Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mlowo – Kamsamba – Kiliyamatundu – Kibaoni itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, wakati wa kampeni Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli aliahidi kwamba kabla ya kufika mwaka 2020, barabara hiyo ya kutoka Mlowo kwenda Kamsamba hadi Kibaoni itakuwa imekamilika. Ukiangalia kuanzia sasa hadi mwaka 2020 bado miezi michache tu. Je, ni lini sasa ahadi hii ya Serikali itatekezwa kwa vitendo badala ya maneno?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa katika majibu ya Serikali kwamba kukamilisha usanifu wa kina hawajataja kwamba ni lini usanifu wa kina utakamilishwa. Je, Serikali kutotaja muda wa kukamilisha usanifu wa kina haioni huku ni kutowatendea haki wananchi wa Mikoa ya Songwe, Katavi, pamoja na Rukwa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Haonga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, umetaja ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni, lakini ujenzi wa barabara ni mchakato, lazima ufanye upembuzi yakinifu, usanifu wa kina, baadaye uingie mikataba uanze kujenga. Hauwezi ukafanya kabla ya kukamilisha hizo hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vipande vya barabara ambavyo unavizungumzia tayari kuna kimoja mwezi huu wa tisa cha kutoka Mlowo kwenda mpaka pale tulipokamilisha daraja, mwezi wa tisa usanifu wa kina utakamilika baada ya hapo mambo mengine yanaanza. Upembuzi yakinifu umeanzia kule Muze unakuja kuunga Kamsamba, na tuna matarajio ya kuendelea huko na pia tumeshaanzia Inyonga kuja mpaka Maji ya Moto. Kwa hiyo, utaratibu unaendelea ahadi ya Mheshimiwa Rais inatekelezwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge usiwe na wasiwasi na wananchi jirani zangu wa kule wawe na uhakika kwamba barabara ile itajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mlowo – Kamsamba – Kiliyamatundu – Kibaoni itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naomba kuuliza swali langu la nyongeza:-

Barabara ya kutoka Senga Ibisabageni mpaka Sima ni barabara inayotuunganisha Mkoa wa Geita na Mkoa wa Mwanza na Serikali ilitupa fedha upande wa Geita na upande wa Mwanza. Upande wa Geita tulishalima eneo letu tukamaliza lakini upande wa Mwanza umebakiza kama kilomita tatu na leo ni mara ya tatu namuuliza Mheshimiwa Waziri.

Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kufuatana na mimi kwenda kuona zile kilomita tatu tu ambazo upande wa Mwanza wameshindwa kumaliza ili watu waanze kupitisha magari yao pale? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niko tayari kufuatana naye. (Makofi)

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mlowo – Kamsamba – Kiliyamatundu – Kibaoni itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba niulize swali la nyongeza, kwa kuwa barabara ya Kenyatta itokaya Mwanza Mjini kwenda Usagala kuelekea Shinyanga ni barabara ambayo inahudumia watu wengi na kwa sasa inaendelea kuwa finyu sana. Ni lini Serikali kupitia mipango yake ya uboreshaji miundombinu itaitolea fedha barabara hii walau iwe ya njia tatu mpaka nne ili kuweza kukidhi mahitaji makubwa ya watu wa Mwanza?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kupanua barabara, kuongeza reli, hatuendi hivi hivi lakini mpaka traffic iweze kufikia kwamba sasa yanapita magari 20,000 au 40,000 kwa siku ndiyo tunaipanua ili kuiongezea uwezo. Kwa hiyo, itakapofikia itafanyika.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mlowo – Kamsamba – Kiliyamatundu – Kibaoni itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kama ilivyo katika Wilaya ya Momba, kule Moshi Vijijini katika Kata ya Uru Shimbwe Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli wakati anagombea alikuja pale akahutubia na akaahidi kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mamboleo mpaka Shimbwe. Kwa kweli ile barabara sasa hivi iko katika hali mbaya sana, sasa naomba kujua toka kwa Serikali ni lini ahadi hii ya Mheshimiwa Rais itatimizwa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Komu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni kuunganisha mikoa kwa barabara za lami, lakini na mipaka ya majirani zetu kuunganisha kwa lami halafu baadaye ndiyo tunaendelea na barabara nyingine.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mlowo – Kamsamba – Kiliyamatundu – Kibaoni itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kuelekea Ruaha National Park ambayo ni Jimbo la Kalenga imekuwa ni changamoto na ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne na Rais wa Awamu ya Tano. Ni lini sasa barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ile itajengwa pamoja na Uwanja wa Ndege wa Nduli na itajengwa kupitia fedha za Benki ya Dunia, taratibu za kupata hizo fedha zinaendelea itakapokamilika mradi utaanza.