Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata za Sindano, Lupaso, Lipumburu, Mchauru na Mapili (Chikolopola) ambazo zipo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru majibu mazuri ya Naibu Waziri lakini nina maswali ya kumuuliza Mheshimiwa Waziri.

Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Mapili na Namyomyo, Chikolopola, Lupaso pamoja na maeneo ya Lipumburu wamekuwa wakipata shida ya mawasiliano kwa muda mrefu sana. Ahadi ya Serikali ni kwamba kipaumbele cha kwanza ni kuhakikisha minara inajengwa hasa maeneo ya kandokando mwa vijiji vilivyomo mipakani mwa nchi yetu na nchi jirani. Kwa kuwa kuna tatizo kubwa sana la ucheleweshaji wa kupatikana vibali vya ujenzi iliyopelekea hata kwenye jibu la msingi, kwamba mradi mmoja unasainiwa mwezi Desemba, 2018 lakini unakuja kumalizika kutekelezwa Desemba, 2019.

Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha inaondoa tatizo la urasimu wa upatikanaji wa vibali ili minara ijengwe kwa haraka? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri aliwahi kuahidi kwamba katika Bunge lililopita kwamba atatembelea vijiji hivi vilivyopo mpakani mwa Tanzania, Msumbiji ili kuzungumza na wananchi. Je, yupo tayari sasa baada ya Bunge hili kutembelea vijiji hivyo pamoja na Kijiji cha Lupaso ambacho Kiongozi Mkuu wa nchi mstaafu ndiyo nyumbani kwake? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nishukuru Bunge lako tukufu ambalo lilitunga Sheria ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Mfuko huu utahakikisha kwamba sasa nchi nzima inakuwa na mawasiliano. Ijumaa nilikuwa na mkutano na watoa huduma wote wa mawasiliano tukizungumzia miradi ya kata 521. Tumekubaliana baada ya wiki mbili tunakutana, kwa hiyo, hayo majibu ya msingi yaliyotolewa Mheshimiwa Bwanausi, vijiji vyote hivyo vyote vitapata mawasiliano na hiyo ndiyo ahadi ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili la vibali, suala la vibali sasa hivi halina mgogoro tena, NEMC wamejiandaa vizuri tukiomba vibali tunavipata haraka. Ufumbuzi wa kutoka vibali haraka ulitokana na mradi wa makaa ya mawe pale Mtwara, Mheshimiwa Rais alielekeza kwamba sasa vibali vinatakiwa vitoke haraka na sasa vibali vinatoka haraka hakuna kikwazo tena cha kutoka vibali. (Makofi)