Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD Aliuliza:- Serikali iliahidi kuleta mradi wa maji katika Jimbo la Morogoro Mjini ambao utamaliza kero ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kihonda, Tungi, Lukombe na Mkundi katika Kata ya Mindu. (a) Je, ni lini mradi huo utaanza? (b) Je, mradi huo unategemewa kugharimu kiasi gani?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza nilitaka kujua mradi wa maji wa Kihonda na Mkundi ambao unaunganisha Mitaa ya Yespa, Kilimanjaro umeshaanza; tunataka kujua ni lini utakamika kwa sababu umechukua muda mrefu mpaka sasa haujakamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Mradi wa Maji wa AFD ambao utagharimu Euro milioni 70 Morogoro kama unavyojua kuna kero kubwa za maji; sasa nilitaka kujua ni lini utasainiwa ili uanze kazi uwakombe wananchi wa Morogoro Mjini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji nimpongeze Mheshimiwa Abood ni miongoni mwa Wabunge ambao wachapakazi na amekuwa ni mfuatiliaji mkubwa sana hususan changamoto zinazohusina na wananchi wake, lakini kubwa ambacho ninachotaka kusema pamoja na changamoto zipo jitihada ambazo sisi kama Serikali tunazozifanya katika Mkoa ule kwa maana ya Morogoro Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mradi wa Kilimanyari Yespa mradi takribani milioni 715 ambazo tunatekeleza nimwagize Meneja kwa maana Mkurugenzi wa MORUWASA kuhakikisha mradi ule unakamilika kwa mujibu wa mkataba ili wananchi wale waweze kupata huduma ya maji. Na mimi nataka nimhakikishie Mheshimiwa Abood baada ya Bunge nitafika eneo lile kujionea utekelezaji wa mradi ule. Lakini kikubwa kuhusu la huu mradi huu mkubwa kwa maana kuondoa tatizo la maji Morogoro wa Euro milioni 70 ninachotaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge ukiona giza linatanda ujue kuna kucha.

Mheshimiwa Abood jana sisi tumefungua tender document kwa maana ya kuwapata wataalam wa ushauri ili kuhakikisha mradi ule unaweza kuanza na wananchi wako wanapata maji. Ahsante sana.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD Aliuliza:- Serikali iliahidi kuleta mradi wa maji katika Jimbo la Morogoro Mjini ambao utamaliza kero ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kihonda, Tungi, Lukombe na Mkundi katika Kata ya Mindu. (a) Je, ni lini mradi huo utaanza? (b) Je, mradi huo unategemewa kugharimu kiasi gani?

Supplementary Question 2

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti ninakushukuru, ninaomba niulize swali dogo moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipo kwenye hatari kubwa la kupoteza fedha takribani shilingi bilioni moja na milioni 600 kutokana na mkandarasi wa Mradi wa Mbuta kuvunja mkataba, lakini vilevile mkandarasi wa Mwakijembe kuamua kusimama kufanya kazi kwa sababu ya uchelewashaji wa fedha.

Ni lini Serikali itachukua hatua za haraka kuhakikisha inaokoa fedha hizi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kaka yangu Dastan Kitandula kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika jimbo lake pale Mkinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti sisi kama Wizara ya Maji tulishasema kwamba hatukuwa na kisingizio chochote, kwamba sasa hivi mmetupa rungu kwa maana uazishwaji wa RUWASA kwa maana Wakala wa Maji Vijijini na tumejipanga vizuri kwa maana agizo la Mheshimiwa Waziri kwa maana baadhi ya miradi ya tutaifanya kwa kutumia wataalamu wetu wa ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kumhakikishi katika Mkandarasi yule aliyeondoka site hatuna nafasi tena ya kubembelezana ile kazi tutaifanya kupitia wakala wetu wa maji kwa maana ya Uchimbaji wa Maji Visima (DDCA) nawaagiza waende kuifanya kazi ile mara moja ili wananchi waweze kupata maji. Lakini kuhusu mkandarasi ambaye ametekeleza mradi hajalipwa certificate, nataka nimhakikishie ndani ya mwezi huu wa tisa tutamuweka katika orodha ili kuhakikisha kwamba tunamlipa ili wananchi waendelee kutekelezewa mradi wa maji, ahsante sana.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD Aliuliza:- Serikali iliahidi kuleta mradi wa maji katika Jimbo la Morogoro Mjini ambao utamaliza kero ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kihonda, Tungi, Lukombe na Mkundi katika Kata ya Mindu. (a) Je, ni lini mradi huo utaanza? (b) Je, mradi huo unategemewa kugharimu kiasi gani?

Supplementary Question 3

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana katika Manispaa ya Mtwara Mikindani yaani Jimbo la Mtwara Mjini kumekuwa na tatizo kubwa la maji kutoka yenye tope jingi kwa muda mrefu na maji hayo yanapita katika mita za wananchi kuwasababishia kulipa bili wakati maji wanayoyapata ni machafu. Pamoja na mambo mengine chanzo kikubwa ni kukosekana kwa chujio katika chanzo cha maji cha Mtawanya.

Swali langu, ni lini Serikali itanunua chujio kubwa la uhakika kwa ajili ya kuchuja maji katika chanzo cha Mtawanya ili kusudi wananchi wanaoishi Mtwara Mikindani wapate maji safi na salama? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji niseme kwa ufupi sana ni wajibu na ni haki ya mwananchi kupatiwa maji, si maji tu kwa maana yamaji safi na salama na yenye ubora. Nimefika Mtwara lakini moja ya changamoto kubwa pale ni chujio na nitumie nafasi hii kumwagiza Katibu Mkuu wa Wizara yetu ya Maji kuhakikisha mchakato ule unakamika haraka kwa ajili ya ujenzi wa chujio na wananchi wa Mtwara waweze kupata maji safi salama na yenye ubora. Ahsante sana.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD Aliuliza:- Serikali iliahidi kuleta mradi wa maji katika Jimbo la Morogoro Mjini ambao utamaliza kero ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kihonda, Tungi, Lukombe na Mkundi katika Kata ya Mindu. (a) Je, ni lini mradi huo utaanza? (b) Je, mradi huo unategemewa kugharimu kiasi gani?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kupatikana Mkandarasi wa Mradi wa Lwakajunju katika Jimbo la Karagwe lakini bado wananchi wa Karagwe hawajajua ni lini mkandarasi huyo atakwenda kuanza. Je, ni lini utekelezaji wa Mkandarasi wa maji wa Lwakajunju utaanza ili kuwatua ndoo wakina mama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa jasiri, mpambanaji kwa wanawake wenzake kwa Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ninachotaka kusema sisi kama Wizara ya Maji na kupitia Mheshimiwa Rais tunamshukuru sana tumepata fedha zaidi ya dola milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa miradi katika miji 28 lakini tunashukuru jitihada kubwa ambazo zimefanyw ana Waziri wetu kwa maana ya Mheshimiwa Mbarawa kuhakikisha Mhandisi Mshauri amepatikana kwa haraka na ameshapita katika miji yote sasa hivi tunakamilisha document kwa maana ya kupata kibali ili kumpata mkandarasi na ujenzi wa mradi ule uweze kuanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na kaka yangu Bashungwa siis Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo katika kuhakikisha mkandarasi anapatikana kwa wakati na utekelezaji wa mradi wa maji kwa maana ya kumtua mwanamama ndoo kichwani unaanza mara moja. Ahsante sana.

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD Aliuliza:- Serikali iliahidi kuleta mradi wa maji katika Jimbo la Morogoro Mjini ambao utamaliza kero ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kihonda, Tungi, Lukombe na Mkundi katika Kata ya Mindu. (a) Je, ni lini mradi huo utaanza? (b) Je, mradi huo unategemewa kugharimu kiasi gani?

Supplementary Question 5

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Waziri ulitembelea Jimbo la Mbagala kwenye mradi wa Mgembaki pamoja na Kiwika na ulitoa maagizo kwa sababu miradi hiyo inaendeshwa kiufanisi, wananchi ambao walichangia miradi ile pamoja na Wizara pamoja na watu wa DAWASA wakae pamoja ili waangalie jinsi ya kuiendesha kwa ufanisi, lakini cha ajabu watu wa DAWASA wameingia kule na wanataka kuchukua vyanzo vile bila kushirikisha Kamati zile za wananchi na kuacha kabisa maagizo uliyoyatoa.

Je, utakuwa tayari sasa turudi tena kwa wananchi wale na DAWASA ili tuweze kuangalia jinsi gani ya kuendesha miradi ile kwa maridhiano?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, Mheshimiwa Mbunge unafanyakazi kubwa na sisi kama Wizara ya Maji hatuwezi kuwa kikwazo, nipo tayari kuongozana na wewe. Ahsante sana.

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD Aliuliza:- Serikali iliahidi kuleta mradi wa maji katika Jimbo la Morogoro Mjini ambao utamaliza kero ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kihonda, Tungi, Lukombe na Mkundi katika Kata ya Mindu. (a) Je, ni lini mradi huo utaanza? (b) Je, mradi huo unategemewa kugharimu kiasi gani?

Supplementary Question 6

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Waziri moja ya ziara ambazo umezifanya Jimbo la Nachingwea ni katika Kata ya Mbondo, Kijiji cha Chimbendenga. Sasa hivi ni takribani miezi minane toka uondoke ule mradi mpaka sasa hivi haujakamilika. Naomba kufahamu commitment ya Wizara juu ya kukamilisha mradi wa maji Chimbendenga?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kiukweli nimefika Nachingwea nimejionea kazi kubwa ambazo anazozifanya siyo katika maji tu hata katika maeneo mengine, lakini kikubwa ambacho ninachotaka kusema moja ya changamoto kubwa sana katika sekta yetu ya maji kulikuwa na wakandarasi wengi wababaishaji lakini hata hao wanaotekeleza wamekuwa katika kusuasua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi hatuna nafasi kama Wizara ya Maji kubembeleza watu. Tunawaomba Wakandarasi wafanyekezi kwa wakati na sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo katika kuwalipa fedha zao katika kuhakikisha wanakamilisha miradi ya maji. Ninachotaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, tutafanya mawasiliano na wenzetu wa Nachingwea, tukiona mkandarasi anafanyakazi kwa kusuasua tutamnyang’anya kazi tutaifanya kwa wataalam wetu wa ndani ili mradi wetu uweze kukamilika na wananchi wetu waweze kupata huduma ya maji. Ahsante sana.