Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Omar Abdallah Kigoda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Primary Question
MHE. OMARY A. KIGODA aliuliza:- Barabara ya Handeni – Mziha ni barabara ya mkakati na ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Je, ni lini Serikali itamalizia kipande kilichobaki kutoka Handeni mpaka Mziha?
Supplementary Question 1
MHE. OMARY A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Handeni - Mziha na barabara ya Handeni- Kibirashi kutokana na mvua hazipitiki sasa hivi. Je, ni nini uamuzi wa Serikali kuhakikisha kwamba wanaokoa zile barabara ziweze kupitika wakati tunasubiri ziwekwe lami ili wananchi waweze kusafirisha mali zao na wao waweze kusafiri?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omary Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza uniruhusu niwape pole sana wananchi pamoja na Mheshimiwa Mbunge Kigoda kwa sababu maeneo yale nilitembelea walipata shida kubwa sana wakati wa mvua ilipokuwa kubwa na maji yalikuwa mengi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake tumechukua hatua za dharura kurejesha miundombinu katika maeneo haya. Kulikuwa na uharibifu mkubwa daraja lilikatika pale Nderemi pamoja na bwawa kubwa ambalo lilisababisha pia kukatika kwa daraja hili, tumerejesha kwa kushirikiana na Jeshi na sasa panapitika na maeneo mengine pia tumeweza kutengeneza barabara ya kilometa 24 kuunganisha Mji wa Handeni pamoja na Mziha na sasa panapitika.
Pia tumeiunga barabara ya Handeni pamoja na Korogwe, niseme kwa ujumla tumejipanga kuimarisha maeneo yote yaliyoathirika na mvua na Bunge lako limetenga fedha kwa ajili ya kumudu dharura zinazojitokeza, tutaendelea kutumia fedha za dharura katika maeneo yote nchini ambapo tutakuwa tunapata uharibifu wa mvua, kurejesha miundombinu ili wananchi waendelee kupita wakati wote.
Name
Omari Mohamed Kigua
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilindi
Primary Question
MHE. OMARY A. KIGODA aliuliza:- Barabara ya Handeni – Mziha ni barabara ya mkakati na ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Je, ni lini Serikali itamalizia kipande kilichobaki kutoka Handeni mpaka Mziha?
Supplementary Question 2
MHE. OMARY M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Handeni- Kibirashi hadi Kiteto imekwisha na hatua zote za mwisho zimeshakamilika; na kwa kuwa barabara hii ni barabara ya kimkakati inaunganisha mikoa minne kwa maana ya Mkoa wa Tanga, Manyara, Singida na Dodoma. Je, Serikali sasa haioni umuhimu kuanza kutengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami ili kuondokana na kero hii ya mara kwa mara? Hivi ninavyosema muda huu barabara hii haipitiki kwa wiki sasa.
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kigua, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali inafahamu umuhimu wa barabara hii ndio maana usanifu wa kujenga barabara hii kilometa 461 kutoka Handeni kwenda hadi Singida umeshakamilika. Kwenye bajeti yetu tumetenga fedha kuanza ujenzi wa lami wa barabara hii kilometa 50, kwa hiyo Mheshimiwa Kigua naomba avute subira na kwamba tukipata fedha tutaanza ujenzi. Hata hivyo, kuna maeneo yalikuwa yameathirika na mvua kama nilivyojibu swali langu la msingi, ni kwamba tumejipanga kurejesha maeneo yote ambayo ni korofi na kama mvua zitaendelea kunyesha maeneo yoyote yatakayoonekana kuwa ni korofi tutakwenda maeneo hayo kufanya marejesho ya barabara.
Name
Frank George Mwakajoka
Sex
Male
Party
CHADEMA
Constituent
Tunduma
Primary Question
MHE. OMARY A. KIGODA aliuliza:- Barabara ya Handeni – Mziha ni barabara ya mkakati na ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Je, ni lini Serikali itamalizia kipande kilichobaki kutoka Handeni mpaka Mziha?
Supplementary Question 3
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni lini Serikali itajenga barabara ya baypass ya kutoka Mpemba kwenda Tunduma kwa sababu ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati anafanya kampeni zake kipindi cha mwaka 2015?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakajoka, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua umuhimu wa baypass na usanifu unafanyika, tutajenga mara moja tukipata fedha kwa ajili ya barabara hii.
Name
Shabani Omari Shekilindi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lushoto
Primary Question
MHE. OMARY A. KIGODA aliuliza:- Barabara ya Handeni – Mziha ni barabara ya mkakati na ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Je, ni lini Serikali itamalizia kipande kilichobaki kutoka Handeni mpaka Mziha?
Supplementary Question 4
MHE. SHABAN O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Barabara ya kuanzia Dochi- Nguli – Mombo ambayo ni kilometa 16 mara nyingi nishauliza swali hili lakini sipati majibu na sasa hivi hali ya barabara ile sio nzuri. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuhakikisha kwamba barabara ile inatoboka ili wananchi wangu waweze kupata huduma ya haraka?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mvua zilizonyesha hivi karibuni ziliathiri karibu maeneo yote ya Mkoa wa Tanga na sisi kama Serikali tumejipanga kurejesha maeneo hayo yaliyoharibiwa ikiwemo maeneo ya Dochi kwenda Mombo na eneo la kule Mchinga na maeneo mengine ya kule Pangani tumejipanga vizuri, wenzetu wa TANROADS wako kazini, Mheshimiwa Kilindi aondoe hofu tunafanya marejesho makubwa na kazi zinaendelea.