Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Kijiji cha Chemchem – Karatu?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa sensa iliyopita, wanufaika wameongezeka katika kijiji hicho na wananchi wamekuwa wanatarajia mradi huu ukamilike kwa wakati kwa sababu umekuwa ni mradi wa muda mrefu sana

Je, ni lini kwa uhakika, kwa sababu kilichopo site na unachokisema kina tofauti kidogo, ni lini kwa uhakika wananchi hawa watarajie kupata mradi huu wa maji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuna wananchi wa vijiji vya jirani ikiwemo Rhotia Juu pamoja na Kilimatembo Juu, ni lini na wananchi hawa wataweza kupata maji kwa sababu vijiji hivyo havina maji? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli natambua na Serikali inatambua uwepo wa changamoto hii katika eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge analiongelea na ni kiu ya Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha kwamba wananchi wa maeneo hayo wanapata huduma ya maji. Ni kweli mradi huu umechukua muda mrefu, ni kweli kabisa kwa sababu ya hatua mbalimbali ambazo zilikuwa zinachukuliwa na Serikali ikiwemo utafutaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba kwa mujibu wa majibu yangu ya msingi, mradi huu unaenda kukamilika Juni, 2024. Kwa hiyo, hiyo ndiyo kauli ya Serikali kuhusiana na mradi huo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika eneo la Kilimatembo pamoja na Rhotia, kuna mradi ambao unaendelea pale, lakini Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kukarabati na kupanua miundombinu ili tufikishe huduma ya maji katika maeneo yanayozunguka katika mradi ule na Kijiji cha Kilimatembo pamoja na Rhotia wataweza kupata huduma ya maji safi na salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Kijiji cha Chemchem – Karatu?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Kata za Kimyaki, Siwandeti, Kiranyi, ambayo ni maeneo yenye wananchi wengi zaidi? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kuhakikisha kwamba watu wanapata accessibility ya maji safi na salama na tuna mpango mkakati wa kuhakikisha kwamba vijiji ambavyo vimebaki havina maji, lakini kulingana na programu ya kila Mbunge kupata vijiji vitano ambavyo vitapata huduma ya maji. Tutaangalia sasa kwamba ni vijiji vingapi ambavyo vitakuwa vimebaki havina huduma ya maji ili Serikali iweke mkakati maalum kwa ajili ya kuhakikisha tunafikisha huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambako miradi ya maji bado haijakamilika, tuna maelekezo mahsusi kutoka kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha kwamba miradi yote ambayo imekwama basi tunaikwamua ili wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Kijiji cha Chemchem – Karatu?

Supplementary Question 3

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nataka kujua ni lini Serikali itapeleka fedha katika Mradi wa Maji Itumba - Isongole ulioko Wilaya ya Ileje ili wananchi waweze kunufaika na maji hayo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Stella kwa kupitisha bajeti yetu ya maji kwa kishindo kabisa, alikuwa anapitisha huduma ya maji kwa wananchi wa Ileje. Kwa kupitisha bajeti hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tunapoingia sasa kwenye utekelezaji, tutapeleka fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba mradi huo unaenda kukamilika na wananchi wapate huduma ya maji safi na salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Kijiji cha Chemchem – Karatu?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; je, ni lini Mradi wa Maji wa Kata ya Ruaha Mbuyuni katika Wilaya ya Kilolo utakarabatiwa? Kwa sababu Mto wa Lukosi ulipochepuka uliondoa mabomba yote kwa hiyo, wananchi wa Ruaha Mbuyuni wanapata shida sana kupata maji safi na salama. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia changamoto ambayo imejitokeza katika mto ule. Ni kweli kabisa Serikali inatambua kuna mabomba ambayo yalipitiwa kulingana na mto jinsi ulivyokuwa umechepuka, lakini pia wakati tunajaribu kuweka jitihada za kurejesha huduma, bado mabomba yalipata changamoto. Serikali imeshatenga fedha na tayari tunanunua mabomba kwa ajili ya kwenda kurekebisha eneo lile ili kurudisha huduma haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imetenga kiasi cha shilingi bilioni 5.56 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu yote ya maji ndani ya Jimbo la Kilolo, ahsante sana. (Makofi)