Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 5 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 83 2024-02-05

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatumia drones kusambaza dawa katika Zahanati zetu Vijijini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Jimbo la Kilindi, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilishakamilisha mfumo ambao unahifadhi taarifa zote za vituo kuanzia ngazi ya zahanati hadi Taifa. Mfumo huu utasaidia kupata taarifa za kijiografia (Geo coordinates) za vituo vyote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa tupo kwenye hatua ya kuingiza vituo vyote kwenye mfumo huu ili kuufanyia majaribio na pia kutazama gharama za usafirishaji dawa kupitia mfumo huo wa ndege maalum (drone) ukilinganisha na usafirishaji kwa njia ya magari ili maamuzi sahihi yafanyike katika kutekeleza wazo hili zuri la Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.