Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Je, lini Serikali itaajiri Madereva na Mafundi ambao wamekuwa vibarua wa muda mrefu TANESCO?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kule Tunduru Kusini na Jimbo langu la Nanyumbu tunao madereva pamoja na mafundi sanifu ambao sasa hivi wapo katika ajira za muda kati ya miaka mitano na miaka saba. Je, wizara ipo tayari sasa katika ajira zinazokuja kuwafikiria madereva hawa ambao wamekuwa muda mrefu katika shirika? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, jukumu la kupeleka umeme vijijini lipo chini ya REA. REA jukumu lake ni kupeleka umeme vijijini na baadaye kuwaachia TANESCO kuwaunganishia wateja. Je, Serikali haioni wakati umefika REA baada ya kupeleka umeme vijijini iwaunganishie wateja ndipo iwakabidhi kwa TANESCO wateja wote badala ya kuwaachia TANESCO kufanya kazi ya kuwaunganishia wateja hao? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ajira kwa ajili ya madereva, kwanza niwapongeze Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Mhata na Mheshimiwa Mpakate, kwa kazi nzuri wanazofanya katika majimbo yao. Kuhusiana na ajira za vibarua hawa, kama wizara tunathamini sana mchango wa wafanyakazi wetu vibarua hususani mafundi na madereva. Nataka niwahakikishie kwa kuwa ni wafanyakazi wetu ambao wanafanya kazi kwa jitihada kubwa sana kulitegemeza shirika letu, tutahakikisha ajira zinapotoka wanazingatiwa ipasavyo kulingana na sheria na taratibu za utumishi wa umma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la REA kuendelea na kuunganisha wateja pale ambapo miradi inakamilika. Ushauri wa Mheshimiwa Mbunge tumeupokea na tutauchakata kuona kama unatekelezeka na kama unatekelezeka hatutasita kuufanyia kazi, ahsante. (Makofi)

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Je, lini Serikali itaajiri Madereva na Mafundi ambao wamekuwa vibarua wa muda mrefu TANESCO?

Supplementary Question 2

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wanaotumia umeme wa REA vijijini wamekuwa wakipata changamoto kubwa sana za huduma za haraka pale inapotokea hitilafu ya umeme na hii ni kwa sababu ya mafundi wengi wanakaa Makao Makuu. Swali langu, je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuajiri mafundi hawa maalum kwa ajili ta kitengo cha dharura na kuwasambaza huko vijijini ili wananchi hawa waweze kupata huduma za haraka? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa mawazo mazuri. Nataka nimhakikishie kuhusiana na suala la huduma kwa wateja tayari tumeshaanza kufanyia kazi kuhakikisha tunakitegemeza kitengo hiki ili kiweze kuwa na huduma nzuri kwa wateja. Kuhusiana na suala la mafundi tayari tumekuwa tukiongeza viunga kwenye maeneo ya mbali ili wananchi waweze kupata huduma za uhakika. Kwenye suala la mafundi, kuongeza mafundi Mheshimiwa Mbunge tumelipokea na tutaendelea kulifanyia kazi kuhakikisha wananchi wanapata huduma nzuri. (Makofi)