Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Mwaka 1995 Serikali ilifanya uthamini wa wananchi wa Kata ya Kipawa ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege Dar es Salaam ambapo baadhi ya wananchi hao walilipwa fidia lakini kuna baadhi ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fidia hiyo na hawajui ni lini watalipwa:- Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi hao ambao hawajalipwa ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nilitaka nimuambie Mheshimiwa Naibu Waziri wa Miundombinu kwamba sasa hivi wakazi wanaodai fidia siyo 800 ni wakazi 1,600. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu yake mazuri aliyonipa, lakini nilitaka niongeze maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tathmini iliyofanyika ilifanyika 1995 na wakati huo mfuko wa cement au vitu vyote ambavyo vinavyohusisha ujenzi vilikuwa viko bei ya chini, je, Serikali ina mpango gani wa kuwafanyia tathmini tena hawa wakazi 1,600 ili waweze kupata fidia yao kutokana na bei za vifaa vya ujenzi kupanda?
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nalotaka kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba commitment ya Serikali, iseme itawalipa lini hawa wakazi wa Kipunguni, ambao wamebaki 1,600, kwa sababu mpaka sasa hivi Serikali haijasema itawalipa lini?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILINO: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu concern ya Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kipunguni 742 ambao bado hawajalipwa fidia. Kwanza, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba itabidi tuwasiliane ili tuwe na takwimu sahihi. Kwa mujibu wa takwimu zetu waliobakia ni 742 na sio 1,600 aliowataja. Hata hivyo, kwa sababu yeye anafahamu ni 1,600 tutalisawazisha hilo. Naomba atuletee orodha ili tuweze kuangalia hatimaye tuone kuna tatizo gani katika hizo takwimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuwalipa hao 742 waliobakia, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi, Serikali itawalipa kama ilivyodhamiria. Kuhusu kwamba wafanyiwe tathmini upya, nadhani Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba hakuna sababu ya kufanya tathmini upya kwa sababu tathmini ile iliyofanyika na kwa kipindi ambacho kinachelewa tuna utaratibu wa kuhuisha viwango kwa maana ya kuongeza riba inayotakiwa kuongezeka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba suala la tathmini upya wala siyo la msingi sana. La msingi ni sisi kupata fedha na kuwalipa hawa waliobakia 742 na tutalifanya hilo mara tutakapopata fedha.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Mwaka 1995 Serikali ilifanya uthamini wa wananchi wa Kata ya Kipawa ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege Dar es Salaam ambapo baadhi ya wananchi hao walilipwa fidia lakini kuna baadhi ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fidia hiyo na hawajui ni lini watalipwa:- Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi hao ambao hawajalipwa ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wangu wa Shabiby round about, Arusha Road walifanyiwa tathmini mwaka 2006 na waliambiwa wakati wowote Serikali itabomoa nyumba zao na kujenga barabara pale lakini mpaka leo wananchi hawa hawajalipwa na huu ni mwaka wa 10 hata choo kikibomoka hawajengi. Naomba Waziri aniambie, ni lini wale watu watalipwa fidia zao halali kwa maana zinazostahili kwa leo ili waondoke?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILANO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba umenizuia kusema yale yaliyopo ndani ya roho yangu lakini naomba uniruhusu, unafahamu fika Mheshimiwa Felister Bura…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, ni kwa sababu muda wetu ni mfupi ndiyo maana nimekusaidia kuwatangazia wote kwamba sifa zile zinamwendea kila Mbunge hapa ndani ili wewe uendelee tu kujibu maswali. (Kicheko/Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa juhudi za Mheshimiwa Felister Bura, hivi sasa tunaendelea kukamilisha kilomita nane za lami eneo la Msalato na kwa juhudi zake hizo hizo namhakikishia tutaendelea kuhakikisha tunawalipa fidia hawa watu ambao wanahusika katika hilo eneo. Kama ambavyo nilijibu awali, hakuna sababu ya kufanya tathmini upya badala yake ile formula ya kuongeza riba ndiyo inayotumika na hawa watu watalipwa haki yao bila matatizo yoyote mara fedha zitakapopatikana.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Mwaka 1995 Serikali ilifanya uthamini wa wananchi wa Kata ya Kipawa ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege Dar es Salaam ambapo baadhi ya wananchi hao walilipwa fidia lakini kuna baadhi ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fidia hiyo na hawajui ni lini watalipwa:- Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi hao ambao hawajalipwa ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja?

Supplementary Question 3

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa suala hili la Kipunguni Dar es Salaam kutokana na jibu la msingi limekuwa likileta malalamiko mengi na limekuwa likizungumzwa kwa muda mrefu na kwa kuwa ofisi ya Wizara hii ipo Dar es Salaam:-
Je, kwa nini Serikali hasa Mheshimiwa Naibu Waziri asitoke yeye aende Kipunguni pamoja na wataalam ili aweze kupata majibu ya kujiridhisha badala ya kumsubiri Mheshimiwa Mbunge yeye ndiyo alete majibu hapa Bungeni.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hawa wa Kipunguni walishafika ofisini kwetu, nikaondoka nao nikaenda kwa acting CEO wa Uwanja ule wa Ndege na baada ya kujadiliana kwa mpana ndiyo hayo majibu ninayoyatoa hapa yanatokana na vikao hivyo. Mimi mwenyewe nimekutana nao ofisini baada ya wao kuja na baadaye tulifanyia vikao Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam tukiangalia maeneo yote yale matatu ya Kipunguni, Kipawa na Kigilagila. Kwa hiyo, namhakikishia kwamba hicho nachokisema hapa ni kutokana na kile nilichokifanyia kazi. Ndiyo maana nasema huu utofauti kati yangu na Mheshimiwa Mbunge wa figure alizoleta hapa ningependa nipate ushahidi wa hicho anachokiongea.
Mheshimiwa Naibu Spika, nachokisema, waliobakia ni 742 na tutawalipa mara fedha zitakapopatikana, ni kutokana na kazi kubwa niliyoifanya katika eneo hilo. Hata hivyo, bado nitaendelea kuliangalia suala hilo nikishirikiana na hawa Waheshimiwa Wabunge ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Kaluwa kuhakikisha kwamba hicho tunachokisema ndicho sahihi.

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Mwaka 1995 Serikali ilifanya uthamini wa wananchi wa Kata ya Kipawa ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege Dar es Salaam ambapo baadhi ya wananchi hao walilipwa fidia lakini kuna baadhi ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fidia hiyo na hawajui ni lini watalipwa:- Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi hao ambao hawajalipwa ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja?

Supplementary Question 4

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Jambo lililotokea Segerea linafanana sana na lile linalotokea barabara ya Bwanga Ruzewe ambapo wananchi walivunjiwa nyumba kupisha ujenzi wa barabara hiyo miaka minne sasa na waliahidiwa kwamba watalipwa fidia na wameambiwa mara nyingi kuandika barua, wamekuwa wakifuatilia lakini hakuna jambo lolote linalofanyika. Naomba commitment ya Serikali, ni lini wananchi hawa watapewa malipo yao?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nafurahi sana Mheshimiwa Doto Biteko amechukua nafasi ya kuwa Mbunge wa Bukombe kwa sababu Mbunge aliyemtangulia alileta kwetu pendekezo kwamba tutangulie kukamilisha ujenzi wa lami wa ile barabara baada ya hapo tushughulikie fidia. Mheshimiwa Doto Biteko anafuatilia sana ulipaji wa fidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia yote mawili tutayafanya lakini naomba sana tena sana tuanze kwanza kukamilisha ile lami. Kwa hiyo, kadiri tutakavyopata fedha kwanza tumalizie lami ambayo tumekusudia kuimaliza hivi karibuni, baada ya hapo, tutaendelea na hilo la fidia kama ambavyo Mbunge aliyemtangulia alikuwa anasisitiza sana na sisi tunapenda kufuata ile continuity.