Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Tangu uhuru Wilaya ya Mbinga imekuwa ikitegemea zao moja la biashara ambalo ni kahawa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka zao lingine la biashara Wilayani humo?

Supplementary Question 1

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Niipongeze Serikali kwa majibu mazuri katika swali hilo. Pia kwa dhati kabisa nichukue fursa hii kuishukuru Serikali kwa kupeleka Mnada wa Kahawa Wilayani Mbinga kuanzia msimu huu wa mwaka 2019. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa na maswali madogo mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni kweli Serikali imepeleka zao la korosho katika Kata za Rwanda na Litumbandyosi. Changamoto ya wakulima hao ni upatikanaji wa miche bora na kwa bei nafuu. Je, Serikali iko tayari kuendelea kutoa miche ya mikorosho bora kwa bei nafuu au bure kwa wananchi wa Kata ya Rwanda na Litumbandyosi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika jibu la msingi, Serikali imekiri kuwa ilitoa mafunzo ya uzalishaji wa miche bora ya mikorosho katika vikundi sita vya Jembe Halimtupi Mtu, Chapakazi, Twiga, Juhudi, Kiboko na Korosho ni Mali lakini vikundi hivi bado vinaidai Bodi ya Korosho. Je, ni lini madeni ya vikundi hivyo yatalipwa?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tupo tayari kupeleka miche ya mikorosho kwa bei nafuu kwa wakulima wa Wilaya ya Mbinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kama tunavyofahamu deni likivuka mwaka madeni yote haya ya Serikali yanahamia Hazina. Sasa hivi Serikali tuko kwenye hatua za mwisho za kumalizia uhakiki na vikundi vyote ambavyo uhakiki umemalizika vimeshaanza kulipwa na hivi alivyovitaja vitaanza kulipwa baada ya uhakiki kukamilika.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Tangu uhuru Wilaya ya Mbinga imekuwa ikitegemea zao moja la biashara ambalo ni kahawa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka zao lingine la biashara Wilayani humo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Serikali imeamua zao la mchikichi lilimwe Kigoma na liweze kuwa zao la biashara na Waziri Mkuu kwa kuweka msisitizo ameenda Kigoma mara tatu kufuatilia zao hili la mchikichi; na kwa kuwa wananchi wameamua kuitikia mwito huo wa kulima zao hilo…

MWENYEKITI: Swali.

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha wananchi wanapata mbegu na kuanza kulima zao hilo?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Genzabuke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tuko tayari kwa ajili ya uzalishaji wa miche ya michikichi na kuigawa kwa wakulima. Sasa hivi tumeshatenga zaidi ya shilingi bilioni 5 kwa ajili ya kuanza uzalishaji mwaka huu na mwaka huu mwezi Septemba, miche zaidi ya milioni moja itakwenda sokoni. Tumeshaingia mkataba na sekta binafsi kuzalisha miche milioni tano kwa msimu huu unaokuja na ndani ya miaka mitatu tunategemea kuzalisha miche zaidi ya milioni 20 na kuigawa Tanzania nzima.