Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Kyaka Katoro – Ibwera hadi Kyetema Nkenge kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa commitment ya Serikali katika barabara hiyo na ni kweli, imeshakabidhiwa. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, naomba kujua ujenzi wa barabara katika Jimbo la Nkenge, Wilaya ya Misenyi, Barabara ya Katuma – Bukwali ambayo nimekuwa nikiomba iongezewe bajeti kwa ajili ya kuikamilisha kwa kiwango cha lami, je, ni lini hiyo bajeti itaongezwa ili iweze kukamilika?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, naishukuru Serikali kwamba barabara ya Mutukula kwenda Minziro, mpaka sasa hivi kilometa sita tayari, je, ni lini sasa kile kipande cha kilometa saba kwa wale wananchi kitakamilika? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, Barabara ya Katoma - Bukwali yenye urefu wa kama kilometa 38, tulikuwa tunaijenga kwa awamu na karibu kilometa nane zimekamilika. Hata hivyo, tulichokifanya Serikali ni kumpata Mhandisi Mshauri ili aweze kusanifu barabara yote na tuweze kuijenga yote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mutukula – Minziro, na kwa bahati nzuri hizi barabara zote nimezitembelea, imeshafunguliwa yote kwa maana ya kuifungua ambayo ilikuwa haipo, na sasa tunatengeneza tuta. Tunapoongea sasa, tayari mkandarasi wa kuendelea kutengeneza tuta ameshapatikana ili barabara ipitike mwaka wote ikiwa ni pamoja na kujenga madaraja ambayo yako katika barabara hiyo.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Kyaka Katoro – Ibwera hadi Kyetema Nkenge kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itaongeza pesa kwa Barabara za Nata – Sanzate na Busekela – Mugango hadi Musoma Mjini kwa sababu ni barabara zilizokaa muda mrefu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara ya Sanzate – Nata yenye urefu wa kilometa 40, mkandarasi yuko site anaendelea kujenga, labda tu ni kasi iongezeke. Pia barabara ya Musoma – Busekela yenye urefu wa kilometa 40 inatangazwa mwaka huu ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.