Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 127 2024-04-19

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa wa Uwanja wa Mpira wa Ali Hassan Mwinyi - Tabora ili utumike AFCON 2027?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa ukarabati wa Uwanja wa Mpira wa Ali Hassan Mwinyi uliopo Tabora pamoja na viwanja vingine hapa nchini na imeendelea kusisitiza wadau na wamiliki wa viwanja kujenga na kutunza miundombinu hiyo sawa na maelekezo ya Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Mwaka 1995 sehemu ya 7(1)-(6).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivi sasa Serikali inajenga na kukarabati viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya AFCON 2027 ambavyo ni Benjamin Mkapa uliopo Dar es Salaam, Amaan Zanzibar na Uwanja mpya wa Dkt. Samia Suluhu Hassan unaojengwa katika Jiji la Arusha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ipo tayari kutoa ushauri wa kitaalam wa namna bora ya kujenga, kukarabati na kuhudumia miundombinu mbalimbali ya michezo kulingana na mahitaji.