutoa feedback. (Makofi)

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 8

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante pamoja na changamoto za kulipa fidia wananchi katika Taifa hili lakini Mkoa wa Katavi katika barabara ya kutoka Sumbawanga kuelekea Kigoma wakazi wa Kata ya Mpanda hoteli Misukumilo pamoja na Ilembo pamoja na Milala walirukwa katika masuala ya fidia mpaka sasa ni mwaka wa nne hawajalipwa pesa hizo. Je, ni kwanini Serikali mnawazungusha kuwalipa watu hawa ambao walitumia gharama kubwa kujenga nyumba zao?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwa ujumla hii Serikali hii inawajali sana wananchi wake na hakuna sababu ya kutokumlipa mwananchi haki yake. Kwa hiyo, naomba tu nilichukuwe hili kama ni suala mahususi ili nilifuatilie nione nini kilitokea kwa sababu ni nia ya Serikali kuwahudumia vema wananchi na kuwalipa haki zao kwa hiyo, tutalifuatilia suala hili.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 9

MHE. BONAH KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Mheshimiwa Waziri Serikali ina mpango gani kuhusiana na Barabara ya Kimanga, kwa sababu last time Naibu Waziri alienda kufanya ziara lakini ile barabara mpaka sasa hivi imeachwa kutengenezwa. Pia nauliza kuhusiana na daraja la Segerea Seminari ambalo limechukuliwa na maji tangu mwaka 2012 lakini pia ni ahadi ya Mheshimiwa Rais mpaka leo halijatengenezwa ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu anapigania sana barabara za eneo la jimbo lake. Lakini niseme tu ile barabara ya Kimanga kulikuwa na mradi unaendelea nitafuata tu ufuatiliaji nione nini kimetokea kama ule mradi unasua sua na tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge tukatembelee mradi tuone changamoto iliyokuwepo ili tuweze kuitatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu lile daraja la upande ule wa Seminari, nilitembelea eneo hili tunahitaji kuweka daraja kubwa pale, Serikali bado inajipanga kutafuta fedha za kutosha hili tuweze kuboresha katika eneo hili. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba uvute Subira tutajipanga vizuri tutaporesha eneo hili kwa sababu linahitaji fedha nyingi ili kuweza kuboresha mahali hapa ambapo ni sehemu korofi ahsante sana.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Supplementary Question 10

MHE. MWIGULU L. NCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa barabara ya Singida, Sepuka, Ndago, Kizaga kwa kiwango cha lami ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na ipo kwenye ilani ya uchaguzi ukurasa wa 56. Kwa kuwa upembuzi yakinifu katika barabara hii ulishafanyika na Mheshimiwa Naibu Waziri alishafanya ziara kukagua masuala yote katika barabara hiyo ni lini sasa ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza katika barabara hiyo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge nakupongeza sana kwa sababu nimefuatilia kweli barabara hii muhimu na niseme tu ni mwaka wa fedha uliopita ndiyo tulikuwa tunaendelea kufanya kazi ya usanifu wa kina kwa ajili ya Ujenzi wa lami wa barabara hii. Mheshimiwa Mbunge vuta subira kwa sababu tunakwenda kwa hatua baada ya kukamilisha hili zoezi ambalo tulikuwa tunalifanya sasa tunatafuta fedha ili tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami barabara hii muhimu.