Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Je, ni lini Barabara ya Masasi – Nachingwea – Nanganga itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, naomba kwa ruhusa yako unipe nafasi nitoe pole kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi, hasa wananchi wa Kilwa pamoja na Mchinga ambao wamepata maafa ya mafuriko. Sisi kama Wabunge wa Mkoa pamoja na Taifa tunaungana nao na tuko pamoja nao. Pia nikumbushe hoja ambayo ilitolewa na Mbunge mwenzangu jana juu ya kuona umuhimu wa Bunge kuchangia Mkoa wa Lindi, hasa wale wahanga ambao wamepata maafa. Kwa hiyo, kupitia Kiti chako tutaomba mwongozo wako. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hilo, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Mheshimiwa Rais wetu alifanya ziara tarehe 16 Oktoba, 2019 na katika ziara hiyo Mheshimiwa Naibu Waziri aliambatana na Mheshimiwa Rais. Moja ya ahadi kubwa ambayo aliitoa na ambayo wananchi wa Masasi, Nachingwea na Ruangwa wanasubiria ni kuona utekelezaji wa kile ambacho alikitolea maagizo juu ya kuanza kwa ujenzi wa lami kwa barabara hii ambayo kwa muda mrefu wananchi kwao imekuwa kero. Sasa naomba kufahamu kauli ya Serikali kwa nini mpaka sasa bado maagizo yale hayajaanza kufanyiwa kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, Wilaya ya Nachingwea inaungana na Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma. Kwa muda mrefu wananchi wa maeneo ya Tarafa ya Kilimarondo ambao wanaunganishwa na Mto Lumesule wamekuwa wanapata changamoto kubwa sana ya kupata mawasiliano. Naomba kauli ya Serikali kupitia Wizara, wana mpango gani juu ya kufungua barabara hiyo ya Kilimarondo kwenda Namatunu kutokea Lumesule kwenda kuunganisha Tunduru ili tuweze kufungua barabara hii tuweze kunufaika kiuchumi?

Mheshimi Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa Wizara yangu inatekeleza ahadi zote za Ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini pamoja na viongozi wetu wakuu wa Serikali. Ni kweli Mheshimiwa Rais aliahidi na sisi Wizara tunalifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo hatua, baada ya ahadi lazima tujipange na kuandaa bajeti ndiyo tuendelee kutekeleza. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge na sasa hivi ndiyo tunaandaa bajeti, kwa hiyo tutaendelea kutekeleza hilo lakini pia kumbuka kwamba tunapenda kwanza kukamilisha ujenzi wa barabara zote za mikoa halafu baadaye ndiyo twende kwenye regional roads. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia feeder roads kwa vile kuna TARURA kuna ambazo zitaingia kwenye TARURA lakini kuna ambazo zitatekelezwa na Wizara ya Ujenzi. Kwa hiyo, barabara hiyo aliyoisema kwenda Kilimarondo tutaipitia na kuona kwamba itekelezwe na taasisi gani. (Makofi)

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Je, ni lini Barabara ya Masasi – Nachingwea – Nanganga itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Bajeti ya mwaka jana nilipata fedha kwa ajili ya kujenga barabara ya kutoka Igunga kwenda Itumba na barabara ya kutoka Mbutu kwenda Kininginila lakini niliuliza swali Bunge lililopita kwamba kwa nini barabara hizi hazijajengwa na Waziri aliniahidi kwamba wataanza kujenga mara moja lakini hadi sasa barabara hizi hazijaanza kujengwa. Nini kinachojiri huku?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la kaka yangu, Mheshimiwa Dkt. Kafumu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Kafumu, nafahamu kwamba tumeongea mara nyingi juu ya mtandao wa barabara katika Jimbo lake la Igunga na kwa kweli eneo lake hili ni bonde, kuna mabonde makubwa sana. Nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Kafumu kwamba tumejipanga na nimwombe tu baada ya Bunge hili tukutane ili angalau tuweze kupitia kwa upana kabisa juu ya barabara zake na kuona namna ambavyo tumejipanga kuzishughulikia. Ipo mipango mizuri tu, namwomba sana tuonane ili aweze kupata ufahamu wa kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Je, ni lini Barabara ya Masasi – Nachingwea – Nanganga itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya yetu ya Bukoba Vijijini tuna barabara ya kutoka Kanazi – Ibwela – Nakibimbiri – Katoro mpaka Kyaka. Barabara hiyo ni mbovu sana hasa kipindi hiki cha mvua haipitiki. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na uharibifu wa barabara Mkoa wa Kagera, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha barabara nyingi sana zimeharibika na niliagiza TANROADS wafanye makadirio, mpaka tarehe 31 Januari tunahitaji shilingi bilioni 25 kwa ajili ya kurejesha miundombinu ya barabara katika hali waliyokuwa nayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na barabara ambayo ameiulizia, kwa sababu ndiyo ametupa taarifa sasa hivi tutaiangalia na kumuagiza Meneja wa TANROADS ili kwanza tuone, je, ni barabara ya TARURA au ni barabara ambayo inahudumiwa na TANROADS tuweze kuifanyia kazi na Mheshimiwa Mbunge tutamjibu kadiri inatakavyowezekana.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Je, ni lini Barabara ya Masasi – Nachingwea – Nanganga itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo ni mara ya 15 nauliza kuhusiana na barabara muhimu sana ya Chuo cha Ardhi – Makongo – Goba. Mara ya mwisho nilijibiwa tukiwa tunaelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali ya Mtaa ambapo Mkuu wa Mkoa alienda na mkandarasi wakaweka vifaa pale wakawaambia wananchi barabara itajengwa watalipwa fidia. Leo baada ya uchakachuzi mkandarasi ameondoka, ile lami kilometa moja ambayo tulijenga Halmashauri imekwanguliwa, wananchi hawajui mustakabali wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kama mwakilishi wao, naomba Waziri anipe jibu na jibu liwe la ukweli na uhakika, ni lini barabara ya Makongo inayoanzia Chuo cha Ardhi – Makongo Juu – Goba itajengwa kwa kiwango cha lami na wananchi kulipwa fidia yao wanayostahili? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Makongo tayari tumeanza kuijenga, kama unavyosema ni kweli mitambo ilienda lakini huwezi ukajenga barabara katika kipindi cha mvua nzito, huo ndiyo utaratibu, hiyo ndiyo sayansi yake, kwa sababu udongo unakuwa umeloana, kuna kiwango maalum kinachohitajika kwenye maji ya ujenzi wa barabara, huwezi ukafanya ushindiliaji kama moisture content iko high.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na suala la fidia, kwa vile tumeshasaini mikataba tayari fidia ni lazima ilipwe. Huwezi ukajenga barabara bila kulipa fidia lakini pia fidia italipwa kwa mujibu wa sheria. Kama kuna mtu alijenga ndani ya hifadhi ya barabara hatuwezi kumlipa lakini yule ambaye tumemfuata, alikuwa yuko nje ya hifadhi ya barabara, huyo lazima tutamlipa, kwa hiyo fidia italipwa kwa mujibu wa sheria.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:- Je, ni lini Barabara ya Masasi – Nachingwea – Nanganga itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya kuanzia Mombo – Soni - Lushoto ni nyembamba mno hata kuhatarisha maisha ya watu pamoja na mali zao. Je, ni lini upanuzi wa barabara ya Soni – Mombo - Lushoto utaanza ili kuondoa kadhia wanayoendelea kuipata wananchi wa Lushoto?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na barabara ya Mombo – Lushoto, kwamba ni nyembamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara ile ni nyembamba lakini imepita katika milima mirefu na udongo ule uko sensitive sana kwenye erosion. Kwa hiyo, tulijenga katika hali ile lakini baadaye tuta-redesign na kuipanua huku tukiwa waangalifu kwa sababu ni lazima ukate milima. Sasa utakapokata milima maana yake unaifanya tena ielekee kwenye mwelekeo ikinyesha mvua nyingi iweze kubomoka. Mwaka jana Mheshimiwa Mbunge ni shahidi, udongo uli-slide ukaifunika barabara moja kwa moja.

Kwa hiyo, ile barabara lazima ijengwe kwa uangalifu sana kwa sababu udongo wake mvua ikinyesha mara nyingi unaporomoka.