Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 12 Water and Irrigation Wizara ya Maji 204 2024-02-14

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: -

Je, ni lini Wananchi wa Kata za Nachingwea, Kiegei, Matekwe na Namapwia – Nachingwea, Lihimalya na Kandawale - Kilwa watapatiwa maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika kuboresha huduma ya maji kwenye Kata za Matekwe, Kiegei na Namapwia, Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 inaendelea na zoezi la uchimbaji wa visima vinne ambapo kisima kimoja tayari kimechimbwa katika Kijiji cha Kilimarondo na uchimbaji wa visima vitatu unaendelea na unatarajiwa kukamilika Mwezi Juni, 2024.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Kata ya Nachingwea, Serikali inaendelea na kazi ya usanifu wa mradi pacha toka vyanzo vya Mbwinji na unatarajia kukamilika mwezi Juni, 2024, ambapo utekelezaji wa mradi utaanza katika Mwaka wa Fedha 2024/2025. Aidha, Kwa upande wa Kata ya Kandawale yenye jumla ya Vijiji Vinne, Vijiji viwili vya Kandawale na Mtumbei vinapata huduma ya majisafi na salama kupitia miradi iliyojengwa yenye jumla ya vituo 13. Pia, Vijiji vya Ngarambi na Matewa vinatarajiwa kuchimbiwa visima katika Mwaka wa Fedha 2024/2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Kata ya Lihimalya, Serikali katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 itafanya upanuzi wa Mradi wa Maji wa Pande kwa ajili ya kufikisha huduma ya maji kwenye vijiji vya kata hiyo.