Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 52 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 463 2022-06-27

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-

Je, hasara na faida gani Taifa linapata kuwa uchumi wa kati na asilimia ngapi ya wananchi wanafahamu na kuishi uchumi wa kati?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Tanzania kuingia kwenye kundi la nchi za uchumi wa pato la kati la chini kunaambatana na fursa pamoja na changamoto mbalimbali. Fursa hizo ni pamoja na kuongezeka kwa wigo wa upatikanaji wa fedha za mikopo ya kibiashara kwa ajili ya miradi ya maendeleo, uhuru wa kupanga matumizi ya fedha za mikopo ya kibiashara, kuchochea uwekezaji kutokana na ukuaji wa wastani wa pato la mtu na mtu, na kuzidi kuaminika katika taasisi za kifedha za Kimataifa kutokana na kutengamaa kwa viashiria vya uchumi.

Mheshimiwa Spika, changamoto ni pamoja na kupungua kwa upatikanaji wa misaada na mikopo yenye masharti nafuu, kuongezeka kwa kiwango cha michango kwa taasisi na mashirika mbalimbali ya Kimataifa. Ni matumaini ya Serikali kupitia juhudi ya vyombo vya habari kuwa wananchi walio wengi wanafahamu kuhusu nchi kuingia katika uchumi wa kati wa chini. Hali hiyo imejidhihirisha kwa kuona mabadiliko chanya kwa mwananchi mmoja mmoja na ushiriki wao katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.