Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 124 2024-04-19

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-

Je, lini Serikali itaajiri Madereva na Mafundi ambao wamekuwa vibarua wa muda mrefu TANESCO?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekuwa likiajiri watumishi wa kada mbalimbali kwa kuzingatia mahitaji ya kiuendeshaji na uwezo wa kibajeti kwa mwaka husika. Katika ikama na bajeti ya mishahara ya mwaka 2024/2025 pamoja na mambo mengine, shirika limetenga fedha kwa ajili ya nafasi 430 za ajira mpya kwa mchanganuo ufuatao:-

Mheshimiwa Naibu Spika, wahandisi 67, fundi sanifu 135, fundi mchundo 205 na madereva 23. Aidha, ujazaji wa nafasi hizi utazingatia sheria na taratibu katika utumishi wa umma. Ahsante. (Makofi)