Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 113 2023-11-08

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

Manufaa yatokanayo na kero za Muungano zilizopatiwa ufumbuzi

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza:-

Je, kero 11 za Muungano zilizopatiwa ufumbuzi zimeleta manufaa kiasi gani katika utekelezaji kwa pande zote mbili?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Said Issa, Mbunge wa Jimbo la Konde, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mafanikio yaliyotokana na ufumbuzi wa changamoto 11 za Muungano wa kiuchumi, kijamii na kisiasa hasa katika maeneo ya ajira kwa Watumishi wa Zanzibar wanaofanya kazi katika Taasisi za Muungano, wameendelea kunufaika na ajira hizo ikiwa ni 79% kwa Tanzania Bara na 21% kwa Zanzibar. Mgawanyo wa Fedha za Mapato yatokanayo na Misaada na Mikopo Nafuu ya Kibajeti (GBS) imeendelea kuongezeka tangu kupatiwa ufumbuzi kwa changamoto hii na kuendelea kuimarisha Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa pande zote mbili za Muungano.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Kodi ya Mapato yatokanayo na mishahara ya watumishi wa Taasisi za Muungano zilizopo Zanzibar ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.75 kimekuwa kikitolewa kwenda SMZ kila mwezi kuanzia mwaka 2012/2013 kama malipo ya PAYE; na Kampuni zilizosajiliwa Tanzania Bara na zenye matawi Zanzibar zimeanza kulipa Kodi ya Zuio (Withholding Tax) kwa upande wa Zanzibar. Aidha, mapato yanayotokana na Tozo za VISA kutumika pale yalipokusanywa kama ilivyo kwenye mapato mengine ya Muungano.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja ya kwamba wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili, suala hili limepatiwa ufumbuzi na sasa wafanyabiashara kulipa kodi inayostahiki kwa tathmini ya bidhaa inayotumika Tanzania Bara. Kwa muktadha huo, suala la ulipaji wa tofauti ya kodi kwa bidhaa zinazotoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara imewekwa vizuri kwa wafanyabiashara wa Zanzibar, nakushukuru.