Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika Zahanati za Buhulyu, Luhumbo, Mambali, Ikindwa, Lukuyi, Mbutu na Karitu – Bukene?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameidhinisha ajira mpya 46,000 zikiwemo ajira za kada ya Afya. Je, Serikali itakuwa tayari kutoa commitment hapa kwamba katika hizi ajira mpya 46,000 ambazo ndani yake kuna ajira za kada ya afya, itapeleka angalau mganga mmoja na nesi mmoja kwenye Zahanati za Buhulyu, Luhumbo, Mambali, Ikindwa, Lukuyi, Mbutu na Karitu? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwajali wananchi, tayari Mheshimiwa Rais, ametoa kibali cha ajira za watumishi wa sekta ya afya na pia watumishi wa sekta nyingine.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatoa commitment siku ya leo kwamba kwenye zahanati hizi ambazo zina mtumishi mmoja mmoja, tutahakikisha kwenye ajira hizi ambazo zinafuata tunapeleka watumishi ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi, ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika Zahanati za Buhulyu, Luhumbo, Mambali, Ikindwa, Lukuyi, Mbutu na Karitu – Bukene?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa kada ya Afya kwenye vituo vya afya kumi na Hospitali ya Wilaya na zahanati kumi ambazo hazina watumishi. Ni lini mtapeleka watumishi kwenye Halmashauri hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali ilishafanya tathmini ya maeneo ya halmashauri kote nchini yenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi na katika kile kibali cha ajira kinapotokea maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi yanapewa kipaumbele cha kupelekewa watumishi wengi zaidi kuliko maeneo yale ambayo yana upungufu mdogo zaidi ya watumishi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kakoso kwamba Halmashauri ya Tanganyika na halmashauri nyingine zote zenye maeneo ambayo yana upungufu mkubwa zaidi wa watumishi yatapewa kipaumbele zaidi wakati wa ajira hizi ili watumishi waweze kupelekwa kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi, ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika Zahanati za Buhulyu, Luhumbo, Mambali, Ikindwa, Lukuyi, Mbutu na Karitu – Bukene?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza wauguzi na waganga katika Zahanati ya Makuburi na Mavurunza katika Halmashauri ya Ubungo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge Mariam kwamba tunatambua kwamba vituo hivyo vinahudumia wananchi wengi sana na vinahitaji kuongezewa watumishi. Tayari Serikali imeshatambua pengo la watumishi katika vituo hivyo na katika ajira hizi tutapeleka watumishi. Pia tutaendelea kupeleka watumishi kwa awamu kadri ya vibali vya ajira vinavyojitokeza. Ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika Zahanati za Buhulyu, Luhumbo, Mambali, Ikindwa, Lukuyi, Mbutu na Karitu – Bukene?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Mafinga inahudumia wagonjwa mpaka kutoka Halmashauri ya Mlimba, je, Serikali iko tayari kutuangalia kwa macho mawili na kutuongezea watumishi katika Hospitali ya Mji wa Mafinga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko tayari kuiangalia Hospitali ya Mji wa Mafinga kwa jicho la tatu na kupeleka watumishi zaidi ili wananchi wetu waweze kuhudumiwa vizuri, ahsante.