Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 135 2024-04-22

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika Zahanati za Buhulyu, Luhumbo, Mambali, Ikindwa, Lukuyi, Mbutu na Karitu – Bukene?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya upungufu wa watumishi wa sekta ya afya katika vituo vya huduma za afya. Hivyo, Serikali imeendelea kuajiri wataalamu wa kada mbalimbali za afya ambapo katika kipindi cha miaka mitatu Serikali imeajiri jumla ya watumishi 18,418 na kuwapangia vituo kote nchini.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023 jumla ya wataalamu 73 waliajiriwa na kupangwa kwenye vituo vya kutolea huduma katika Halmashauri ya Wilaya ya Nzega.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti na kuajiri wataalamu wa kada mbalimbali za afya ili kupunguza pengo hilo, ahsante.