Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Water and Irrigation Wizara ya Maji 384 2024-05-20

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Kijiji cha Chemchem – Karatu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Chemchem unaohusisha ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 135,000 kwenye mnara wa meta sita, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 16.5, ujenzi wa vituo 14 vya kuchotea maji, ujenzi wa ofisi ya CBWSO, ujenzi wa nyumba ya kuendeshea mitambo (pump house), kufunga mfumo wa umeme jua (solar system) pamoja na ujenzi wa mbauti ya kunyweshea mifugo (cattle trough).

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 85% na umeanza kutoa huduma ya maji safi na salama kwenye baadhi ya maeneo ikiwemo; Shule ya Msingi Chemchem, Shule ya Sekondari Chemchem na Zahanati ya Chemchem. Utekelezaji wa mradi huo unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2024 na kunufaisha wananchi wapatao 6,010 wa Kijiji cha Chemchem, ahsante. (Makofi)