Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 11 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 146 2024-04-22

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Kyaka Katoro – Ibwera hadi Kyetema Nkenge kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa Barabara ya Kyaka – Katoro – Ibwera hadi Kyetema yenye urefu wa kilometa 60.7 pamoja na daraja la Kalebe kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa taratibu za kutangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi wa kilometa 10 za barabara hiyo kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa daraja la Kalebe zinaendelea na inategemewa zabuni za kazi zitakuwa zimetangazwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2024. Kwa sehemu iliyobaki Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi, ahsante.