Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Ilani ya CCM iliahidi kutengeneza barabara ya kutoka Njombe - Lupembe - Madeke - Morogoro - kwa lami katika mwaka 2015/2016:- Je, ni lini barabara hiyo itaanza kutengenezwa hasa ikizingatiwa kuwa imebaki miezi mitano katika mwaka wa fedha 2015/2016?

Supplementary Question 1

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, naomba Mheshimiwa Waziri aweze kunithibitishia juu ya kuanza ujenzi huo kwa mwaka 2016/2017, kwa kuwa kwenye vitabu vya bajeti sijaona bajeti iliyotengwa au fedha iliyotengwa kwa ajili ya barabara hiyo.
Swali la pili, barabara ya Lupembe kwa sasa hivi imefungwa, magari yote yanayoanzia tani kumi na kuendelea hayaruhusiwi kuingia, wakati wananchi wa Lupembe, hasa kata nane, wanategemea barabara hii kusafirisha mbao, wanategemea barabara hii kusafirisha nguzo na vifaa vya ujenzi kama mchanga na tofali, sasa hivi imefungwa hawawezi kusafirisha, hivyo kuathiri uchumi wa wananchi hawa. Naomba Serikali iniambie, ni utaratibu gani ambao itauweka kwa sasa hivi ambapo tunasubiri ujenzi wa barabara hii ili wananchi wasiendelee kuathirika kwa uchumi wao?
Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwa swali lake dogo la kwanza, naomba asubiri hotuba ya Waziri wangu wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ili apate tafsiri sahihi ya randama ambayo ameiangalia. Namhakikishia ujenzi huo unaanza mwaka 2016/2017 kama tulivyoeleza katika jibu la swali la msingi.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kuharibika na kukatika kwa barabara hiyo, naomba nichukue fursa hii kuwakumbusha tena TANROADS mikoani wote pamoja na Chief wao, kuhakikisha kwamba barabara zote ambazo zimekatika kutokana na mvua kubwa iliyopita zinafunguliwa, wasimamie suala hilo ili wananchi waendelee kupata huduma ya usafiri na maisha yaendelee kama kawaida.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Ilani ya CCM iliahidi kutengeneza barabara ya kutoka Njombe - Lupembe - Madeke - Morogoro - kwa lami katika mwaka 2015/2016:- Je, ni lini barabara hiyo itaanza kutengenezwa hasa ikizingatiwa kuwa imebaki miezi mitano katika mwaka wa fedha 2015/2016?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa, Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga barabara ya lami kilometa 1.5 katika Mji wa Mombo na Rais wa Awamu ya Tano ameahidi vilevile kujenga barabara hiyo kilometa moja, lakini cha kushangaza mpaka leo hii hela hazijaingia katika Mfuko wa Mkoa. Je, ile barabara ambayo imeahidiwa na Marais wawili itajengwa lini kwa kiwango cha lami kule Mombo?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia kwamba ahadi za viongozi wetu, Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne na Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano, tuliopewa dhamana tutaitekeleza.