Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA Aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano imekaribisha wawekezaji wa nje na ndani kuwekeza sehemu mbalimbali hapa nchini:- Je, Serikali ipo tayari sasa kuelekeza wawekezaji hao kuwekeza katika Mkoa wa Tabora?

Supplementary Question 1

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mafupi ya nyongeza. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri ambayo inafanywa kwa ajili ya mambo ya uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba kwa kuwa alipokuwepo Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, alikuwa ameandaa na alishawatayarisha wawekezaji kutoka nchini China ambao walikuwa tayari kuwekeza katika Kiwanda cha Tumbaku, kwa bahati mbaya waliishia Dar es Salaam na kulikuwa na matatizo ya Uhamiaji: Je, Waziri yuko tayari sasa kuwafuatilia hawa wawekezaji wa Kichina ambao walikuwa tayari kabisa na maeneo yalitengwa ili waweze kuja kuwekeza kwenye zao la tumbaku?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili: kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, amefanya jitihada kubwa na Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kwa kuboresha maeneo katika mkoa mzima na Wilaya zote: Sasa je, Waziri yupo tayari sasa kuwaleta wataalamu rasmi ili kuweza kuainisha hayo maeneo?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (UWEKEZAJI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niseme tunashukuru kwa pongezi na nikuhakikishie tutaendelea kufanya kazi nawe pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine pamoja na mikoa yetu katika kuhakikisha kwamba tunachochea na kuvutia uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kweli nimefahamishwa kwamba alikuwepo mwekezaji kutoka China ambaye alikuwa na nia ya kuwekeza Kiwanda cha Tumbaku Tabora. Mpaka sasa tumeendelea kumfuatilia, lakini bado hajaonyesha nia.

Napenda kusema kwamba tutaendelea kumhamasisha yeye zaidi na kutafuta wawekezaji wengine zaidi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Viwanda pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili katika swali lake la pili kuhusiana kuleta wataalam, kwanza napenda kuwapongeza Mkoa wa Tabora kwa kutenga ardhi hiyo ya zaidi ya ekari 42, lakini kipekee napenda kusema tu kwamba ni takribani asilimia tano ndiyo tayari inakidhi vigezo. Imewekwa ardhi kubwa, mfano ukiangalia Kaliuwa, wana zaidi ya ekari 37,201, lakini ni asilimia tano tu ya Mkoa mzima wa Tabora katika maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa, ndiyo ambayo tayari yalimewekewa miundombinu wezeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutaendelea kushirikiana na Wizara ya Fedha, Wizara ya Ujenzi pamoja na Mkoa husika wa Tabora kwanza kuhakikisha kwamba maeneo hayo yanawekewa miundombinu wezeshi lakini pia kuhakikisha Halmashauri nazo zinaendelea kutenga fedha ili miundombinu iweze kutengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapongeza sana kipekee Halmashauri ya Nzega ambao tayari kwenye bajeti yao wameweka zaidi ya shilingi milioni 40 kwa ajili ya suala zima ya upimaji. Kwa hiyo, natoa rai kwa Halmashauri nyingine saba zilizobakia na nyingine nchini, basi wajitahidi kutenga fedha katika bajeti yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala zima la kuleta wataalam, nimhakikishie kwamba tuko tayari kuleta wataalamu, lakini zaidi niwapongeze Halmashauri zile nane, kila moja imekuja na mradi wake wa kimkakati; wako ambao wana mradi wa machinjio, wako ambao wana mradi wa mashamba ya mifugo, kuweka kiwanda cha usindikaji na utengenezaji wa vyakula vya mifugo pamoja na sehemu nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza mikoa yote na Halmashauri zote ambazo tayari wameweza kubuni miradi ya mikakati. Nawaomba waendelee kufuatilia, washirikiane na Wizara ya Kilimo pamoja na Benki yatu ya Kilimo na benki nyingine za kimaendeleo ili kuweza kupata mitaji ya kuweza kuwekeza. Nakushukuru.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA Aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano imekaribisha wawekezaji wa nje na ndani kuwekeza sehemu mbalimbali hapa nchini:- Je, Serikali ipo tayari sasa kuelekeza wawekezaji hao kuwekeza katika Mkoa wa Tabora?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Napenda tu kuuliza Serikali, tuna mradi mkubwa wa uchimbaji wa madini ya niobium katika milima ya Panda Hill Songwe; na kwa bahati nzuri ile miradi ita-attract direct investment ya karibu dola milioni 200 na wawekezaji wapo tayari; na katika ziara ya Mheshimiwa Rais alipofanya ziara kule Mbeya…

MWENYEKITI: Swali, swali!

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu: Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuwaruhusu hao wawekezaji waanze kuchimba haya madini ya niobium ili vile vile wajenge na kiwanda cha kuchakata hayo madini ambacho ni cha kwanza Afrika na cha nne duniani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (UWEKEZAJI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kusema kwamba tunatambua kuhusiana na mradi huu wa Niobium ambao utafanyika katika milima ya Panda Hill na bahati nzuri nami nilipata bahati ya kukaa katika Wizara ya Madini, niliweza kuwaona wawekezaji hawa; na ni madini ambayo kwa kweli ni ya muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tulishaanza kuwashughulikia, pia tumekuwa na mashauriano na Wizara ya Madini pamoja na Wizara ya Viwanda kupitia EPZ. Tutakutana pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Madini pamoja na Wizara ya Viwanda ili kuweza kuona ni kwa namna gani tunakwamua mradi huu muhimu.