Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatumia drones kusambaza dawa katika Zahanati zetu Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya kwa maelezo mazuri tu kwamba ndege hizi zisizokuwa na rubani ni muhimu kwa ajili ya kutoa huduma za kiafya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hali ambayo Watanzania tumeipata ya Mvua za El Nino ni dhahiri kwamba utaratibu huu ni mzuri na unatija kwa Serikali. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, mko tayari kuhakikisha kwamba mfumo huu wa kupeleka dawa vijijini unaharakishwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, tuko tayari na kweli kwa wakati kama huu njia hiyo ni mkombozi hasa ndani ya Wilaya bila kuzungumzia kwa maana ya kutoka Taifa kwenda kwenye Wilaya, lakini kutoka ndani kwenye Wilaya kwenda kwenye vituo utaokoa sana. Tutaendelea kuharakisha tuone tutafika mahali gani, lakini nisiahidi kwamba kwa kipindi gani, ila tunaendelea, kwa sababu coordinate ni muhimu ili kuongoza lile jambo la network.