Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Kwanza ilikuwa na mazao ya kimkakati ya biashara kama Kahawa, Pamba, 9 Pareto na Katani ili kuwa chachu ya kukuza Viwanda:- Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati gani mahsusi wa kuanzisha uzalishaji wa mazao na kaulimbiu ya Tanzania ya Viwanda?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa bahati Mheshimiwa Naibu Waziri ameanza kwa kusema kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ni mwendelezo wa Serikali zilizopita.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, zao la kahawa linaelekea kupotea kwa kasi kubwa sana na sababu kubwa inalolifanya zao hili hili lipotee ni mabadiliko ya tabianchi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya utafiti upya ili kuleta mbegu ambazo zitaendana na hali ya hewa ambayo ipo sasa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri amesema kwamba mazao haya yalikuwa ni mkakati kwa ajili ya malighafi za viwanda. Sasa nataka aniambie, tulikuwa na kiwanda cha VOIL pale Mwanza, Kiwanda cha Magunia Morogoro, Kiwanda cha Magunia Moshi, tulikuwa na Kiwanda cha Nyuzi Tabora. Hivi viwanda havipo ilhali wananchi wanaendelea kuzalisha: Je, hizi malighafi wananchi wanazozalisha, zinakwenda katika viwanda vipi?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. HUSSEIN M. BASHE): Mheshimiwa Spika, suala la mabadiliko ya tabianchi ni challenge ambayo inaikabili nchi yetu na dunia kwa ujumla. Wizara ya Kilimo kupita taasisi yake ya TARI sasa hivi tunafanya utafiti wa kuwa na mbegu sitakazokabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Hii imeonekana katika korosho ambapo tumepunguza muda wa mpaka zao la korosho kuja kuzalisha matokeo. Kwa hiyo, tunafanya hivyo hivyo katika mazao yote ya kimkakati na hata mazao ya chakula.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, utafiti huu unaendelea pamoja na soil profiling ili kuweza kujua kwamba eneo hili ambalo tunalima kahawa je, bado litaweza kuhimili zao la kahawa au ama tuweze kuwashauri wananchi jambo lingine? Sasa hivi Wizara kupitia taasisi yake ya TARI inaendelea na utafiti katika vyuo mbalimbali lakini wakati huo huo tunafanya suala la soil profiling.

Mheshimiwa Spika, pamoja na changamoto ya tabianchi, zao la kahawa linakabiliana na changamoto nyingi ikiwepo mfumo wa uzalishaji na mfumo wa uuzaji kupitia ushirika, Wizara inapitia mfumo mzima wa kuanzia uzalishaji mpaka uuzaji wa mazao yote ili kuweza kuleta tija kwa mkulima.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la viwanda ni ukweli usiofichika kwamba Taifa letu limepitia nyakati mbalimbali na viwanda vyetu vingi vimepitwa na teknolojia. Sasa hivi Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda na Biashara tunafanya mapping na ku-develop new strategy ili ku-attract investors ili waje kuwekeza katika Sekta ya Viwanda ili waweze ku-take off mazao ya wakulima.

Mheshimiwa Spika, Kiwanda cha Nyuzi Tabora na viwanda alivyovitaja Mheshimiwa Waziri vikiwemo viwanda vya pamba, sasa hivi vingi vimepitwa na teknolojia. Tunaposema tunafufua, sisi kama Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda tumekubaliana mkakati wetu siyo suala la kufufua tu ni ku-attract uwekezaji mpya utakaoendana na teknolojia ya sasa ili mazao ya kilimo yaweze kupata tija na kuweze kupata masoko ya uhakika. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Kwanza ilikuwa na mazao ya kimkakati ya biashara kama Kahawa, Pamba, 9 Pareto na Katani ili kuwa chachu ya kukuza Viwanda:- Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati gani mahsusi wa kuanzisha uzalishaji wa mazao na kaulimbiu ya Tanzania ya Viwanda?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Zao la kahawa ni miongoni mwa mazao ya kimkakati, lakini zao hili bei yake imekuwa ikisuasua kila mwaka; na ukilinganisha uzalishaji wa zao hili kwa mkulima gharama zinakuwa kubwa:-

Nini mkakati wa Serikali ili kuweza kuongeza bei ya kahawa ili mkulima aweze kuendeleza zao hili? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. HUSSEIN M. BASHE): Mheshimiwa Spika, kwanza mkakati wa Serikali ni kutambua gharama halisi za uzalishaji za wakulima. Wizara ya Kilimo chini ya Naibu Katibu wa Mkuu Prof. Tumbo, sasa hivi tumeanza program ya kuanza kufanya evaluation ya mazao yote kujua mkulima anatumia shilingi ngapi.

Mheshimia Spika, kuhusu zao la kahawa, kama nilivyosema wakati namjibu Mheshimiwa Shangazi, ni kweli linakumbana na changamoto nyingi. Changamoto ya bei ya ni matokeo ya mfumo ambao umekuwepo muda mrefu ambao umemnyonya mkulima. Sasa hivi tunatumia Benki ya TADB ambayo imeanza kuzipa fedha taasisi za ushirika zilizopo katika Mkoa wa Kagera ili waanze kuchukua mazao ya wakulima kwa bei maalum na wakati huo huo tukitafuta masoko ya uhakika.

Mheshimiwa Spika, nawaomba Waheshimiwa Wabunge watupe muda kama Wizara, mazao yote haya tutayabadilisha mfumo wake na kuruhusu sekta binafsi iwe competitive wakati huo huo tukipunguza gharama za uzalishaji kama Serikali ili mkulima awezi kupata faida.