Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Anatropia Lwehikila Theonest
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. LUCIA M. MLOWE) aliuliza:- Njombe ni kati ya Mikoa mikubwa ya Kilimo na ina mashamba darasa ambapo wanafunzi wa maeneo mengine wanakuja kujifunza:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Chuo cha Kilimo katika Mkoa wa Njombe?
Supplementary Question 1
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Wazir, licha ya hayo majibu kwamba, vyuo vipo bado hawa wataalam wanaokuwa wanamaliza kwenye vyuo hawapewi ajira na ndio maana tunazidi kuona upungufu wa maafisa ugani kwenye maeneo yetu. Je, nini mkakati wa Serikali kuajiri maafisa ugani wa kutosha kwa ajili ya kusaidia kufundisha wakulima kuzalisha mbegu bora?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mkoa wa Kagera hususan Wilaya ya Kyerwa ni walimaji wakubwa wa zao la mgomba, kwa maana ya migomba. Nini mkakati wa Serikali kuja na viwanda au kuja na mbinu ya kuongeza thamani katika zao la ndizi kwa kuwa hilo zao au ndizi huwa zinaharibika muda mfupi baada ya kukomaa?
Name
Omary Tebweta Mgumba
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini Mashariki
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza anataka kujua mkakati wa Serikali kutoa ajira kwa maafisa ugani; kwanza niseme ni kweli maafisa ugani hawatoshelezi, lakini kwamba, tutaendelea kuajiri kutokana na vilevile kuzingatia kipato cha Serikali kwa sababu hata tukiwaajiri hawa wana stahiki zao lazima wapewe, badala yake tukija kuwaajiri bila kuwalipa tutaanzisha changamoto nyingine ambayo haiwezekani. Kwa hiyo, tutaendelea kuajiri kwa kuzingatia uwezo wa serikali kuwalipa na kutoa gharama nyingine. Lakini la katika kukabiliana na tatizo lililopo kama Serikali cha kwanza mkakati tuliokuwanao tunaendelea kujenga vituo vya rasilimali kilimo kila kata, ili maafisa ugani wachache hawa waliokuwepo waweze kuwakusanya wakulima na kutoa elimu ya kilimo cha kisasa kwa wakulima walio wengi kwenye kata zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwenye suala la Kagera kwenye suala la migomba; ni kweli migomba ni zao ambalo linapoteza thamani mapema. Mkakati wa Serikali kama tulivyosema siku zote Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi ni Serikali ya Viwanda, tutaendelea kuweka mazingira ya kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ili kuja kuwekeza katika viwanda kuongeza thamani. Na hii tutumieni kama fursa hata wabunge tuna uwezo hapa wa kwenda kuanzisha hivi viwanda vidogovidogo kuongeza thamani kwa sababu Serikali tulishajitoa kwenye suala la kufanya biashara tangu miaka ya 90.
Name
Aida Joseph Khenani
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Nkasi Kaskazini
Primary Question
MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. LUCIA M. MLOWE) aliuliza:- Njombe ni kati ya Mikoa mikubwa ya Kilimo na ina mashamba darasa ambapo wanafunzi wa maeneo mengine wanakuja kujifunza:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Chuo cha Kilimo katika Mkoa wa Njombe?
Supplementary Question 2
MHE. AIDA J. KHENAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na kuwa na vyuo vitatu Nyanda za Juu Kusini, lakini bado tunakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa fedha kwenye chuo cha utafiti. Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha za kutosha ili kuleta tija kwa ajili ya uzalishaji unaoendelea Nyanda za Juu Kusini?
Name
Omary Tebweta Mgumba
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini Mashariki
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, anataka kujua mkakati wa Serikali kupeleka fedha; kwenye bajeti ya mwaka huu tumetenga na tunapeleka fedha zaidi ya bilioni 10 kwenye vyuo vyetu vya utafiti na kilimo kwa ajili ya kwenda kuimarisha utafiti katika vyuo hivyo, ili viweze kuwahudumia wakulima.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved